< Isaya 40 >

1 Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu.
Comfort ye, comfort ye my people, saith your God.
2 Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.
Speak ye [comfort] to the heart of Jerusalem, and call out unto her, that her time of sorrow is accomplished, that her iniquity is atoned for; for she hath received from the hand of the Lord double for all her sins.
3 Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya Bwana, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu.
A voice calleth out, In the wilderness make ye clear the way of the Lord, make straight in the desert a highway for God.
4 Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa.
Every valley shall be raised, and every mountain and hill shall be made low; and the crooked shall be made a straight path, and the rough places a plain:
5 Utukufu wa Bwana utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”
And the glory of the Lord shall be revealed; and all flesh shall see it together; for the mouth of the Lord hath spoken it.
6 Sauti husema, “Piga kelele.” Nami nikasema, “Nipige kelele gani?” “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao wote ni kama maua ya kondeni.
A voice saith, Proclaim; and he saith, What shall I proclaim? all flesh is grass, and all its goodliness is as the flower of the field:
7 Majani hunyauka na maua huanguka, kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza. Hakika wanadamu ni majani.
The grass withereth, the flower fadeth; because the breath of the Lord hath blown upon it; surely the people is grass.
8 Majani hunyauka na maua huanguka, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
The grass withereth, the flower fadeth; but the word of our God will stand firm for ever.
9 Wewe uletaye habari njema Sayuni, panda juu ya mlima mrefu. Wewe uletaye habari njema Yerusalemu, inua sauti yako kwa kupiga kelele, inua sauti, usiogope; iambie miji ya Yuda, “Yuko hapa Mungu wenu!”
Upon a high mountain get thee up, thou that bringest good tidings to Zion; lift up with strength thy voice, thou who bringest good tidings to Jerusalem; lift it up, be not afraid; say unto the cities of Judah, Behold, [here is] your God!
10 Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu, nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake. Tazameni, ujira wake u pamoja naye, nayo malipo yake yanafuatana naye.
Behold, the Lord Eternal will come with might, and his arm ruleth for him: behold, his reward is with him, and his recompense before him.
11 Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo: Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake na kuwachukua karibu na moyo wake, huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.
Like a shepherd will he feed his flock: with his arm will he gather the lambs, and in his bosom will he carry them, will he lead gently those that suckle their young.
12 Ni nani aliyepima maji ya bahari kwenye konzi ya mkono wake, au kuzipima mbingu kwa shibiri yake? Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu, au kupima milima kwenye kipimio na vilima kwenye mizani?
Who hath measured in the hollow of his hand the waters, and meted out the heavens with the span, and comprised in a measure the dust of the earth, and weighed in the scale-beam the mountains, and the hills in balances?
13 Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana, au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?
Who hath meted out the Spirit of the Lord? and [who was] his counsellor that he could have given him information?
14 Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
With whom took he counsel, that he gave him understanding, and taught him the path of justice, and taught him knowledge, and caused him to know the way of understanding?
15 Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo, ni kama vumbi jembamba juu ya mizani, huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.
Behold, nations are as a drop out of a bucket, and as the small dust of the balance are they accounted: behold, isles are like the flying dust.
16 Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.
And Lebanon is not sufficient for burning, and its beasts do not suffice for burnt-offering.
17 Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu, yanaonekana yasio na thamani na zaidi ya bure kabisa.
All the nations are as naught before him; less than nothing, and vanity are they accounted to him.
18 Basi, utamlinganisha Mungu na nani? Utamlinganisha na kitu gani?
To whom then will ye liken God? or what likeness will ye compare unto him?
19 Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu, naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu na kuitengenezea mikufu ya fedha.
The graven image the artificer hath cast and the goldsmith hath overspread it with gold, and fabricated [on it] silver chains.
20 Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii huuchagua mti usiooza. Humtafuta fundi stadi wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.
He that is skilled in the choice chooseth a wood that will not rot; he seeketh unto himself a skilful workman to prepare a graven image, that shall not be moved.
21 Je, hujui? Je, hujasikia? Je, hujaambiwa tangu mwanzo? Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?
Know ye not? hath it not been told you from the beginning? have ye not paid attention to the foundations of the earth?
22 Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia, nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi. Huzitandaza mbingu kama chandarua, na kuzitandaza kama hema la kuishi.
[It is he] that dwelleth above the circle of the earth, while its inhabitants are as grasshoppers; that stretched out the heavens as a curtain, and spreadeth them out as a tent to dwell in;
23 Huwafanya wakuu kuwa si kitu, na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.
That bringeth princes to naught; rendering the judges of the earth as vanity.
24 Mara baada ya kupandwa, mara baada ya kutiwa ardhini, mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini, ndipo huwapulizia nao wakanyauka, nao upepo wa kisulisuli huwapeperusha kama makapi.
Yes, they were not yet planted; yea, they were not yet sown; yea, their stem had not yet taken root in the earth: when he but breathed upon them, and they withered, and the storm-wind carrieth them away as stubble.
25 “Utanilinganisha mimi na nani? Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.
To whom then will ye liken me, that I should be equal to? saith the Holy One.
26 Inueni macho yenu mtazame mbinguni: Ni nani aliyeumba hivi vyote? Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine na kuziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu, hakuna hata mojawapo inayokosekana.
Lift up your eyes on high, and see who hath created these? he that bringeth out their host by number; that calleth them all by name; from the Mighty One not one escapeth.
27 Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa Bwana asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?”
Why wilt thou say, O Jacob, and speak, O Israel, My way is hidden from the Lord, and my cause hath passed from the cognizance of my God?
28 Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? Bwana ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake.
Dost thou not know? hast thou not heard? The God of everlasting is the Lord, is the Creator of the ends of the earth; he will not be faint and weary; unsearchable is his understanding.
29 Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu.
He giveth to the faint strength; and to the powerless he imparteth much might.
30 Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,
Though youths should grow faint and be weary, and young men should utterly stumble:
31 bali wale wamtumainio Bwana atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.
Yet they that wait upon the Lord shall acquire new strength, they shall mount up with wings as eagles; they shall run and not be weary, they shall walk, and not become faint.

< Isaya 40 >