< Isaya 34 >
1 Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize; sikilizeni kwa makini, enyi kabila za watu! Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake, ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!
Nāciet klāt, pagāni, klausīties, un tautas, ņemiet vērā! Lai dzird zeme un kas tur mīt, pasaule un viss, kas tur rodas!
2 Bwana ameyakasirikia mataifa yote; ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote. Atawaangamiza kabisa, atawatia mikononi mwa wachinjaji.
Jo Tā Kunga dusmība ir pār visiem pagāniem un bardzība pār visu viņu pulku; Viņš tos izdeldēs un tos nodos uz kaušanu.
3 Waliouawa watatupwa nje, maiti zao zitatoa uvundo, milima itatota kwa damu zao.
Un viņu nokautie taps nosviesti, un no viņu līķiem celsies smaka, un kalni izkusīs no viņu asinīm.
4 Nyota zote za mbinguni zitayeyuka na anga litasokotwa kama kitabu, jeshi lote la angani litaanguka kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu, kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.
Un viss debesu pulks iznīkst, un debesis top satītas kā grāmatu rullis, un viss viņu pulks savīst, tā kā lapas vīst pie vīnakoka, un kā tās vīst pie vīģes koka.
5 Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni, tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu, wale watu ambao nimeshawahukumu, kuwaangamiza kabisa.
Jo Mans zobens ir dusmu pilns debesīs; redzi, tas nolaidīsies par sodību uz Edomu un uz tiem ļaudīm, ko Es izdeldēšu.
6 Upanga wa Bwana umeoga katika damu, umefunikwa na mafuta ya nyama: damu ya kondoo na mbuzi, mafuta kutoka figo za kondoo dume. Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra, na machinjo makuu huko Edomu.
Tā Kunga zobens aptraipās asinīm un taukiem, jēru un āžu asinīm, aunu īkšķu(nieru) taukiem; jo Tam Kungam ir upurēšana Bocrā un liela kaušana Edoma zemē.
7 Nyati wataanguka pamoja nao, ndama waume na mafahali wakubwa. Nchi yao italowana kwa damu, nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.
Tad sumbri līdz ar viņiem kritīs pie zemes, un jauni vērši līdz ar barotiem, un viņu zeme būs piedzērusies no asinīm un viņu pīšļi taps trekni no taukiem.
8 Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi, mwaka wa malipo, siku ya kushindania shauri la Sayuni.
Jo šī būs atriebšanas diena Tam Kungam, atmaksāšanas gads, lai Ciāna dabū taisnību.
9 Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami, mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho, nchi yake itakuwa lami iwakayo!
Un (Edoma) upes pārvērtīsies par darvu un viņa pīšļi par sēru, un viņa zeme taps par degošu darvu.
10 Haitazimishwa usiku wala mchana, moshi wake utapaa juu milele. Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa, hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.
Ne nakti, ne dienu tas neizdzisīs, bet viņas dūmi uzkāps mūžīgi, līdz cilšu ciltīm tā būs postā, neviens tur nestaigās ne mūžam.
11 Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki, bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo. Mungu atanyoosha juu ya Edomu kamba ya kupimia ya machafuko matupu, na timazi ya ukiwa.
Bet pelikāns un ezis to iemantos, un pūce un krauklis tur mājos; jo viņš to atmēros tuksnesim un nosvērs postam.
12 Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote kitakachoitwa ufalme huko, nao wakuu wao wote watatoweka.
Viņas cienīgie, - tiem vairs nebūs ķēniņa, ko lai izsauc, un visi viņas lielkungi būs par nieku.
13 Miiba itaenea katika ngome za ndani, viwawi na michongoma itaota kwenye ngome zake. Itakuwa maskani ya mbweha, makao ya bundi.
Un viņas skaistos namos uzdīgs ērkšķi, nātres un dadži viņas pilīs, un būs mājas vieta vilkiem un pagalms jauniem strausiem.
14 Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi, nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana; huko viumbe vya usiku vitastarehe pia na kujitafutia mahali pa kupumzika.
Tur satiekās tuksneša vilki un šakāļi, un jods(āžkāja) brēc uz jodu, ir nakts biedēklis tur apmetīsies un dusēs.
15 Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai, atayaangua na kutunza makinda yake chini ya uvuli wa mabawa yake; pia huko vipanga watakusanyika, kila mmoja na mwenzi wake.
Un tas lēkātājs zalktis tur darīs ligzdu un dēs un perēs un sapulcinās savu perēkli apakš savas ēnas, arī vanagi viens ar otru tur pulcēsies.
16 Angalieni katika gombo la Bwana na msome: Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana, hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake. Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza, na Roho wake atawakusanya pamoja.
Meklējiet Tā Kunga grāmatā un lasiet! Neviena no tiem netrūkst, tie visi sarodas kopā; jo (Tā Kunga) mute to ir pavēlējusi, un Viņa Gars tos sapulcinās.
17 Huwagawia sehemu zao, mkono wake huwagawanyia kwa kipimo. Wataimiliki hata milele na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
Un Viņš pats tiem to daļu nolēmis, un Viņa roka tiem to ir nomērojusi par tiesu, mūžam tie to paturēs, uz dzimumu dzimumiem tie tur mitīs.