< Isaya 39 >
1 Wakati huo Merodaki-Baladani, mwana wa Baladani mfalme wa Babeli, akamtumia Hezekia barua na zawadi, kwa sababu alikuwa amesikia habari za kuugua na kupona kwake.
Ie amy zay, nampañitrike taratasy naho ravoravo am’ Iekizkia t’i Merodak-baladane ana’ i Baladane, mpanjaka’ i Bavele; amy te jinanji’e t’ie natindry vaho nibodañe.
2 Hezekia akawapokea wale wajumbe kwa furaha na kuwaonyesha vitu vile vilivyokuwa katika ghala zake: yaani fedha, dhahabu, vikolezo na mafuta safi, ghala la silaha lote, na kila kitu kilichokuwa katika hazina zake. Hapakuwa na kitu chochote katika jumba lake la kifalme au katika ufalme wake wote ambacho Hezekia hakuwaonyesha.
Nifale t’Iekizkia vaho natoro’e iareo ty trañom-bara’e, ty volafoty, ty volamena, naho o fampafiriañeo, i menake sarotsey naho i trañom-pikalaña’e iabiy naho ze hene nioniñe amo vara’eo; tsy añ’anjomba’e ao ndra am-pifehea’e iaby ty tsy natoro’e.
3 Ndipo nabii Isaya akaenda kwa Mfalme Hezekia na kumuuliza, “Watu hao walisema nini, na wametoka wapi?” Hezekia akamjibu, “Wametoka nchi ya mbali. Walikuja kwangu kutoka Babeli.”
Aa le niheo mb’ am’ Iekizkia mb’eo t’Iesaià nanao ty hoe: Ino ty nisaontsia’ indaty rey? Le aia ty nihirifa’ iareo te nimb’ ama’o? Le hoe t’Iekizkia: Boak’ am-pifelehañe tsietoitane añe t’ie nimb’ amako mb’ etoy; hirike e Bavele añe.
4 Nabii akauliza, “Waliona nini katika jumba lako la kifalme?” Hezekia akajibu, “Waliona kila kitu katika jumba langu la kifalme. Hakuna kitu chochote katika hazina yangu ambacho sikuwaonyesha.”
Le hoe re: Ino ty niisa’ iareo añ’anjomba’o ao? Nanoiñe ty hoe t’Iekizkia: Fonga niisa’ iereo ze añ’anjombako ao, tsy amo varakoo ty tsy nitoroako.
5 Ndipo Isaya akamwambia Hezekia, “Sikia neno la Bwana Mwenye Nguvu Zote:
Aa le hoe t’Iesaià am’ Iekizkia: Janjiño ty tsara’ Iehovà’ i Màroy:
6 Hakika wakati unakuja ambapo vitu vyote katika jumba lako la kifalme, na vyote ambavyo baba zako waliweka akiba mpaka siku hii, vitachukuliwa kwenda Babeli. Hakuna chochote kitakachosalia, asema Bwana.
Toe ho avy ty andro, te hendeseñe mb’e Bavele mb’eo ze he’e añ’ anjomba’o ao naho o vara nahajan-droae’o ho ami’ty andro toio, leo raike tsy hapoke, hoe t’Iehovà.
7 Nao baadhi ya wazao wako, nyama yako na damu yako mwenyewe watakaozaliwa kwako, watachukuliwa mbali, nao watakuwa matowashi katika jumba la mfalme wa Babeli.”
Le o anake hiboak’ ama’oo, o hasama’oo, ro hasese mb’eo ho vositse añ’ anjombam-panjaka’ i Bavele ao.
8 Hezekia akamjibu Isaya, “Neno la Bwana ulilosema ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, “Patakuwepo amani na usalama wakati wa uhai wangu.”
Le hoe ty natoi’ Iekizkia am’ Iesaià: Soa i tsara’ Iehovà nisaontsie’oy, ie nañereñere ty hoe; Amy te hanjo fierañerañañe naho havañonan-draho amo androkoo.