< Isaya 34 >

1 Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize; sikilizeni kwa makini, enyi kabila za watu! Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake, ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!
Neiye, ye hethene men, and here; and ye puplis, perseyue; the erthe, and the fulnesse therof, the world, and al buriownyng therof, here ye.
2 Bwana ameyakasirikia mataifa yote; ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote. Atawaangamiza kabisa, atawatia mikononi mwa wachinjaji.
For whi indignacioun of the Lord is on alle folkis, and strong veniaunce on al the chyualrie of hem; he killide hem, and yaf hem in to sleyng.
3 Waliouawa watatupwa nje, maiti zao zitatoa uvundo, milima itatota kwa damu zao.
The slayn men of hem schulen be cast forth, and stynk schal stie of the careyns of hem; hillis schulen flete of the blood of hem.
4 Nyota zote za mbinguni zitayeyuka na anga litasokotwa kama kitabu, jeshi lote la angani litaanguka kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu, kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.
And al the chyualrie of heuenys schal faile, and heuenys schulen be foldid togidere as a book, and al the knyythod of tho schal flete doun, as the leef of a vyner and of a fige tre fallith doun.
5 Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni, tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu, wale watu ambao nimeshawahukumu, kuwaangamiza kabisa.
For my swerd is fillid in heuene; lo! it schal come doun on Ydumee, and on the puple of my sleyng, to doom.
6 Upanga wa Bwana umeoga katika damu, umefunikwa na mafuta ya nyama: damu ya kondoo na mbuzi, mafuta kutoka figo za kondoo dume. Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra, na machinjo makuu huko Edomu.
The swerd of the Lord is fillid of blood, it is maad fat of the ynner fatnesse of the blood of lambren and of buckis of geet, of the blood of rammes ful of merow; for whi the slayn sacrifice of the Lord is in Bosra, and greet sleyng is in the lond of Edom.
7 Nyati wataanguka pamoja nao, ndama waume na mafahali wakubwa. Nchi yao italowana kwa damu, nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.
And vnycornes schulen go doun with hem, and bolis with hem that ben myyti; the lond of hem schal be fillid with blood, and the erthe of hem with ynnere fatnesse of fatte beestis;
8 Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi, mwaka wa malipo, siku ya kushindania shauri la Sayuni.
for it is a dai of veniaunce of the Lord, a yeer of yeldyng of the dom of Sion.
9 Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami, mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho, nchi yake itakuwa lami iwakayo!
And the strondis therof schulen be turned in to pitche, and the erthe therof in to brymstoon; and the lond therof schal be in to brennyng pitch, niyt and dai.
10 Haitazimishwa usiku wala mchana, moshi wake utapaa juu milele. Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa, hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.
It schal not be quenchid withouten ende, the smoke therof schal stie fro generacioun in to generacioun, and it schal be desolat in to worldis of worldis; noon schal passe therbi.
11 Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki, bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo. Mungu atanyoosha juu ya Edomu kamba ya kupimia ya machafuko matupu, na timazi ya ukiwa.
And onocrotalus, and an irchoun schulen welde it; and a capret, and a crowe schulen dwelle therynne; and a mesure schal be stretchid forth theronne, that it be dryuun to nouyt, and an hangynge plomet in to desolacyoun.
12 Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote kitakachoitwa ufalme huko, nao wakuu wao wote watatoweka.
The noble men therof schulen not be there; rathere thei schulen clepe the kyng in to help, and alle the princes therof schulen be in to nouyt.
13 Miiba itaenea katika ngome za ndani, viwawi na michongoma itaota kwenye ngome zake. Itakuwa maskani ya mbweha, makao ya bundi.
And thornes and nettlis schulen growe in the housis therof, and a tasil in the strengthis therof; and it schal be the couche of dragouns, and the lesewe of ostrichis.
14 Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi, nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana; huko viumbe vya usiku vitastarehe pia na kujitafutia mahali pa kupumzika.
And fendis, and wondurful beestis, lijk men in the hiyere part and lijk assis in the nethir part, and an heeri schulen meete; oon schal crie to an other.
15 Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai, atayaangua na kutunza makinda yake chini ya uvuli wa mabawa yake; pia huko vipanga watakusanyika, kila mmoja na mwenzi wake.
Lamya schal ligge there, and foond rest there to hir silf; there an irchoun hadde dichis, and nurschide out whelpis, and diggide aboute, and fostride in the schadewe therof; there kitis weren gaderid togidere, oon to another.
16 Angalieni katika gombo la Bwana na msome: Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana, hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake. Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza, na Roho wake atawakusanya pamoja.
Seke ye diligentli in the book of the Lord, and rede ye; oon of tho thingis failide not, oon souyte not another; for he comaundide that thing, that goith forth of my mouth, and his spirit he gaderide tho togidere.
17 Huwagawia sehemu zao, mkono wake huwagawanyia kwa kipimo. Wataimiliki hata milele na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
And he sente to hem eritage, and his hond departide it in mesure; til in to withouten ende tho schulen welde that lond, in generacioun and in to generacioun tho schulen dwelle ther ynne.

< Isaya 34 >