< Isaya 39 >
1 Wakati huo Merodaki-Baladani, mwana wa Baladani mfalme wa Babeli, akamtumia Hezekia barua na zawadi, kwa sababu alikuwa amesikia habari za kuugua na kupona kwake.
En ce temps-là, Marodach Baladan, fils de Baladan, roi de Babylone, envoya à Ézéchias des lettres, des messagers et des présents, parce qu'il avait appris sa maladie mortelle et sa guérison.
2 Hezekia akawapokea wale wajumbe kwa furaha na kuwaonyesha vitu vile vilivyokuwa katika ghala zake: yaani fedha, dhahabu, vikolezo na mafuta safi, ghala la silaha lote, na kila kitu kilichokuwa katika hazina zake. Hapakuwa na kitu chochote katika jumba lake la kifalme au katika ufalme wake wote ambacho Hezekia hakuwaonyesha.
Et à cause d'eux Ézéchias fut réjoui, et il leur montra la maison de Nechotha, et l'or, et l'argent, les parfums, les aromates et la myrrhe, puis l'arsenal et ses magasins, enfin tout ce qui se trouvait dans ses trésors. Et il n'y eut rien qu'Ézéchias ne fit voir dans son palais et dans ses domaines.
3 Ndipo nabii Isaya akaenda kwa Mfalme Hezekia na kumuuliza, “Watu hao walisema nini, na wametoka wapi?” Hezekia akamjibu, “Wametoka nchi ya mbali. Walikuja kwangu kutoka Babeli.”
Mais le prophète Isaïe alla trouver le roi Ézéchias, et il lui dit: Que vous ont dit ces hommes, et d'où sont-ils venus? Ézéchias répondit: Ils sont venus vers moi d'une contrée lointaine, de Babylone.
4 Nabii akauliza, “Waliona nini katika jumba lako la kifalme?” Hezekia akajibu, “Waliona kila kitu katika jumba langu la kifalme. Hakuna kitu chochote katika hazina yangu ambacho sikuwaonyesha.”
Et le prophète reprit: Qu'ont-ils vu dans ton palais? Et le roi répondit: Ils ont vu tout ce que mon palais renferme; il n'y a rien que je ne leur aie montré, soit dans mon palais, soit dans mes trésors.
5 Ndipo Isaya akamwambia Hezekia, “Sikia neno la Bwana Mwenye Nguvu Zote:
Et le prophète Isaïe dit à Ézéchias: Écoute la parole du Seigneur des armées.
6 Hakika wakati unakuja ambapo vitu vyote katika jumba lako la kifalme, na vyote ambavyo baba zako waliweka akiba mpaka siku hii, vitachukuliwa kwenda Babeli. Hakuna chochote kitakachosalia, asema Bwana.
Voilà que les jours approchent où tout ce que renferme ton palais, tous les trésors que tes pères ont amassés jusqu'à ce moment, seront pris et iront à Babylone, et ils n'en laisseront rien; ainsi l'a dit Dieu.
7 Nao baadhi ya wazao wako, nyama yako na damu yako mwenyewe watakaozaliwa kwako, watachukuliwa mbali, nao watakuwa matowashi katika jumba la mfalme wa Babeli.”
Quant à tes fils que tu as engendrés, ils les prendront, ils les feront eunuques dans le palais du roi de Babylone.
8 Hezekia akamjibu Isaya, “Neno la Bwana ulilosema ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, “Patakuwepo amani na usalama wakati wa uhai wangu.”
Et Ézéchias dit à Isaïe: Juste est la parole que le Seigneur a prononcée; mais que la paix et la justice se maintiennent tous les jours de ma vie.