< Isaya 38 >

1 Katika siku hizo Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Nabii Isaya mwana wa Amozi akaenda kwake na kumwambia, “Hili ndilo asemalo Bwana: Tengeneza mambo ya nyumba yako, kwa sababu utakufa, hutapona.”
Ke pacl se inge Tokosra Hezekiah el masak ac apkuran in misa. Mwet palu Isaiah, wen natul Amoz, el som nu yorol ac fahk nu sel, “LEUM GOD El fahk mu kom in akoela ma nukewa in wo, mweyen kom ac tia kwela. Kom ac misa.”
2 Hezekia akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana:
Hezekiah el forang nu pe sinka uh ac pre:
3 “Ee Bwana, kumbuka jinsi nilivyoenenda mbele zako kwa uaminifu na kujitoa kwa moyo wangu wote, na kufanya yaliyo mema machoni pako.” Naye Hezekia akalia kwa uchungu.
“LEUM GOD, esam lah nga kulansupwekom ke inse pwaye ac suwohs, ac pacl nukewa nga srike na nga in oru ma lungse lom.” Na el mutawauk in tung arulana upa.
4 Ndipo neno la Bwana likamjia Isaya, kusema:
Na LEUM GOD El sap Isaiah elan
5 “Nenda ukamwambie Hezekia, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa baba yako Daudi: Nimeyasikia maombi yako na nimeona machozi yako. Nitakuongezea miaka kumi na mitano katika maisha yako.
folokla nu yorol Hezekiah ac fahk nu sel, “Nga, LEUM GOD lal David, papa matu tomom, lohng pre lom ac liye sroninmotom. Nga ac fah lela nu sum in sifilpa moul ke yac singoul limekosr.
6 Nami nitakuokoa wewe pamoja na mji huu mkononi mwa mfalme wa Ashuru. Nitaulinda mji huu.
Nga fah molikomla ac siti Jerusalem lukel Tokosra Fulat lun Assyria, ac nga fah karinganangna siti se inge.”
7 “‘Hii ndiyo ishara ya Bwana kwako ya kwamba Bwana atafanya kile alichoahidi:
Isaiah el topuk ac fahk, “LEUM GOD El ac sot sie akul nu sum in akpwayei lah El ac liyaung wulela lal.
8 Nitafanya kivuli cha jua kwenye ngazi iliyojengwa na Ahazi kirudi nyuma madaraja kumi.’” Hivyo jua likarudi nyuma madaraja kumi ambayo lilikuwa limeshuka.
Ke nien fan se ma musaiyukla sel Tokosra Ahaz, LEUM GOD El ac oru lulin faht uh in foloki fahluk singoul.” Na lul sac foloki ke fahluk singoul.
9 Maandiko ya Hezekia mfalme wa Yuda baada ya kuugua kwake na kupona:
Tukun Hezekiah el kwela liki mas lal, el simusla on in kaksak soko inge:
10 Nilisema, “Katika ustawi wa maisha yangu, je, ni lazima nipite katika malango ya mauti, na kupokonywa miaka yangu iliyobaki?” (Sheol h7585)
Nga pangon mu nga ac som nu in facl sin mwet misa Ke pacl se nga sun kuiyen moul luk, Ac tiana aksafyela moul luk. (Sheol h7585)
11 Nilisema, “Sitamwona tena Bwana, Bwana katika nchi ya walio hai, wala sitamtazama tena mwanadamu, wala kuwa na wale ambao sasa wanakaa katika ulimwengu huu.
Nga tuh nunku mu in facl sin mwet moul inge Nga fah tiana sifilpa liye LEUM GOD Ku kutena mwet moul.
12 Kama hema la mchunga mifugo, nyumba yangu imebomolewa na kutwaliwa kutoka kwangu. Kama mfumaji nimevingirisha maisha yangu, naye amenikatilia mbali kutoka kitanda cha mfumi. Mchana na usiku uliyakomesha maisha yangu.
Moul luk uh utukla likiyu, Oana sie lohm nuknuk ma tuleyuki, Oana sie nuknuk ma laslasla liki mwe tol nuknuk. Nga nunku mu God El aksafyela moul luk.
13 Nilingoja kwa uvumilivu hadi mapambazuko, lakini alivunja mifupa yangu yote kama simba. Mchana na usiku uliyakomesha maisha yangu.
Nga tung fong nufon se ke ngal, Oana lion soko in koteya sri keik. Nga nunku mu God El aksafyela moul luk.
14 Nililia kama mbayuwayu au korongo, niliomboleza kama hua aombolezaye. Macho yangu yalififia nilipotazama mbinguni. Ee Bwana, ninataabika, njoo unisaidie!”
Pusrek munasla ac srikeni, Ac nga sasao oana sie wule. Atronmutuk totola ke nga nget nu inkusrao. LEUM GOD, moliyula liki mwe lokoalok inge nukewa.
15 Lakini niseme nini? Amesema nami, naye yeye mwenyewe amelitenda hili. Nitatembea kwa unyenyekevu katika miaka yangu yote kwa sababu ya haya maumivu makali ya nafsi yangu.
Mea nga ku in fahk? LEUM GOD pa oru ma inge. Insiuk keoklana, ac nga tia ku in motul.
16 Bwana, kwa mambo kama haya watu huishi, nayo roho yangu hupata uzima katika hayo pia. Uliniponya na kuniacha niishi.
LEUM GOD, nga ac moul nu sum, nu sum mukena; Akeyeyula ac lela nu sik in moul.
17 Hakika ilikuwa ya faida yangu ndiyo maana nikapata maumivu makali. Katika upendo wako ukaniokoa kutoka shimo la uharibifu; umeziweka dhambi zangu zote nyuma yako.
Keok luk fah ekla nu ke inse misla. Kom molela moul luk liki mwe sensen nukewa; Kom sisla ma koluk luk nukewa.
18 Kwa maana kaburi haliwezi kukusifu, mauti haiwezi kuimba sifa zako; wale washukao chini shimoni hawawezi kuutarajia uaminifu wako. (Sheol h7585)
Wangin sie mwet in facl sin mwet misa ku in kaksakin kom; Mwet misa tia ku in lulalfongi ke oaru lom. (Sheol h7585)
19 Walio hai, walio hai: hao wanakusifu, kama ninavyofanya leo. Baba huwaambia watoto wao habari za uaminifu wako.
Mwet moul pa kaksakin kom, Oana ke nga kaksakin kom inge. Papa uh fahk nu sin tulik natulos lupan oaru lom.
20 Bwana ataniokoa, nasi tutaimba kwa vyombo vya nyuzi siku zote za maisha yetu katika Hekalu la Bwana.
LEUM GOD, kom akkeyeyula. Kut fah srital ke harp ac onkakin kom; Kut fah alullul ke on in kaksak in Tempul lom ke lusen moul lasr.
21 Isaya alikuwa amesema, “Tengenezeni dawa ya kubandika ya tini, mweke juu ya jipu, naye atapona.”
Na Isaiah el fahk nu sel tokosra elan apisya ono se orekla ke fokinsak fig nu ke faf kacl ah, na el ac fah kwela.
22 Hezekia alikuwa ameuliza, “Kutakuwa na ishara gani kwamba nitapanda kwenda Hekalu la Bwana?”
Na Tokosra Hezekiah el siyuk, “Akul fuka se ac akpwayei lah nga ac ku in sifilpa som nu in Tempul?”

< Isaya 38 >