< Isaya 34 >
1 Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize; sikilizeni kwa makini, enyi kabila za watu! Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake, ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!
Zbliżcie się, narody, aby słuchać, i wy, ludy, słuchajcie uważnie! Niech słucha ziemia i to, co ją napełnia, świat i wszystko, co się na nim rodzi.
2 Bwana ameyakasirikia mataifa yote; ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote. Atawaangamiza kabisa, atawatia mikononi mwa wachinjaji.
Bo oburzenie PANA spadło na wszystkie narody, jego zapalczywość – na wszystkie ich wojska. Wytracił je doszczętnie, wydał je na rzeź.
3 Waliouawa watatupwa nje, maiti zao zitatoa uvundo, milima itatota kwa damu zao.
Ich zabici będą porzuceni, a z ich trupów będzie unosił się smród i ich krew z gór popłynie.
4 Nyota zote za mbinguni zitayeyuka na anga litasokotwa kama kitabu, jeshi lote la angani litaanguka kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu, kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.
Cały zastęp niebios stopnieje, a niebiosa jak zwój zostaną zwinięte, całe ich zastępy opadną, jak opada liść z winorośli i jak opada niedojrzały owoc z drzewa figowego.
5 Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni, tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu, wale watu ambao nimeshawahukumu, kuwaangamiza kabisa.
Mój miecz bowiem nasyci się na niebie. Oto spadnie na Edom i na lud, który przekląłem, na sąd.
6 Upanga wa Bwana umeoga katika damu, umefunikwa na mafuta ya nyama: damu ya kondoo na mbuzi, mafuta kutoka figo za kondoo dume. Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra, na machinjo makuu huko Edomu.
Miecz PANA jest pełny krwi, pokrył się tłuszczem i krwią baranków i kozłów, tłuszczem nerek baranich, bo ofiara PANA dokonuje się w Bosra, a wielka rzeź w ziemi Edom.
7 Nyati wataanguka pamoja nao, ndama waume na mafahali wakubwa. Nchi yao italowana kwa damu, nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.
Zstąpią z nimi jednorożce i byki z wołami, ich ziemia nasiąknie krwią, a ich proch nasyci się tłuszczem.
8 Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi, mwaka wa malipo, siku ya kushindania shauri la Sayuni.
To jest bowiem dzień pomsty PANA i rok odpłaty za spór z Syjonem.
9 Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami, mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho, nchi yake itakuwa lami iwakayo!
Potoki obrócą się w smołę, a proch w siarkę, jego ziemia stanie się smołą płonącą.
10 Haitazimishwa usiku wala mchana, moshi wake utapaa juu milele. Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa, hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.
Nie zagaśnie ani w nocy, ani w dzień, jej dym będzie się unosił na wieki. Z pokolenia na pokolenie będzie pustkowiem; na wieki wieków nikt przez nią nie przejdzie.
11 Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki, bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo. Mungu atanyoosha juu ya Edomu kamba ya kupimia ya machafuko matupu, na timazi ya ukiwa.
Ale pelikan i bąk ją posiądą, a sowa i kruk w niej zamieszkają. Rozciągnie on nad nią sznur spustoszenia i próżne wagi.
12 Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote kitakachoitwa ufalme huko, nao wakuu wao wote watatoweka.
Wezwą jej szlachtę na królestwo, ale nie będzie tam żadnego, a wszyscy jej książęta obrócą się wniwecz.
13 Miiba itaenea katika ngome za ndani, viwawi na michongoma itaota kwenye ngome zake. Itakuwa maskani ya mbweha, makao ya bundi.
W ich pałacach wyrosną ciernie, w ich zamkach – pokrzywy i osty. Będzie siedliskiem smoków i dziedzińcem dla strusiów.
14 Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi, nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana; huko viumbe vya usiku vitastarehe pia na kujitafutia mahali pa kupumzika.
Tam będą się spotykać dzikie zwierzęta pustyni ze strasznymi bestiami wysp, a kozice będą się nawoływać; tam leżeć będzie płomykówka i znajdzie dla siebie odpoczynek.
15 Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai, atayaangua na kutunza makinda yake chini ya uvuli wa mabawa yake; pia huko vipanga watakusanyika, kila mmoja na mwenzi wake.
Tam sowa się zagnieździ, zniesie jajka, wyleży [młode] i zbierze je w swoim cieniu. Tam też zlecą się sępy, jeden z drugim.
16 Angalieni katika gombo la Bwana na msome: Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana, hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake. Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza, na Roho wake atawakusanya pamoja.
Szukajcie w księdze PANA i czytajcie. Ani jedno z nich nie przepadnie, żadne z nich nie będzie bez drugiego, bo usta PANA to rozkazały, a jego Duch je zgromadził.
17 Huwagawia sehemu zao, mkono wake huwagawanyia kwa kipimo. Wataimiliki hata milele na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
On też rzucił dla nich los i jego ręka wydzieliła im [to] sznurem mierniczym. Posiadać ją będą na wieki, będą w niej mieszkać z pokolenia na pokolenie.