< Isaya 39 >

1 Wakati huo Merodaki-Baladani, mwana wa Baladani mfalme wa Babeli, akamtumia Hezekia barua na zawadi, kwa sababu alikuwa amesikia habari za kuugua na kupona kwake.
En ce même temps, Mérodach-Baladan fils de Baladan, roi de Babylone, envoya une lettre et des présents à Ezechias, car il avait appris qu'il avait été malade et qu'il était rétabli.
2 Hezekia akawapokea wale wajumbe kwa furaha na kuwaonyesha vitu vile vilivyokuwa katika ghala zake: yaani fedha, dhahabu, vikolezo na mafuta safi, ghala la silaha lote, na kila kitu kilichokuwa katika hazina zake. Hapakuwa na kitu chochote katika jumba lake la kifalme au katika ufalme wake wote ambacho Hezekia hakuwaonyesha.
Ezéchias se réjouit de la venue des envoyés, et il leur montra la maison de son trésor, l'argent et l'or, les aromates et l'huile de prix, tout son arsenal et tout ce qui se trouvait dans ses trésors; il n'y eut rien qu'Ezéchias ne leur fit voir dans sa maison et dans tous ses domaines.
3 Ndipo nabii Isaya akaenda kwa Mfalme Hezekia na kumuuliza, “Watu hao walisema nini, na wametoka wapi?” Hezekia akamjibu, “Wametoka nchi ya mbali. Walikuja kwangu kutoka Babeli.”
Mais Isaïe, le prophète, vint auprès du roi Ezéchias, et lui dit: " Qu'ont dit ces gens-là, et d'où sont-ils venus vers toi? " Ezéchias répondit: " Ils sont venus vers moi d'un pays éloigné, de Babylone. "
4 Nabii akauliza, “Waliona nini katika jumba lako la kifalme?” Hezekia akajibu, “Waliona kila kitu katika jumba langu la kifalme. Hakuna kitu chochote katika hazina yangu ambacho sikuwaonyesha.”
Isaïe dit: " Qu'ont-ils vu dans ta maison? " Et Ezéchias répondit: " Ils ont vu tout ce qui est dans ma maison; il n'y a rien dans mes trésors que je ne leur aie fait voir. "
5 Ndipo Isaya akamwambia Hezekia, “Sikia neno la Bwana Mwenye Nguvu Zote:
Et Isaïe dit à Ezéchias: " Ecoute la parole de Yahweh des armées:
6 Hakika wakati unakuja ambapo vitu vyote katika jumba lako la kifalme, na vyote ambavyo baba zako waliweka akiba mpaka siku hii, vitachukuliwa kwenda Babeli. Hakuna chochote kitakachosalia, asema Bwana.
Voici que des jours viendront où l'on emportera à Babylone tout ce qui est dans ta maison et ce que tes pères ont amassé jusqu'à ce jour; il n'en restera rien, dit Yahweh.
7 Nao baadhi ya wazao wako, nyama yako na damu yako mwenyewe watakaozaliwa kwako, watachukuliwa mbali, nao watakuwa matowashi katika jumba la mfalme wa Babeli.”
Et l'on prendra de tes fils, qui seront sortis de toi, que tu auras engendrés, pour en faire des eunuques dans le palais du roi de Babylone. "
8 Hezekia akamjibu Isaya, “Neno la Bwana ulilosema ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, “Patakuwepo amani na usalama wakati wa uhai wangu.”
Ezéchias répondit à Isaïe: " La parole de Yahweh que tu as prononcée est bonne. " Et il ajouta: " Car, il y aura paix et stabilité pendant ma vie ".

< Isaya 39 >