< Isaya 39 >
1 Wakati huo Merodaki-Baladani, mwana wa Baladani mfalme wa Babeli, akamtumia Hezekia barua na zawadi, kwa sababu alikuwa amesikia habari za kuugua na kupona kwake.
In pacl sac pacna Merodach Baladan, tokosra lun acn Babylonia su wen natul Baladan, el lohng lah Tokosra Hezekiah el mas, na el supwala leta se wi mwe kite se nu sel.
2 Hezekia akawapokea wale wajumbe kwa furaha na kuwaonyesha vitu vile vilivyokuwa katika ghala zake: yaani fedha, dhahabu, vikolezo na mafuta safi, ghala la silaha lote, na kila kitu kilichokuwa katika hazina zake. Hapakuwa na kitu chochote katika jumba lake la kifalme au katika ufalme wake wote ambacho Hezekia hakuwaonyesha.
Hezekiah el paing mwet tutafpo inge nu in lohm sel, ac sang elos in liye lupan mwe kasrup lal inge: silver ac gold lal, mwe akyuye mwe mongo ac ono keng lal, ac kufwen mwe mweun nukewa lal. Wangin kutena ma ke nien filma lal, ku kutena acn in tokosrai lal, su el tia sang elos in liye.
3 Ndipo nabii Isaya akaenda kwa Mfalme Hezekia na kumuuliza, “Watu hao walisema nini, na wametoka wapi?” Hezekia akamjibu, “Wametoka nchi ya mbali. Walikuja kwangu kutoka Babeli.”
Tukun ma inge, mwet palu Isaiah el som nu yorol Tokosra Hezekiah ac siyuk, “Mwet inge tuku ya me, ac mea elos fahk nu sum ah?” Hezekiah el topuk, “Elos tuku Babylonia me, sie facl su oan yen loessula.”
4 Nabii akauliza, “Waliona nini katika jumba lako la kifalme?” Hezekia akajibu, “Waliona kila kitu katika jumba langu la kifalme. Hakuna kitu chochote katika hazina yangu ambacho sikuwaonyesha.”
“Mea elos liye inkul sin tokosra?” “Elos liye ma nukewa. Wangin kutena ma in nien filma su nga tia sang elos liye.”
5 Ndipo Isaya akamwambia Hezekia, “Sikia neno la Bwana Mwenye Nguvu Zote:
Na Isaiah el fahk nu sel tokosra, “LEUM GOD Kulana El fahk mu
6 Hakika wakati unakuja ambapo vitu vyote katika jumba lako la kifalme, na vyote ambavyo baba zako waliweka akiba mpaka siku hii, vitachukuliwa kwenda Babeli. Hakuna chochote kitakachosalia, asema Bwana.
pacl se ac fah tuku ke ma nukewa inkul sum uh, ac ma nukewa ma mwet matu lom elos tuh elosak nwe misenge, ac fah utukla nu Babylonia. Wangin ma ac fah oan.
7 Nao baadhi ya wazao wako, nyama yako na damu yako mwenyewe watakaozaliwa kwako, watachukuliwa mbali, nao watakuwa matowashi katika jumba la mfalme wa Babeli.”
Kutu sin tulik na pwaye ke fwilin tulik nutum ac fah utukla in orekla mwet eunuch tuh elos in kulansap ke inkul sin tokosra lun acn Babylonia.”
8 Hezekia akamjibu Isaya, “Neno la Bwana ulilosema ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, “Patakuwepo amani na usalama wakati wa uhai wangu.”
Tokosra Hezekiah el eis mu kalmen ma se inge pa ac fah oasr misla ac wangin lokoalok wacl. Ouinge el fahk, “Wona kas in palu ma kom fahk nu sik sin LEUM GOD inge.”