< Isaya 34 >
1 Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize; sikilizeni kwa makini, enyi kabila za watu! Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake, ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!
Przystąpcie, narody! ku słuchaniu, a wy ludzie pilnie uważajcie! Niech słucha ziemia, i pełność jej, okrąg ziemi, i wszystko, co się rodzi na niej.
2 Bwana ameyakasirikia mataifa yote; ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote. Atawaangamiza kabisa, atawatia mikononi mwa wachinjaji.
Bo rozgniewanie Pańskie jest na wszystkie narody, a popędliwość jego na wszystko wojsko ich; wytraci je jako przeklęte, a poda je na zabicie.
3 Waliouawa watatupwa nje, maiti zao zitatoa uvundo, milima itatota kwa damu zao.
I będą wyrzuceni pobici ich, a z trupów ich smród wynijdzie, a krew ich z gór popłynie.
4 Nyota zote za mbinguni zitayeyuka na anga litasokotwa kama kitabu, jeshi lote la angani litaanguka kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu, kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.
I niszczeć będzie wszystko wojsko niebieskie, a niebiosa jako księgi zwinione będą, i wszystko wojsko ich opadnie, jako opada liść z winnej macicy, i jako opada niedojrzały owoc z figowego drzewa.
5 Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni, tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu, wale watu ambao nimeshawahukumu, kuwaangamiza kabisa.
Albowiem opojony jest na niebie miecz mój; oto zstąpi na Edomczyków, i na sąd ludu przeklętego odemnie.
6 Upanga wa Bwana umeoga katika damu, umefunikwa na mafuta ya nyama: damu ya kondoo na mbuzi, mafuta kutoka figo za kondoo dume. Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra, na machinjo makuu huko Edomu.
Miecz Pański pełny będzie krwi, utłuści się w łoju i we krwi baranków i kozłów, w łoju nerek baranich; bo ofiara Pańska będzie w Bocra, a porażka wielka w ziemi Edomskiej.
7 Nyati wataanguka pamoja nao, ndama waume na mafahali wakubwa. Nchi yao italowana kwa damu, nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.
Zstąpią z nimi i jednorożce, i byki z wołami, i opojona będzie krwią ziemia ich, a proch ich będzie opojony tukiem.
8 Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi, mwaka wa malipo, siku ya kushindania shauri la Sayuni.
Albowiem to dzień pomsty Pańskiej będzie, i rok odpłaty, aby się pomszczono Syonu.
9 Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami, mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho, nchi yake itakuwa lami iwakayo!
I obrócą się potoki jej w smołę, a proch jej w siarkę, a ziemia jej obróci się w smołę gorejącą;
10 Haitazimishwa usiku wala mchana, moshi wake utapaa juu milele. Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa, hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.
Ani w nocy ani we dnie nie zagaśnie, na wieki będzie występował dym jej; od narodu do narodu pustą zostanie; na wieki wieczne nie będzie, ktoby szedł przez nią.
11 Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki, bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo. Mungu atanyoosha juu ya Edomu kamba ya kupimia ya machafuko matupu, na timazi ya ukiwa.
Ale ją pelikan i bąk posiędą, a sowa i kruk mieszkać w niej będą; i rozciągnie po niej sznur spustoszenia, i wagi próżności.
12 Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote kitakachoitwa ufalme huko, nao wakuu wao wote watatoweka.
Szlachty jej na królestwo wzywać będą, ale nie będzie tam żadnego; bo wszyscy książęta jej wniwecz się obrócą.
13 Miiba itaenea katika ngome za ndani, viwawi na michongoma itaota kwenye ngome zake. Itakuwa maskani ya mbweha, makao ya bundi.
I urosną na pałacach ich ciernie, pokrzywy i oset na zamkach ich; i będzie przybytkiem smoków, a mieszkaniem strusiów.
14 Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi, nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana; huko viumbe vya usiku vitastarehe pia na kujitafutia mahali pa kupumzika.
Tam się będą potykały dzikie zwierzęta z koczkodanami, i pokusa jedna drugiej ozywać się będzie; tam leżeć będzie jędza, a znajdzie sobie odpocznienie.
15 Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai, atayaangua na kutunza makinda yake chini ya uvuli wa mabawa yake; pia huko vipanga watakusanyika, kila mmoja na mwenzi wake.
Tam sobie sęp gniazdo uczyni, zniesie jajka, i wylęże, a schowa pod cień swój; tamże się zlecą kanie jedna do drugiej.
16 Angalieni katika gombo la Bwana na msome: Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana, hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake. Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza, na Roho wake atawakusanya pamoja.
Szukajcież w księgach Pańskich, a czytajcie; ani jedno z tych nie uchybi, a jedno bez drugiego nie będzie; albowiem usta Pańskie to rozkazały, a duch jego sam zgromadzi je.
17 Huwagawia sehemu zao, mkono wake huwagawanyia kwa kipimo. Wataimiliki hata milele na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
Bo im on los rzucił, a ręka jego onę im sznurem rozmierzyła; aż na wieki dziedzicznie ją posiądą, od narodu do narodu mieszkać w niej będą.