< Isaya 39 >

1 Wakati huo Merodaki-Baladani, mwana wa Baladani mfalme wa Babeli, akamtumia Hezekia barua na zawadi, kwa sababu alikuwa amesikia habari za kuugua na kupona kwake.
Ob tistem času je babilonski kralj Merodáh Baladán poslal Ezekíju pisma in darilo, kajti slišal je, da je bil bolan in je okreval.
2 Hezekia akawapokea wale wajumbe kwa furaha na kuwaonyesha vitu vile vilivyokuwa katika ghala zake: yaani fedha, dhahabu, vikolezo na mafuta safi, ghala la silaha lote, na kila kitu kilichokuwa katika hazina zake. Hapakuwa na kitu chochote katika jumba lake la kifalme au katika ufalme wake wote ambacho Hezekia hakuwaonyesha.
Ezekíja jih je bil vesel in jim razkazal hišo svojih dragocenih stvari: srebro, zlato, dišave, dragoceno mazilo in vso hišo svoje orožarne in vsega, kar se je našlo v njegovih zakladnicah. Ničesar ni bilo v njegovi hiši niti v vsem njegovem gospostvu, česar jim Ezekíja ni razkazal.
3 Ndipo nabii Isaya akaenda kwa Mfalme Hezekia na kumuuliza, “Watu hao walisema nini, na wametoka wapi?” Hezekia akamjibu, “Wametoka nchi ya mbali. Walikuja kwangu kutoka Babeli.”
Potem je prerok Izaija prišel h kralju Ezekíju in mu rekel: »Kaj so rekli ti možje? In od kod so prišli k tebi?« Ezekíja je rekel: »K meni so prišli iz daljne dežele, celó iz Babilona.«
4 Nabii akauliza, “Waliona nini katika jumba lako la kifalme?” Hezekia akajibu, “Waliona kila kitu katika jumba langu la kifalme. Hakuna kitu chochote katika hazina yangu ambacho sikuwaonyesha.”
Potem je rekel: »Kaj so videli v tvoji hiši?« Ezekíja je odgovoril: »Videli so vse, kar je v moji hiši. Ničesar ni med mojimi zakladi, česar jim ne bi pokazal.«
5 Ndipo Isaya akamwambia Hezekia, “Sikia neno la Bwana Mwenye Nguvu Zote:
Potem Izaija reče Ezekíju: »Poslušaj besedo Gospoda nad bojevniki:
6 Hakika wakati unakuja ambapo vitu vyote katika jumba lako la kifalme, na vyote ambavyo baba zako waliweka akiba mpaka siku hii, vitachukuliwa kwenda Babeli. Hakuna chochote kitakachosalia, asema Bwana.
›Glej, prihajajo dnevi, da bo vse, kar je v tvoji hiši in to, kar so tvoji očetje prihranili v shrambi do tega dne, odneseno v Babilon. Nič ne bo ostalo, ‹ govori Gospod.
7 Nao baadhi ya wazao wako, nyama yako na damu yako mwenyewe watakaozaliwa kwako, watachukuliwa mbali, nao watakuwa matowashi katika jumba la mfalme wa Babeli.”
›In izmed tvojih sinov, ki bodo izšli iz tebe, ki jih boš zaplodil, jih bodo odvedli proč in bodo evnuhi v palači babilonskega kralja.‹«
8 Hezekia akamjibu Isaya, “Neno la Bwana ulilosema ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, “Patakuwepo amani na usalama wakati wa uhai wangu.”
Potem je Ezekíja rekel Izaiju: »Dobra je Gospodova beseda, ki si jo povedal.« Poleg tega je rekel: »Kajti mir in resnica bosta v mojih dneh.«

< Isaya 39 >