< Isaya 36 >
1 Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
И бысть во четвертоенадесять лето царствующу Езекии, взыде Сеннахирим царь Ассирийск на грады тверды Иудейски и взя оныя.
2 Kisha mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wa jeshi pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Jemadari wa jeshi akasimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
И посла царь Ассирийск Рапсака от Лахиса во Иерусалим ко царю Езекии с силою великою, и ста у водоважды купели вышния на пути села Кнафеова.
3 Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakamwendea.
И изыде к нему Елиаким сын Хелкиев домостроитель, и Сомнас книгочий, и Иоах сын Асафов памятописец.
4 Jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia, “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
И рече им Рапсак: рцыте Езекии: сия глаголет царь великий, царь Ассирийск: на что уповаеши?
5 Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
Еда советом и словесы устными битва бывает? И ныне на кого уповаеши, яко не покаряешися мне?
6 Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
Се, уповаеши на жезл тростян сокрушенный сей, на Египет, на негоже аще опрется муж, внидет в руку его и прободет ю: тако есть фараон царь Египетский, и вси уповающии на него:
7 Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya”?
аще же глаголете, на Господа Бога нашего уповаем: не сей ли есть, егоже разори Езекиа высокая и требища его, и заповеда Иуде и Иерусалиму: пред олтарем сим поклонитеся?
8 “‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
Ныне соединитеся господину моему царю Ассирийску, и дам вам две тысящы коней, аще можете дати вседающыя на них:
9 Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
и како можете отвратити лице воеводы единаго? Раби суть, иже уповают на Египтян, на коней и всадников:
10 Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza nchi hii bila Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
и ныне еда без Господа приидохом на страну сию, воевати на ню? Господь рече ко мне: взыди на землю сию и погуби ю.
11 Ndipo Eliakimu, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
И рече к нему Елиаким и Сомнас книгочий и Иоах: глаголи к рабом твоим сирски, разумеем бо мы, а не глаголи к нам иудейски: и вскую глаголеши во ушы человеком седящым на стене?
12 Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
И рече к ним Рапсак: еда ко господину вашему, или к вам посла мя господин мой глаголати словеса сия? Не к человеком ли седящым на ограде, да ядят мотыла и пиют мочь с вами вкупе?
13 Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni maneno ya mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
И ста Рапсак, и возопи гласом велиим иудейски и рече: слышите словеса царя великаго, царя Ассирийска:
14 Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa!
сия глаголет царь: да не прельщает вас Езекиа словесы, не может избавити вас:
15 Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
и да не глаголет вам Езекиа, яко избавит вы Бог, и не предастся град сей в руце царя Ассирийска:
16 “Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
не слушайте Езекии: сия глаголет царь Ассирийский: аще хощете благословени быти, изыдите ко мне и ядите кийждо виноград свой и смокви, и пийте от потока вашего,
17 mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na ya mashamba ya mizabibu.
дондеже прииду и поиму вы в землю, яже аки ваша земля, земля пшеницы и вина и хлебов и виноградов:
18 “Msikubali Hezekia awapotoshe asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’ Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
да не прельщает вас Езекиа, глаголя: Бог ваш избавит вы: еда избавиша бози язычестии, кийждо страну свою от руки царя Ассирийска?
19 Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
Где есть бог Емафов и Арфафов? И где бог града Сепфарима? Еда возмогоша избавити Самарию от руки моея?
20 Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
Кто от богов всех языков сих, иже избави землю свою от руки моея, яко избавит Бог Иерусалима от руки моея?
21 Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
И умолкоша, и никтоже отвеща ему словесе, повеления ради царева, да никтоже отвещает.
22 Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.
И вниде Елиаким сын Хелкиев домостроитель, и Сомнас книгочий силы, и Иоах сын Асафов памятописец ко Езекии в растерзаных ризах и поведаша ему словеса Рапсакова.