< Isaya 40 >

1 Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu.
Comfort ye, comfort ye, my people, Saith your God.
2 Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.
Speak ye encouragement to Jerusalem, and declare to her, That her hard service is ended; That her iniquity is expiated; That she hath received from the hand of Jehovah Double for all her sins.
3 Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya Bwana, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu.
A voice crieth: “Prepare ye in the wilderness the way of Jehovah; Make straight in the desert a highway for our God!
4 Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa.
Every valley shall be exalted, And every mountain and hill be made low; The crooked shall become straight, And the rough places plain.
5 Utukufu wa Bwana utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”
For the glory of Jehovah shall be revealed, And all flesh shall see it together; For the mouth of Jehovah hath spoken it!”
6 Sauti husema, “Piga kelele.” Nami nikasema, “Nipige kelele gani?” “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao wote ni kama maua ya kondeni.
A voice said, Proclaim! And I said, What shall I proclaim? All flesh is grass, And all its comeliness as the flower of the field.
7 Majani hunyauka na maua huanguka, kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza. Hakika wanadamu ni majani.
The grass withereth, the flower fadeth, When the breath of Jehovah bloweth upon it. Truly the people is grass.
8 Majani hunyauka na maua huanguka, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
The grass withereth, the flower fadeth, But the word of our God shall stand forever.
9 Wewe uletaye habari njema Sayuni, panda juu ya mlima mrefu. Wewe uletaye habari njema Yerusalemu, inua sauti yako kwa kupiga kelele, inua sauti, usiogope; iambie miji ya Yuda, “Yuko hapa Mungu wenu!”
Get thee up on the high mountain, O thou that bringest glad tidings to Zion; Lift up thy voice with strength, thou that bringest glad tidings to Jerusalem; Lift it up; be not afraid; Say to the cities of Judah, Behold your God!
10 Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu, nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake. Tazameni, ujira wake u pamoja naye, nayo malipo yake yanafuatana naye.
Behold, the Lord Jehovah shall come with might, And his arm shall rule for him; Behold, his reward is with him, And his recompense before him.
11 Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo: Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake na kuwachukua karibu na moyo wake, huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.
He shall feed his flock like a shepherd; He shall gather up the lambs in his arms, And carry them in his bosom, And gently lead the nursing ewes.
12 Ni nani aliyepima maji ya bahari kwenye konzi ya mkono wake, au kuzipima mbingu kwa shibiri yake? Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu, au kupima milima kwenye kipimio na vilima kwenye mizani?
Who hath measured the waters in the hollow of his hand, And meted out the heavens with his span, And gathered the dust of the earth into a measure, And weighed the mountains in scales, And the hills in a balance?
13 Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana, au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?
Who hath searched out the spirit of Jehovah, Or, being his counsellor, hath taught him?
14 Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
With whom took he counsel, and who instructed him, And taught him the path of justice, And taught him knowledge, And showed him the way of understanding?
15 Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo, ni kama vumbi jembamba juu ya mizani, huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.
Behold, the nations are as a drop from a bucket, And are accounted as the small dust of the balance; Behold, he taketh up the isles as a very little thing,
16 Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.
And Lebanon is not sufficient for fire, Nor its beasts for a burnt-offering.
17 Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu, yanaonekana yasio na thamani na zaidi ya bure kabisa.
All the nations are as nothing before him; They are accounted by him as less than nothing, and vanity.
18 Basi, utamlinganisha Mungu na nani? Utamlinganisha na kitu gani?
To whom then will ye liken God, And what likeness will ye compare unto him?
19 Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu, naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu na kuitengenezea mikufu ya fedha.
The workman casteth an image, And the smith overlayeth it with gold, And casteth for it silver chains.
20 Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii huuchagua mti usiooza. Humtafuta fundi stadi wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.
He that is too poor to make an oblation Chooseth a piece of wood that will not rot; He seeketh for himself a skilful artificer, To prepare an image that shall not be moved.
21 Je, hujui? Je, hujasikia? Je, hujaambiwa tangu mwanzo? Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?
Do ye not know? Have ye not heard? Hath it not been declared to you from the beginning? Have ye not considered the foundations of the earth?
22 Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia, nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi. Huzitandaza mbingu kama chandarua, na kuzitandaza kama hema la kuishi.
It is He that sitteth above the circle of the earth, And the inhabitants are to him as grasshoppers; That stretcheth out the heavens as a canopy, And spreadeth them out as a tent to dwell in;
23 Huwafanya wakuu kuwa si kitu, na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.
That bringeth princes to nothing, And reduceth the rulers of the earth to vanity.
24 Mara baada ya kupandwa, mara baada ya kutiwa ardhini, mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini, ndipo huwapulizia nao wakanyauka, nao upepo wa kisulisuli huwapeperusha kama makapi.
Yea, scarcely are they planted, scarcely are they sown, Scarcely hath their stem taken root in the ground, When He bloweth upon them and they wither, And the whirlwind beareth them away like stubble.
25 “Utanilinganisha mimi na nani? Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.
To whom then will ye liken me, And to whom shall I be compared? Saith the Holy One.
26 Inueni macho yenu mtazame mbinguni: Ni nani aliyeumba hivi vyote? Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine na kuziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu, hakuna hata mojawapo inayokosekana.
Lift up your eyes to the heavens, and behold! Who hath created these? He draweth forth their host by number, He calleth them all by name; Through the greatness of his strength and the mightiness of his power, Not one of them faileth to appear.
27 Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa Bwana asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?”
Why sayest thou, O Jacob, and speakest, O Israel, “My way is hidden from Jehovah, My cause passeth by before my God”?
28 Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? Bwana ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake.
Do ye not know? Have ye not heard? Jehovah is an everlasting God, The creator of the ends of the earth; He fainteth not, nor is he weary; His understanding is unsearchable.
29 Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu.
He giveth power to the faint; To the feeble abundant strength.
30 Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,
The youths shall faint and be weary, And the young warriors shall utterly fall.
31 bali wale wamtumainio Bwana atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.
But they that trust in Jehovah shall renew their strength; They shall mount up with wings like eagles; They shall run and not be weary; They shall walk and not faint.

< Isaya 40 >