< Isaya 36 >

1 Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
I Kong Ezekias's fjortende Regeringsår drog Assyrerkongen Sankerib op mod alle Judas befæstede Byer og indtog dem.
2 Kisha mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wa jeshi pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Jemadari wa jeshi akasimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
Assyrerkoogen sendte så Rasjake med en anselig Styrke fra Lakisj til Kong Ezekias i Jerusalem, og han gjorde Holdt ved Øvredammens Vandledning, ved Vejen til Blegepladsen.
3 Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakamwendea.
Da gik Paladsøversten Eljakim, Hilkijas Søn, Statsskriveren Sjebna og Kansleren Joa, Asafs Søn, ud til ham.
4 Jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia, “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
Rabsjake sagde fil dem: "Sig til Ezekias: Således siger Storkongen, Assyrerkongen: Hvad er det for en Fortrøsfning, du hengiver dig til?
5 Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
Du mener vel, at et blot og bart Ord er det samme som Plan og Styrke i Krig? Og til hvem sætter du egentlig din Lid, siden du gør Oprør imod mig?
6 Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
Se, du sætter din Lid til Ægypten, denne brudte Rørkæp, som river Sår i Hånden på den, der støtter sig til den! Thi således går det alle dem, der sætter deres Lid til Farao, Ægyptens Konge.
7 Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya”?
Men vil du sige til mig: Det er HERREN vor Gud, vi sætter vor Lid til! er det så ikke ham, hvis Offerhøje og Altre Ezekias skaffede bort, da han sagde til Juda og Jerusalem: Foran dette Alter skal I tilbede!
8 “‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
Og nu, indgå et Væddemål med min Herre, Assyrerkongen: Jeg giver dig to Gange tusinde Heste, hvis du kan stille Ryttere til dem!
9 Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
Hvorledes vil du afslå et Angreb af en eneste Statholder, en af min Herres ringeste Tjenere? Og du sætter din Lid til Ægypten, til Vogne og Heste?
10 Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza nchi hii bila Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
Mon det desuden er uden HERRENs Vilje, at jeg er draget op mod dette Land for at ødelægge det? Det var HERREN selv, der sagde til mig: Drag op mod dette Land og ødelæg det!"
11 Ndipo Eliakimu, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
Men Eljakim, Sjebna og Joa sagde til Rabsjake: "Tal dog Aramæisk til dine Trælle, det forstår vi godt; tal ikke Judæisk til os, medens Folkene på Muren hører på det!"
12 Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
Men Rabsjake svarede dem: "Er det til din Herre og dig, min Herre har sendt mig med disse Ord? Er det ikke til de Mænd, der sidder på Muren hos eder og æder deres eget Skarn og drikker deres eget Vand?"
13 Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni maneno ya mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
Og Rabsjake trådte hen og råbte med høj Røst på Judæisk: "Hør Storkongens, Assyrerkongens, Ord!
14 Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa!
Således siger Kongen: Lad ikke Ezekias vildlede eder, thi han er ikke i Stand til at frelse eder!
15 Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
Og lad ikke Ezekias forlede eder til at sætte eders Lid til HERREN, når han siger: HERREN skal sikkert frelse os, og denne By skal ikke overgives i Assyrerkongens Hånd!
16 “Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
Hør ikke på Ezekias, thi så; ledes siger Assyrerkongen: Vil I slutte Fred med mig og overgive eder til mig, så skal enhver af eder spise af sin Vin, stok og sit Figentræ og drikke af sin Brønd,
17 mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na ya mashamba ya mizabibu.
indtil jeg kommer og tager eder med til et Land, der ligner eders, et Land med Korn og Most, et Land med Brød og Vingårde.
18 “Msikubali Hezekia awapotoshe asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’ Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
Lad ikke Ezekias forføre eder med at sige: HERREN vil frelse os! Mon nogen af Folkenes Guder har kunnet frelse sit Land af Assyrerkongens Hånd?
19 Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
Hvor er Hamats og Arpads Guder, hvor er Sefarvajims Guder, hvor er Landet Samarias Guder? Mon de frelste Samaria af min Hånd?
20 Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
Hvor er der blandt alle disse Landes Guder nogen, der har frelst sit Land af min Hånd? Mon da HERREN skulde kunne frelse Jerusalem?"
21 Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
Men de tav og svarede ham ikke et Ord, thi Kongens Bud lød på, at de ikke måtte svare ham.
22 Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.
Derpå gik Paladsøversten Eljakim, Hilkijas Søn, Statsskriveren Sjebna og Kansleren Joa, Asafs Søn, med sønderrevne Klæder til Ezekias og meddelte ham, hvad Rabsjake havde sagt.

< Isaya 36 >