< Isaya 37 >

1 Mfalme Hezekia aliposikia haya, akararua nguo zake na kuvaa nguo ya gunia, naye akaenda katika Hekalu la Bwana.
Et il arriva que lorsque le roi Ezéchias les eut entendues, il déchira ses vêtements, et se couvrit d’un sac, et entra dans la maison du Seigneur.
2 Akawatuma Eliakimu msimamizi wa nyumba ya mfalme, Shebna mwandishi, na viongozi wa makuhani, wote wakiwa wamevaa nguo za magunia, waende kwa nabii Isaya mwana wa Amozi.
Et il envoya Eliacim qui était intendant dans la maison, et Sobna, le scribe, et les plus anciens d’entre les prêtres, couverts de sacs, vers Isaïe, le prophète, fils d’Amos,
3 Wakamwambia, “Hili ndilo asemalo Hezekia: Siku hii ni siku ya dhiki, ya kukaripiwa na ya aibu, kama wakati watoto wanapofikia karibu kuzaliwa na kumbe hakuna nguvu ya kuwazaa.
Et ils lui dirent: Voici ce qu’a dit Ezéchias: Jour de tribulation, de reproche et de blasphème, est ce jour-ci, parce que des enfants sont venus jusqu’à l’enfantement, et la force manque à la mère pour enfanter.
4 Yamkini Bwana, Mungu wako atayasikia maneno ya jemadari wa jeshi, ambaye bwana wake, mfalme wa Ashuru, amemtuma kumdhihaki Mungu aliye hai, tena kwamba atamkemea kwa maneno ambayo Bwana, Mungu wako ameyasikia. Kwa hiyo omba kwa ajili ya mabaki ambao bado wako.”
Peut-être que le Seigneur ton Dieu entendra les paroles de Rabsacès qu’a envoyé le roi des Assyriens son maître pour blasphémer le Dieu vivant, et pour l’insulter par les paroles qu’a entendues le Seigneur ton Dieu; fais donc monter une prière pour les restes qui ont été retrouvés.
5 Maafisa wa Mfalme Hezekia walipofika kwa Isaya,
Et les serviteurs du roi Ezéchias vinrent vers Isaïe,
6 Isaya akawaambia, “Mwambieni bwana wenu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Usiogope kwa hayo uliyoyasikia, yale maneno ambayo watumishi wa mfalme wa Ashuru wamenitukana nayo.
Et Isaïe leur dit: Vous direz ceci à votre maître: Voici ce que dit le Seigneur: Ne crains point à cause des paroles que tu as entendues, par lesquelles m’ont blasphémé les serviteurs du roi des Assyriens.
7 Sikiliza! Nitatia roho fulani ndani yake ili kwamba atakaposikia taarifa fulani, atarudi nchi yake mwenyewe, nami huko nitafanya auawe kwa upanga.’”
Voilà que moi je lui enverrai un esprit de frayeur; il apprendra une nouvelle, et il retournera dans sa terre, et je le ferai tomber par le glaive dans sa terre.
8 Jemadari wa jeshi aliposikia kwamba mfalme wa Ashuru ameondoka Lakishi, alirudi, akamkuta mfalme akipigana na Libna.
Or Rabsacès s’en retourna, et trouva le roi des Assyriens formant le siège de Lobna. Car il avait appris qu’il était parti de Lachis,
9 Basi Senakeribu akapata taarifa kwamba Tirhaka, Mkushi mfalme wa Misri, alikuwa anaenda kupigana naye. Aliposikia jambo hili akatuma wajumbe kwa Hezekia na neno hili:
Et Sennachérib entendit, au sujet de Tharaca, roi d’Ethiopie, des gens disant: Il est sorti pour combattre contre vous. Ce qu’ayant entendu, il envoya des messagers à Ezéchias, en disant:
10 “Mwambieni Hezekia mfalme wa Yuda: Usikubali huyo Mungu unayemtumainia akudanganye wakati anaposema, ‘Yerusalemu haitatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru.’
Vous direz ceci à Ezéchias, roi de Juda: Qu’il ne vous trompe pas, votre Dieu, en qui vous vous confiez, disant: Jérusalem, ne sera pas livrée à la main du roi des Assyriens.
11 Hakika umesikia yale ambayo wafalme wa Ashuru wametenda kwa nchi zote, wakiwaangamiza kabisa. Je, wewe utaokolewa?
Voilà que vous-même vous avez appris tout ce qu’ont fait les rois des Assyriens à tous les pays qu’ils ont détruits; et vous, vous pourrez échapper?
12 Je, miungu ya mataifa ambayo yaliangamizwa na baba zangu iliweza kuwaokoa? Yaani miungu ya Gozani, Harani, Resefu, na ya watu wa Edeni waliokuwa Telasari?
Est-ce que les dieux des nations ont délivré ceux qu’ont détruits mes pères, c’est-à-dire Gozam, et Haram, et Réseph, et les fils d’Eden qui étaient en Thalassar?
13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, mfalme wa mji wa Sefarvaimu, au wa Hena au wa Iva?”
Où est le roi d’Emath, et le roi d’Arphad, et le roi de la ville de Sépharvaïm, d’Ana et d’Ava?
14 Hezekia akapokea barua kutoka kwa wale wajumbe naye akaisoma. Kisha akapanda katika Hekalu la Bwana, akaikunjua mbele za Bwana.
Et Ezéchias reçut les livres de la main des messagers, et les lut, et il monta à la maison du Seigneur, et Ezéchias les étendit devant le Seigneur.
15 Naye Hezekia akamwomba Bwana akisema:
Et Ezéchias pria le Seigneur, disant:
16 “Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, uketiye juu ya kiti cha enzi kati ya makerubi, wewe peke yako ndiwe Mungu juu ya falme zote za dunia. Wewe umeumba mbingu na nchi.
Seigneur des armées, Dieu d’Israël, qui êtes assis sur les chérubins, c’est vous qui êtes seul Dieu de tous les royaumes de la terre, c’est vous qui avez fait le ciel et la terre.
17 Tega sikio, Ee Bwana, usikie; fungua macho yako, Ee Bwana, uone; sikiliza maneno yote ambayo Senakeribu ametuma kumtukana Mungu aliye hai.
Inclinez, Seigneur, votre oreille, et écoutez; ouvrez, Seigneur, vos yeux, et voyez, et écoutez toutes les paroles de Sennachérib, qu’il a envoyées pour blasphémer le Dieu vivant.
18 “Ni kweli, Ee Bwana, kwamba wafalme wa Ashuru wameyaangamiza mataifa haya yote pamoja na nchi zao.
Car il est vrai, Seigneur, les rois des Assyriens ont rendu déserts les pays et leurs contrées.
19 Wameitupa miungu yao kwenye moto na kuiangamiza, kwa kuwa haikuwa miungu, bali miti na mawe tu, iliyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
Ils ont jeté leurs dieux au feu; car ce n’étaient pas des dieux, mais des ouvrages de mains d’hommes, du bois et de la pierre; et ils les ont mis en pièces.
20 Sasa basi, Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe kutoka mkononi mwake, ili kwamba falme zote duniani zipate kujua kwamba wewe peke yako, Ee Bwana, ndiwe Mungu.”
Et maintenant, Seigneur notre Dieu, sauvez-nous de sa main; et qu’ils sachent, tous les royaumes de la terre, que c’est vous qui êtes le seul Seigneur.
21 Kisha Isaya mwana wa Amozi akapeleka ujumbe kwa Hezekia, akasema: “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Kwa sababu umeniomba kuhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru,
Et Isaïe, fils d’Amos, envoya vers Ezéchias, disant: Voici ce que dit le Seigneur Dieu d’Israël: À l’égard de ce que tu m’as demandé touchant Sennachérib, roi d’Assyrie,
22 hili ndilo neno ambalo Bwana amelisema dhidi yake: “Bikira binti Sayuni anakudharau na kukudhihaki. Binti Yerusalemu anatikisa kichwa chake unapokimbia.
Voici la parole que le Seigneur a dite à son sujet: Elle t’a méprisé, et elle t’a raillé, la vierge, fille de Sion; derrière toi elle a secoué la tête, la fille de Jérusalem.
23 Ni nani uliyemtukana na kumkufuru? Ni nani uliyeinua sauti yako dhidi yake, na kumwinulia macho yako kwa kiburi? Ni dhidi ya yule Aliye Mtakatifu wa Israeli!
Qui as-tu insulté, qui as-tu blasphémé, et contre qui as-tu élevé la voix, et porté en haut tes yeux? Contre le saint d’Israël.
24 Kupitia kwa wajumbe wako umelundika matukano juu ya Bwana. Nawe umesema, ‘Kwa magari yangu mengi ya vita, nimepanda juu ya vilele vya milima, vilele vya juu sana katika Lebanoni. Nami nimeiangusha mierezi yake mirefu, misunobari yake iliyo bora sana. Nimefikia sehemu zake zilizoinuka juu sana, misitu yake iliyo mizuri sana.
Par l’entremise de tes serviteurs tu as insulté le Seigneur, et tu as dit: Avec la multitude de mes quadriges, moi je suis monté sur la hauteur des montagnes, les chaînes du Liban; je couperai les cimes de ses cèdres, et ses plus beaux sapins, et je pénétrerai jusqu’à la pointe de son sommet, jusqu’à la forêt de son Carmel.
25 Nimechimba visima katika nchi za kigeni na kunywa maji yake. Kwa nyayo za miguu yangu nimekausha vijito vyote vya Misri.’
C’est moi qui ai creusé des sources, et j’ai bu de l’eau, et j’ai séché par la trace de mon pied toutes les rivières retenues par des digues.
26 “Je, hujasikia? Zamani sana niliamuru hili. Siku za kale nilipanga hili; sasa nimelifanya litokee, kwamba umegeuza miji yenye ngome kuwa malundo ya mawe.
N’as-tu donc pas ouï dire les choses qu’autrefois j’y ai faites? dès les temps anciens, c’est moi qui ai disposé cela; et maintenant je l’ai amené et accompli en détruisant les collines qui s’entrechoquent et les cités fortifiées.
27 Watu wa miji hiyo wameishiwa nguvu, wanavunjika mioyo na kuaibishwa. Wao ni kama mimea katika shamba, kama machipukizi mororo ya kijani, kama majani yachipuayo juu ya paa la nyumba, ambayo hukauka kabla ya kukua.
Leurs habitants, à la main raccourcie, ont tremblé et ont été confondus; ils sont devenus comme le foin d’un champ et le gazon d’un pâturage, et l’herbe des toits, qui a séché avant qu’elle fût mûre.
28 “Lakini ninajua mahali ukaapo, kutoka kwako na kuingia kwako, na jinsi unavyoghadhibika dhidi yangu.
Ton habitation, et ta sortie, et ton entrée, je les ai connues, ainsi que ta fureur extravagante contre moi.
29 Kwa sababu unaghadhibika na ufidhuli dhidi yangu, na kwa sababu ufidhuli wako umefika masikioni mwangu, nitaweka ndoana yangu puani mwako na hatamu yangu kinywani mwako, nami nitakufanya urudi kwa njia ile uliyoijia.
Lorsque tu étais furieux contre moi, ton orgueil est monté à mes oreilles; je mettrai donc un cercle à tes narines, et un mors à ta bouche, et je te ramènerai par la voie par laquelle tu es venu.
30 “Hii ndiyo itakuwa ishara kwako, ee Hezekia: “Mwaka huu utakula kile kiotacho chenyewe, na mwaka wa pili utakula kutoka machipukizi yake. Lakini katika mwaka wa tatu panda na uvune, panda mashamba ya mizabibu na ule matunda yake.
Mais pour toi, Ezéchias, voici un signe: Mange cette année de ce qui naîtra de soi-même, et en la seconde année nourris-toi de fruits; mais en la troisième année, semez et moissonnez, et plantez des vignes, et mangez-en le fruit.
31 Mara nyingine tena mabaki ya nyumba ya Yuda wataeneza mizizi chini na kuzaa matunda juu.
Et ce qui sera sauvé de la maison de Juda, et ce qui est resté, jettera racine en bas, et fera du fruit en haut;
32 Kwa kuwa kutoka Yerusalemu watakuja mabaki, na kutoka Mlima Sayuni kundi la walionusurika. Wivu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, ndio utatimiza jambo hili.
Parce que de Jérusalem sortiront des restes, et ce qui sera sauvé de la montagne de Sion; le zèle du Seigneur des armées fera cela.
33 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme wa Ashuru: “Hataingia katika mji huu wala hatapiga mshale hapa. Hatakuja mbele yake na ngao wala kupanga majeshi kuuzingira.
À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur du roi des Assyriens: Il n’entrera pas dans cette cité, il n’y lancera pas de flèche, et pas un bouclier ne l’occupera, et il n’élèvera pas de terrasse autour d’elle.
34 Kwa njia ile aliyoijia ndiyo atakayorudi; hataingia katika mji huu,” asema Bwana.
Il retournera par la voie par laquelle il est venu; il n’entrera pas dans cette cité, dit le Seigneur;
35 “Nitaulinda mji huu na kuuokoa, kwa ajili yangu mwenyewe, na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu!”
Et je protégerai cette cité, afin que je la sauve à cause de moi et à cause de David, mon serviteur.
36 Ndipo malaika wa Bwana akaenda, akawaua wanajeshi 185,000 katika kambi ya Waashuru. Wenzao walipoamka asubuhi yake, walikuta maiti kila mahali!
Or un ange du Seigneur sortit et frappa dans le camp des Assyriens cent quatre-vingt-cinq mille hommes. On se leva le matin, et voici que tous étaient des corps de morts.
37 Basi Senakeribu mfalme wa Ashuru akavunja kambi na kuondoka. Akarudi Ninawi na kukaa huko.
Et il partit, et il s’en alla, et il retourna, Sennachérib, roi des Assyriens, et il habita à Ninive.
38 Siku moja, alipokuwa akiabudu katika hekalu la mungu wake Nisroki, wanawe Adrameleki na Shareza wakamuua kwa upanga, nao wakakimbilia nchi ya Ararati. Naye Esar-Hadoni mwanawe akawa mfalme badala yake.
Et il arriva que, comme il adorait dans le temple de Nesroch, son dieu, Adramélech et Sarasar ses fils le frappèrent du glaive et s’enfuirent dans la terre d’Ararat, et Asarhaddon son fils régna en sa place.

< Isaya 37 >