< Isaya 40 >
1 Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu.
Potěšujte, potěšujte lidu mého, dí Bůh váš.
2 Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.
Mluvte k srdci Jeruzaléma, a ohlašujte jemu, že se již doplnil čas uložený jeho, že jest odpuštěna nepravost jeho, a že vzal z ruky Hospodinovy dvojnásobně za všecky hříchy své.
3 Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya Bwana, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu.
Hlas volajícího: Připravtež na poušti cestu Hospodinovu, přímou učiňte na pustině stezku Boha našeho.
4 Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa.
Každé údolí ať jest vyvýšeno, a všeliká hora i pahrbek ať jest snížen; což jest křivého, ať jest přímé, a místa nerovná ať jsou rovinou.
5 Utukufu wa Bwana utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”
Nebo se zjeví sláva Hospodinova, a uzří všeliké tělo spolu, že ústa Hospodinova mluvila.
6 Sauti husema, “Piga kelele.” Nami nikasema, “Nipige kelele gani?” “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao wote ni kama maua ya kondeni.
Hlas řkoucího: Volej. I řekl: Co mám volati? To, že všeliké tělo jest tráva, a všeliká vzácnost jeho jako květ polní.
7 Majani hunyauka na maua huanguka, kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza. Hakika wanadamu ni majani.
Usychá tráva, květ prší, jakž vítr Hospodinův povane na něj. V pravděť jsou lidé ta tráva.
8 Majani hunyauka na maua huanguka, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
Usychá tráva, květ prší, ale slovo Boha našeho zůstává na věky.
9 Wewe uletaye habari njema Sayuni, panda juu ya mlima mrefu. Wewe uletaye habari njema Yerusalemu, inua sauti yako kwa kupiga kelele, inua sauti, usiogope; iambie miji ya Yuda, “Yuko hapa Mungu wenu!”
Na horu vysokou vystup sobě, Sione, zvěstovateli věcí potěšených, povyš mocně hlasu svého, Jeruzaléme, zvěstovateli věcí potěšených, povyš, aniž se boj. Rci městům Judským: Aj, Bůh váš.
10 Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu, nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake. Tazameni, ujira wake u pamoja naye, nayo malipo yake yanafuatana naye.
Aj, Panovník Hospodin proti silnému přijde, a rámě jeho panovati bude nad ním; aj, mzda jeho s ním, a dílo jeho před ním.
11 Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo: Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake na kuwachukua karibu na moyo wake, huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.
Jako pastýř stádo své pásti bude, do náručí svého shromáždí jehňátka, a v klíně svém je ponese, březí pak poznenáhlu povede.
12 Ni nani aliyepima maji ya bahari kwenye konzi ya mkono wake, au kuzipima mbingu kwa shibiri yake? Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu, au kupima milima kwenye kipimio na vilima kwenye mizani?
Kdo změřil hrstí svou vody, a nebesa pídí rozměřil? A kdo změřil měrou prach země, a zvážil na váze hory, a pahrbky na závaží?
13 Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana, au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?
Kdo vystihl ducha Hospodinova, a rádcím jeho byl, že by mu oznámil?
14 Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
S kým se radil, že by mu přidal srozumění, a naučil jej stezce soudu, a vyučil jej umění, a cestu všelijaké rozumnosti jemu v známost uvedl?
15 Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo, ni kama vumbi jembamba juu ya mizani, huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.
Aj, národové jako krůpě od okova, a jako prášek na vážkách se počítají, ostrovy jako nejmenší věc zachvacuje.
16 Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.
Ani Libán nepostačil by k zanícení ohně, a živočichové jeho nepostačili by k zápalné oběti.
17 Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu, yanaonekana yasio na thamani na zaidi ya bure kabisa.
Všickni národové jsou jako nic před ním, za nic a za marnost pokládají se u něho.
18 Basi, utamlinganisha Mungu na nani? Utamlinganisha na kitu gani?
K komu tedy připodobníte Boha silného? A jaké podobenství přirovnáte jemu?
19 Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu, naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu na kuitengenezea mikufu ya fedha.
Jakžkoli rytinu líčí řemeslník, a zlatník zlatem ji potahuje, a řetízky stříbrné k ní slévá;
20 Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii huuchagua mti usiooza. Humtafuta fundi stadi wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.
A ten, kterýž pro chudobu nemá co obětovati, dřevo, kteréž by nepráchnivělo, vybírá, a řemeslníka umělého sobě hledá k přistrojení rytiny, aby se nepohnula.
21 Je, hujui? Je, hujasikia? Je, hujaambiwa tangu mwanzo? Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?
Zdaliž nevíte? Zdaliž neslýcháte? Zdaliž se vám nezvěstuje od počátku? Zdaliž nesrozumíváte z základů země?
22 Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia, nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi. Huzitandaza mbingu kama chandarua, na kuzitandaza kama hema la kuishi.
Ten, kterýž sedí nad okršlkem země, jejížto obyvatelé jako kobylky, kterýž rozprostřel jako kortýnu nebesa, a roztáhl je jako stánek k přebývání,
23 Huwafanya wakuu kuwa si kitu, na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.
Onť přivodí knížata na nic, soudce zemské jako nic rozptyluje,
24 Mara baada ya kupandwa, mara baada ya kutiwa ardhini, mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini, ndipo huwapulizia nao wakanyauka, nao upepo wa kisulisuli huwapeperusha kama makapi.
Tak že nebývají štípeni ani sáti, aniž kořene pouští do země pařez jejich. Nebo jakž jen zavane na ně, hned usychají, a vicher jako plevu zanáší je.
25 “Utanilinganisha mimi na nani? Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.
K komu tedy připodobníte mne, abych podobný byl jemu, praví Svatý?
26 Inueni macho yenu mtazame mbinguni: Ni nani aliyeumba hivi vyote? Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine na kuziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu, hakuna hata mojawapo inayokosekana.
Pozdvihněte zhůru očí svých, a vizte, kdo to stvořil? Kdo vyvodí v počtu vojsko jejich, a všeho toho zejména povolává? Vedlé množství síly a veliké moci ani jedno z nich nehyne.
27 Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa Bwana asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?”
Pročež tedy říkáš, Jákobe, a mluvíš, Izraeli: Skrytať jest cesta má před Hospodinem, a pře má před Boha mého nepřichází?
28 Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? Bwana ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake.
Zdaliž nevíš, zdaž jsi neslýchal, že Bůh věčný Hospodin, kterýž stvořil končiny země, neustává ani zemdlívá, a že vystižena býti nemůže moudrost jeho?
29 Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu.
On dává ustalému sílu, a tomu, ješto žádné síly nemá, moci hojně udílí.
30 Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,
Ustává a umdlévá mládež, a mládenci těžce klesají,
31 bali wale wamtumainio Bwana atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.
Ale ti, jenž očekávají na Hospodina, nabývají nové síly. Vznášejí se peřím jako orlice; běží, a však neumdlévají, chodí, a neustávají.