< Isaya 36 >

1 Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
La quatorzième année du roi Ézéchias, Sennacherib, roi d'Assyrie, attaqua toutes les villes fortifiées de Juda et les captura.
2 Kisha mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wa jeshi pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Jemadari wa jeshi akasimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
Le roi d'Assyrie envoya Rabshakeh de Lakis à Jérusalem auprès du roi Ézéchias avec une grande armée. Il se tenait près de l'aqueduc de l'étang supérieur, sur la route du champ du foulon.
3 Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakamwendea.
Et Éliakim, fils de Hilkija, qui dirigeait la maison, et Shebna, le scribe, et Joach, fils d'Asaph, le secrétaire, sortirent vers lui.
4 Jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia, “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
Rabschaké leur dit: « Dis maintenant à Ézéchias: Le grand roi, le roi d'Assyrie, dit: Quelle est cette confiance en laquelle tu te confies?
5 Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
Je dis que vos conseils et votre force pour la guerre ne sont que de vaines paroles. Et maintenant, en qui vous confiez-vous, puisque vous vous êtes révoltés contre moi?
6 Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
Voici, vous vous confiez dans le bâton de ce roseau meurtri, en Égypte, qui, si un homme s'appuie dessus, entre dans sa main et la transperce. Il en est de même de Pharaon, roi d'Égypte, pour tous ceux qui se confient en lui.
7 Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya”?
Mais si vous me dites: « Nous nous confions en Yahvé notre Dieu », n'est-ce pas lui dont Ezéchias a enlevé les hauts lieux et les autels, et qui a dit à Juda et à Jérusalem: « Vous vous prosternerez devant cet autel »?
8 “‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
Maintenant donc, je te prie de faire un gage à mon maître, le roi d'Assyrie, et je te donnerai deux mille chevaux, si tu es capable de ton côté d'y mettre des cavaliers.
9 Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
Comment donc peux-tu détourner le visage d'un seul des moindres serviteurs de mon maître, et te confier à l'Égypte pour les chars et pour les cavaliers?
10 Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza nchi hii bila Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
Suis-je monté maintenant sans Yahvé contre ce pays pour le détruire? C'est Yahvé qui m'a dit: « Monte contre ce pays, et détruis-le. »"
11 Ndipo Eliakimu, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
Alors Eliakim, Shebna et Joach dirent à Rabshakeh: « Parle à tes serviteurs en araméen, car nous le comprenons. Ne nous parle pas en langue juive à l'oreille des gens qui sont sur la muraille. »
12 Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
Mais Rabschaké dit: « Mon maître m'a-t-il envoyé seulement vers ton maître et vers toi, pour dire ces paroles, et non pas vers les hommes assis sur la muraille, qui mangeront leur propre fumier et boiront leur propre urine avec toi? ».
13 Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni maneno ya mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
Alors Rabschaké se leva et cria d'une voix forte dans la langue des Juifs, et dit: « Écoutez les paroles du grand roi, le roi d'Assyrie!
14 Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa!
Le roi dit: « Ne vous laissez pas tromper par Ézéchias, car il ne pourra pas vous délivrer.
15 Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
Qu'Ézéchias ne vous incite pas à avoir confiance en Yahvé, en disant: « Yahvé nous délivrera. Cette ville ne sera pas livrée entre les mains du roi d'Assyrie ».
16 “Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
N'écoutez pas Ézéchias, car le roi d'Assyrie dit: « Faites la paix avec moi et sortez vers moi; et chacun de vous mangera de sa vigne, chacun de son figuier, et chacun de vous boira l'eau de sa citerne;
17 mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na ya mashamba ya mizabibu.
jusqu'à ce que je vienne et que je vous emmène dans un pays semblable à votre pays, un pays de blé et de vin nouveau, un pays de pain et de vignes.
18 “Msikubali Hezekia awapotoshe asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’ Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
Prenez garde qu'Ézéchias ne vous persuade, en disant: « Yahvé nous délivrera. » Un seul des dieux des nations a-t-il délivré leurs terres de la main du roi d'Assyrie?
19 Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
Où sont les dieux de Hamath et d'Arpad? Où sont les dieux de Sépharvaïm? Ont-ils délivré Samarie de ma main?
20 Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
Qui sont-ils, parmi tous les dieux de ces pays, ceux qui ont délivré leur pays de ma main, pour que Yahvé délivre Jérusalem de ma main? »
21 Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
Mais ils gardèrent le silence et ne répondirent rien, car l'ordre du roi était: « Ne lui répondez pas. »
22 Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.
Alors Éliakim, fils de Hilkija, chef de la maison, et Shebna, le scribe, et Joach, fils d'Asaph, le secrétaire, vinrent auprès d'Ézéchias, les vêtements déchirés, et lui rapportèrent les paroles de Rabschaké.

< Isaya 36 >