< Isaya 4 >

1 Katika siku ile wanawake saba watamshika mwanaume mmoja wakisema, “Tutakula chakula chetu wenyewe na kuvaa nguo zetu wenyewe, ila wewe uturuhusu tu tuitwe kwa jina lako. Utuondolee aibu yetu!”
Syv Kvinder skal paa hin Dag gribe fat i een Mand og sige: »Vi vil æde vort eget Brød og holde os selv med Klæder, blot vi maa bære dit Navn. Tag Vanæren fra os!«
2 Katika siku ile Tawi la Bwana litakuwa zuri na lenye utukufu, nalo tunda la nchi litakuwa fahari na utukufu wa wale Waisraeli watakaonusurika.
Paa hin Dag Bliver HERRENS Spire til Fryd og Ære og Landets Frugt til Stolthed og Smykke for de undslupne i Israel.
3 Wale watakaoachwa Sayuni, watakaobaki Yerusalemu, wataitwa watakatifu, wale wote ambao wameorodheshwa miongoni mwa walio hai huko Yerusalemu.
Den, som er levnet i Zion og blevet tilovers i Jerusalem, skal kaldes hellig, enhver, der er indskrevet til Livet i Jerusalem,
4 Bwana atausafisha uchafu wa wanawake wa Sayuni, atatakasa madoa ya damu kutoka Yerusalemu kwa Roho ya hukumu na Roho ya moto.
naar Herren faar aftvættet Zions Døtres Smuds og bortskyllet Jerusalems Blodskyld fra dets Midte med Doms og Udrensnings Aand.
5 Kisha Bwana ataumba juu ya Mlima wote wa Sayuni, na juu ya wale wote wanaokusanyika hapo, wingu la moshi wakati wa mchana, na kungʼaa kwa miali ya moto wakati wa usiku, nako juu ya huo utukufu wote kutatanda kifuniko cha ulinzi.
Da skaber Herren over hvert et Sted paa Zions Bjerg og over dets Festforsamlinger en Sky om Dagen og Røg med luende Ildskær om Natten; thi over alt, hvad herligt er, skal der være et Dække
6 Utakuwa sitara na kivuli kutokana na joto la mchana, na kuwa mahali pa kujificha kutokana na dhoruba na mvua.
og Ly til Skygge mod Hede og til Skærm og Skjul mod Skybrud og Regn.

< Isaya 4 >