< Isaya 36 >

1 Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
Or il arriva la quatorzième année du Roi Ezéchias, que Sennachérib, Roi des Assyriens, monta contre toutes les villes closes de Juda, et les prit.
2 Kisha mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wa jeshi pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Jemadari wa jeshi akasimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
Puis le roi des Assyriens envoya Rabsaké avec de grandes forces de Lachis à Jérusalem, vers le roi Ezéchias, et il se présenta près du conduit du haut étang, au grand chemin du champ du foulon.
3 Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakamwendea.
Et Eliakim, fils de Hilkija, Maître d'hôtel, et Sebna le Secrétaire, et Joab fils d'Asaph, commis sur les registres, sortirent vers lui.
4 Jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia, “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
Et Rabsaké leur dit; dites maintenant à Ezéchias; ainsi dit le grand Roi, le Roi des Assyriens; quelle [est] cette confiance que tu as?
5 Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
Je te dis que ce ne sont là que des paroles; [mais] le conseil et la force sont requis à la guerre: or maintenant sur qui t'es-tu confié, que tu te sois rebellé contre moi?
6 Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
Voici, tu t'es confié sur ce bâton qui n'est qu'un roseau cassé, sur l'Egypte, sur lequel si quelqu'un s'appuie, il lui entrera dans la main, et la percera; tel est Pharaon Roi d'Egypte à tous ceux qui se confient en lui.
7 Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya”?
Que si tu me dis; nous nous confions en l'Eternel, notre Dieu; n'est-ce pas celui-là même duquel Ezéchias a ôté les hauts lieux et les autels, et a dit à Juda et à Jérusalem; vous vous prosternerez devant cet autel-ci?
8 “‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
Maintenant donc donne des otages au Roi des Assyriens mon maître; et je te donnerai deux mille chevaux, si tu peux donner autant d'hommes pour monter dessus.
9 Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
Et comment ferais-tu tourner visage au moindre gouverneur d'entre les serviteurs de mon maître? mais tu te confies en l'Egypte, à cause des chariots, et des gens de cheval.
10 Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza nchi hii bila Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
Mais suis-je maintenant monté sans l'Eternel contre ce pays pour le détruire? L'Eternel m'a dit; monte contre ce pays-là, et le détruis.
11 Ndipo Eliakimu, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
Alors Eliakim, et Sebna, et Joab dirent à Rabsaké; nous te prions de parler en langue syriaque à tes serviteurs, car nous l'entendons; mais ne parle point à nous en langue Judaïque, pendant que le peuple, qui est sur la muraille, l'écoute.
12 Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
Et Rabsaké répondit; mon maître m'a-t-il envoyé vers ton maître, ou vers toi, pour dire ces paroles-là? ne m'a-t-il pas envoyé vers les hommes qui se tiennent sur la muraille, pour leur dire qu'ils mangeront leur propre fiente, et qu'ils boiront leur urine avec vous?
13 Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni maneno ya mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
Rabsaké donc se dressa, et s'écria à haute voix en langue Judaïque, et dit; écoutez les paroles du grand Roi, le Roi des Assyriens.
14 Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa!
Le Roi a dit ainsi; qu'Ezéchias ne vous abuse point; car il ne vous pourra pas délivrer.
15 Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
Et qu'Ezéchias ne vous fasse point confier en l'Eternel, en disant; l'Eternel indubitablement nous délivrera; cette ville ne sera point livrée entre les mains du Roi des Assyriens.
16 “Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
N'écoutez point Ezéchias; car ainsi a dit le Roi des Assyriens; faites un accord pour votre bien avec moi, et sortez vers moi, et vous mangerez chacun de sa vigne, et chacun de son figuier, et vous boirez chacun de l'eau de sa citerne;
17 mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na ya mashamba ya mizabibu.
Jusqu'à ce que je vienne, et que je vous emmène en un pays qui est comme votre pays, un pays de froment et de bon vin, un pays de pain et de vignes.
18 “Msikubali Hezekia awapotoshe asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’ Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
Qu'Ezéchias donc ne vous séduise point, en disant; L'Eternel nous délivrera. Les dieux des nations ont-ils délivré chacun leur pays de la main du Roi des Assyriens?
19 Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
Où sont les dieux de Hamath et d'Arpad? où sont les dieux de Sépharvajim? et même a-t-on délivré Samarie de ma main?
20 Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
Qui sont ceux d'entre tous les dieux de ces pays-là qui aient délivré leur pays de ma main, [pour dire] que l'Eternel délivrera Jérusalem de ma main?
21 Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
Mais ils se turent, et ne lui répondirent pas un mot; car le Roi avait commandé, disant; vous ne lui répondrez point.
22 Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.
Après cela Eliakim fils de Hilkija, Maître d'hôtel et Sebna le Secrétaire, et Joab fils d'Asaph, commis sur les registres, s'en revinrent, les vêtements déchirés, vers Ezéchias, et lui rapportèrent les paroles de Rabsaké.

< Isaya 36 >