< Isaya 40 >
1 Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu.
“Be consoled, be consoled, O my people!” says your God.
2 Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.
Speak to the heart of Jerusalem, and call out to her! For her malice has reached its end. Her iniquity has been forgiven. She has received double for all her sins from the hand of the Lord.
3 Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya Bwana, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu.
The voice of one crying out in the desert: “Prepare the way of the Lord! Make straight the paths of our God, in a solitary place.
4 Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa.
Every valley will be exalted, and every mountain and hill will be brought low. And the crooked will be straightened, and the uneven will become level ways.
5 Utukufu wa Bwana utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”
And the glory of the Lord will be revealed. And all flesh together will see that the mouth of the Lord has spoken.”
6 Sauti husema, “Piga kelele.” Nami nikasema, “Nipige kelele gani?” “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao wote ni kama maua ya kondeni.
The voice of one saying, “Cry out!” And I said, “What should I cry out?” “All flesh is grass, and all its glory is like the flower of the field.
7 Majani hunyauka na maua huanguka, kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza. Hakika wanadamu ni majani.
The grass has dried up, and the flower has fallen. For the Spirit of the Lord has blown over it. Truly, the people are like grass.
8 Majani hunyauka na maua huanguka, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
The grass has dried up, and the flower has fallen. But the Word of our Lord remains for eternity.”
9 Wewe uletaye habari njema Sayuni, panda juu ya mlima mrefu. Wewe uletaye habari njema Yerusalemu, inua sauti yako kwa kupiga kelele, inua sauti, usiogope; iambie miji ya Yuda, “Yuko hapa Mungu wenu!”
You who evangelize Zion, climb a high mountain! You who evangelize Jerusalem, lift up your voice with strength! Lift it up! Do not be afraid! Say to the cities of Judah: “Behold, your God!”
10 Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu, nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake. Tazameni, ujira wake u pamoja naye, nayo malipo yake yanafuatana naye.
Behold, the Lord God will arrive in strength, and his arm will rule. Behold, his reward is with him, and his work is before him.
11 Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo: Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake na kuwachukua karibu na moyo wake, huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.
He will pasture his flock like a shepherd. He will gather together the lambs with his arm, and he will lift them up to his bosom, and he himself will carry the very young.
12 Ni nani aliyepima maji ya bahari kwenye konzi ya mkono wake, au kuzipima mbingu kwa shibiri yake? Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu, au kupima milima kwenye kipimio na vilima kwenye mizani?
Who has measured the waters in the hollow of his hand, and who has weighed the heavens with his palm? Who has suspended the mass of the earth with three fingers, and who has weighed the mountains on a balance and the hills on a scale?
13 Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana, au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?
Who has assisted the Spirit of the Lord? Or who has been his counselor and has revealed things to him?
14 Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
With whom has he consulted? And who has instructed him, and taught him the path of justice, and guided him to knowledge, and revealed the way of understanding to him?
15 Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo, ni kama vumbi jembamba juu ya mizani, huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.
Behold, the nations are like a drop of water in a bucket, and they are considered as the smallest grain on a balance. Behold, the islands are like a little dust.
16 Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.
And Lebanon will not be sufficient to start a fire, and its animals will not be sufficient for a burnt offering.
17 Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu, yanaonekana yasio na thamani na zaidi ya bure kabisa.
All the nations in his sight are as if they did not exist, and they are considered by him as if they were nothingness and emptiness.
18 Basi, utamlinganisha Mungu na nani? Utamlinganisha na kitu gani?
Therefore, to whom would you liken God? Or with what image would you replace him?
19 Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu, naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu na kuitengenezea mikufu ya fedha.
Should the workman cast a statue? Or has the goldsmith formed it with gold, or the silversmith with plates of silver?
20 Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii huuchagua mti usiooza. Humtafuta fundi stadi wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.
He has chosen strong wood that will not decay. The skillful artisan seeks a way to set up an idol that cannot be moved.
21 Je, hujui? Je, hujasikia? Je, hujaambiwa tangu mwanzo? Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?
Do you not know? Have you not heard? Has it not been announced to you from the beginning? Have you not understood the foundations of the earth?
22 Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia, nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi. Huzitandaza mbingu kama chandarua, na kuzitandaza kama hema la kuishi.
He is the One who sits upon the globe of the earth, and its inhabitants are like locusts. He extends the heavens as if they were nothing, and he spreads them out like a tent, in which to dwell.
23 Huwafanya wakuu kuwa si kitu, na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.
He has brought those who examine what is secret to nothingness. He has brought the judges of the earth to emptiness.
24 Mara baada ya kupandwa, mara baada ya kutiwa ardhini, mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini, ndipo huwapulizia nao wakanyauka, nao upepo wa kisulisuli huwapeperusha kama makapi.
And certainly, their stalk was neither planted, nor sown, nor rooted in the ground. He has suddenly blown across them, and they have withered, and a whirlwind will carry them away like chaff.
25 “Utanilinganisha mimi na nani? Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.
“And to whom would you compare me or equate me?” says the Holy One.
26 Inueni macho yenu mtazame mbinguni: Ni nani aliyeumba hivi vyote? Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine na kuziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu, hakuna hata mojawapo inayokosekana.
Lift up your eyes on high, and see who has created these things. He leads forth their army by number, and he calls them all by name. Because of the fullness of his strength and robustness and virtue, not one of them was left behind.
27 Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa Bwana asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?”
Why do you say this, O Jacob, and why do you speak this way, O Israel? “My way has been hidden from the Lord, and my judgment escaped notice by my God.”
28 Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? Bwana ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake.
Do you not know, or have you not heard? The Lord is the eternal God, who has created the limits of the earth. He does not diminish, and he does not struggle. Neither is his wisdom searchable.
29 Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu.
It is he who gives strength to the weary, and it is he who increases fortitude and strength in those who are failing.
30 Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,
Servants will struggle and fail, and young men will fall into infirmity.
31 bali wale wamtumainio Bwana atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.
But those who hope in the Lord will renew their strength. They will take up wings like eagles. They will run and not struggle. They will walk and not tire.