< Isaya 4 >
1 Katika siku ile wanawake saba watamshika mwanaume mmoja wakisema, “Tutakula chakula chetu wenyewe na kuvaa nguo zetu wenyewe, ila wewe uturuhusu tu tuitwe kwa jina lako. Utuondolee aibu yetu!”
And seven women shall take hold of one man on that day, saying, We will eat our own bread, and wear our own apparel: only let us be called by thy name, take but away our reproach.
2 Katika siku ile Tawi la Bwana litakuwa zuri na lenye utukufu, nalo tunda la nchi litakuwa fahari na utukufu wa wale Waisraeli watakaonusurika.
On that day shall the sprout of the Lord be for ornament and for honor, and the fruit of the land for excellence and for glory for the escaped of Israel.
3 Wale watakaoachwa Sayuni, watakaobaki Yerusalemu, wataitwa watakatifu, wale wote ambao wameorodheshwa miongoni mwa walio hai huko Yerusalemu.
And it shall come to pass, that whoever is left in Zion, and he that remaineth in Jerusalem, shall be called holy, every one that is written down unto life in Jerusalem:
4 Bwana atausafisha uchafu wa wanawake wa Sayuni, atatakasa madoa ya damu kutoka Yerusalemu kwa Roho ya hukumu na Roho ya moto.
When the Lord shall have washed away the filth of the daughters of Zion, and shall have scoured away the blood-guiltiness of Jerusalem from her midst, by the spirit of judgment, and by the spirit of destruction.
5 Kisha Bwana ataumba juu ya Mlima wote wa Sayuni, na juu ya wale wote wanaokusanyika hapo, wingu la moshi wakati wa mchana, na kungʼaa kwa miali ya moto wakati wa usiku, nako juu ya huo utukufu wote kutatanda kifuniko cha ulinzi.
And then will the Lord create upon every dwelling of mount Zion, and upon her places of assembly, a cloud and smoke by day, and the brightness of a flaming fire by night; for over all the glory shall be a covering.
6 Utakuwa sitara na kivuli kutokana na joto la mchana, na kuwa mahali pa kujificha kutokana na dhoruba na mvua.
And a tabernacle shall it be for a shade in the daytime from the heat, and for a refuge, and for a covert from tempest and from rain.