< Isaya 4 >

1 Katika siku ile wanawake saba watamshika mwanaume mmoja wakisema, “Tutakula chakula chetu wenyewe na kuvaa nguo zetu wenyewe, ila wewe uturuhusu tu tuitwe kwa jina lako. Utuondolee aibu yetu!”
En ce jour-là, sept femmes saisiront un seul homme, en disant: « Nous mangerons notre propre pain, et nous porterons nos propres vêtements. Laisse-nous seulement être appelées par ton nom. Ôte notre opprobre. »
2 Katika siku ile Tawi la Bwana litakuwa zuri na lenye utukufu, nalo tunda la nchi litakuwa fahari na utukufu wa wale Waisraeli watakaonusurika.
En ce jour-là, le rameau de Yahvé sera beau et glorieux, et le fruit du pays sera la beauté et la gloire des survivants d'Israël.
3 Wale watakaoachwa Sayuni, watakaobaki Yerusalemu, wataitwa watakatifu, wale wote ambao wameorodheshwa miongoni mwa walio hai huko Yerusalemu.
Il arrivera que celui qui restera en Sion et celui qui demeurera à Jérusalem seront appelés saints, tous ceux qui seront inscrits parmi les vivants de Jérusalem,
4 Bwana atausafisha uchafu wa wanawake wa Sayuni, atatakasa madoa ya damu kutoka Yerusalemu kwa Roho ya hukumu na Roho ya moto.
quand le Seigneur aura lavé les souillures des filles de Sion et purifié le sang de Jérusalem en son sein, par l'esprit de justice et par l'esprit de feu.
5 Kisha Bwana ataumba juu ya Mlima wote wa Sayuni, na juu ya wale wote wanaokusanyika hapo, wingu la moshi wakati wa mchana, na kungʼaa kwa miali ya moto wakati wa usiku, nako juu ya huo utukufu wote kutatanda kifuniko cha ulinzi.
Yahvé créera sur toute la demeure de la montagne de Sion et sur ses assemblées, une nuée et une fumée le jour, et l'éclat d'un feu ardent la nuit, car il y aura un dais sur toute la gloire.
6 Utakuwa sitara na kivuli kutokana na joto la mchana, na kuwa mahali pa kujificha kutokana na dhoruba na mvua.
Il y aura un pavillon pour faire de l'ombre le jour contre la chaleur, et pour servir de refuge et d'abri contre la tempête et la pluie.

< Isaya 4 >