< Isaya 34 >

1 Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize; sikilizeni kwa makini, enyi kabila za watu! Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake, ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!
ای قومهای روی زمین نزدیک آیید و به این پیام گوش دهید. ای مردم دنیا، سخنان مرا بشنوید:
2 Bwana ameyakasirikia mataifa yote; ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote. Atawaangamiza kabisa, atawatia mikononi mwa wachinjaji.
خداوند بر تمام قومها و سپاهیانشان خشمگین است. او آنها را به مرگ محکوم کرده است و آنها را خواهد کشت.
3 Waliouawa watatupwa nje, maiti zao zitatoa uvundo, milima itatota kwa damu zao.
جنازه‌های آنان دفن نخواهند شد و بوی تعفن آنها زمین را پر خواهد ساخت و خون ایشان از کوهها جاری خواهد گردید.
4 Nyota zote za mbinguni zitayeyuka na anga litasokotwa kama kitabu, jeshi lote la angani litaanguka kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu, kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.
خورشید و ماه نابود خواهند شد و آسمان مثل طوماری به هم خواهد پیچید. ستارگان مانند برگ مو و همچون میوه‌های رسیده که از درخت می‌افتند، فرو خواهند ریخت.
5 Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni, tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu, wale watu ambao nimeshawahukumu, kuwaangamiza kabisa.
خداوند شمشیر خود را در آسمان آماده کرده است تا بر قوم ادوم که مورد غضب او هستند، فرود آورد.
6 Upanga wa Bwana umeoga katika damu, umefunikwa na mafuta ya nyama: damu ya kondoo na mbuzi, mafuta kutoka figo za kondoo dume. Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra, na machinjo makuu huko Edomu.
شمشیر خداوند از خون آنها پوشیده خواهد شد و آنها را مانند بره و بزغالهٔ ذبحی، سر خواهد برید. بله، خداوند در سرزمین ادوم مذبح بزرگی ترتیب خواهد داد و کشتار عظیمی به راه خواهد انداخت.
7 Nyati wataanguka pamoja nao, ndama waume na mafahali wakubwa. Nchi yao italowana kwa damu, nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.
نیرومندان هلاک خواهند شد، جوانان و اشخاص کارآزموده از بین خواهند رفت. زمین از خون سیراب و خاک از چربی حاصلخیز خواهد گردید.
8 Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi, mwaka wa malipo, siku ya kushindania shauri la Sayuni.
زیرا آن روز، روز انتقام گرفتن از ادوم است و سال تلافی کردن ظلمهایی که به اسرائیل کرده است.
9 Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami, mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho, nchi yake itakuwa lami iwakayo!
نهرهای ادوم پر از قیر گداخته و زمین آن از آتش پوشیده خواهد شد.
10 Haitazimishwa usiku wala mchana, moshi wake utapaa juu milele. Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa, hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.
ادوم روز و شب خواهد سوخت و تا ابد دود از آن برخواهد خاست؛ نسل اندر نسل، ویران خواهد ماند و دیگر کسی در آنجا زندگی نخواهد کرد،
11 Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki, bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo. Mungu atanyoosha juu ya Edomu kamba ya kupimia ya machafuko matupu, na timazi ya ukiwa.
جغدها و کلاغها آن سرزمین را اشغال خواهند نمود؛ زیرا خداوند ادوم را به نابودی محکوم کرده است.
12 Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote kitakachoitwa ufalme huko, nao wakuu wao wote watatoweka.
از طبقهٔ اشراف کسی باقی نخواهد ماند تا بتواند پادشاه شود. تمام رهبرانش از بین خواهند رفت.
13 Miiba itaenea katika ngome za ndani, viwawi na michongoma itaota kwenye ngome zake. Itakuwa maskani ya mbweha, makao ya bundi.
قصرها و قلعه‌هایش پوشیده از خار خواهند شد و شغالها و شترمرغها در آنجا لانه خواهند کرد.
14 Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi, nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana; huko viumbe vya usiku vitastarehe pia na kujitafutia mahali pa kupumzika.
حیوانات وحشی در ادوم گردش خواهند کرد و زوزهٔ آنها در شب، همه جا خواهد پیچید. هیولاهای شب بر سر یکدیگر فریاد خواهند زد و غولها برای استراحت به آنجا خواهند رفت.
15 Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai, atayaangua na kutunza makinda yake chini ya uvuli wa mabawa yake; pia huko vipanga watakusanyika, kila mmoja na mwenzi wake.
در آنجا جغدها آشیانه خواهند کرد، تخم خواهند گذاشت، جوجه‌هایشان را از تخم بیرون خواهند آورد و آنها را زیر بال و پر خود پرورش خواهند داد. لاشخورها با جفتهای خود در آنجا جمع خواهند شد.
16 Angalieni katika gombo la Bwana na msome: Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana, hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake. Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza, na Roho wake atawakusanya pamoja.
کتاب خداوند را مطالعه و بررسی کنید و از آنچه که او انجام خواهد داد آگاه شوید. تمام جزئیات این کتاب واقع خواهد شد. هیچ لاشخوری بدون جفت در آن سرزمین نخواهد بود خداوند این را فرموده است و روح او به آن جامهٔ عمل خواهد پوشاند.
17 Huwagawia sehemu zao, mkono wake huwagawanyia kwa kipimo. Wataimiliki hata milele na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
خداوند این سرزمین را پیموده و تقسیم کرده و آن را به این جانوران واگذار نموده است تا برای همیشه، نسل اندر نسل در آن زندگی کنند.

< Isaya 34 >