< Isaya 34 >

1 Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize; sikilizeni kwa makini, enyi kabila za watu! Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake, ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!
to present: come nation to/for to hear: hear and people to listen to hear: hear [the] land: country/planet and fullness her world and all offspring her
2 Bwana ameyakasirikia mataifa yote; ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote. Atawaangamiza kabisa, atawatia mikononi mwa wachinjaji.
for wrath to/for LORD upon all [the] nation and rage upon all army their to devote/destroy them to give: give them to/for slaughter
3 Waliouawa watatupwa nje, maiti zao zitatoa uvundo, milima itatota kwa damu zao.
and slain: killed their to throw and corpse their to ascend: rise stench their and to melt mountain: mount from blood their
4 Nyota zote za mbinguni zitayeyuka na anga litasokotwa kama kitabu, jeshi lote la angani litaanguka kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu, kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.
and to rot all army [the] heaven and to roll like/as scroll: document [the] heaven and all army their to wither like/as to wither leaf from vine and like/as to wither from fig
5 Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni, tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu, wale watu ambao nimeshawahukumu, kuwaangamiza kabisa.
for to quench in/on/with heaven sword my behold upon Edom to go down and upon people devoted thing my to/for justice: judgement
6 Upanga wa Bwana umeoga katika damu, umefunikwa na mafuta ya nyama: damu ya kondoo na mbuzi, mafuta kutoka figo za kondoo dume. Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra, na machinjo makuu huko Edomu.
sword to/for LORD to fill blood to prosper from fat from blood ram and goat from fat kidney ram for sacrifice to/for LORD in/on/with Bozrah and slaughter great: large in/on/with land: country/planet Edom
7 Nyati wataanguka pamoja nao, ndama waume na mafahali wakubwa. Nchi yao italowana kwa damu, nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.
and to go down wild ox with them and bullock with mighty: ox and to quench land: country/planet their from blood and dust their from fat to prosper
8 Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi, mwaka wa malipo, siku ya kushindania shauri la Sayuni.
for day vengeance to/for LORD year recompense to/for strife Zion
9 Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami, mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho, nchi yake itakuwa lami iwakayo!
and to overturn torrent: river her to/for pitch and dust her to/for brimstone and to be land: country/planet her to/for pitch to burn: burn
10 Haitazimishwa usiku wala mchana, moshi wake utapaa juu milele. Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa, hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.
night and by day not to quench to/for forever: enduring to ascend: rise smoke her from generation to/for generation to destroy to/for perpetuity perpetuity nothing to pass in/on/with her
11 Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki, bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo. Mungu atanyoosha juu ya Edomu kamba ya kupimia ya machafuko matupu, na timazi ya ukiwa.
and to possess: possess her pelican and porcupine and owl and raven to dwell in/on/with her and to stretch upon her line formlessness and stone void
12 Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote kitakachoitwa ufalme huko, nao wakuu wao wote watatoweka.
noble her and nothing there kingship to call: call by and all ruler her to be end
13 Miiba itaenea katika ngome za ndani, viwawi na michongoma itaota kwenye ngome zake. Itakuwa maskani ya mbweha, makao ya bundi.
and to ascend: rise citadel: fortress her thorn nettle and thistle in/on/with fortification her and to be pasture jackal abode to/for daughter ostrich
14 Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi, nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana; huko viumbe vya usiku vitastarehe pia na kujitafutia mahali pa kupumzika.
and to meet wild beast [obj] wild beast and satyr upon neighbor his to call: call to surely there to rest night-creature and to find to/for her resting
15 Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai, atayaangua na kutunza makinda yake chini ya uvuli wa mabawa yake; pia huko vipanga watakusanyika, kila mmoja na mwenzi wake.
there [to] to make a nest arrow snake and to escape and to break up/open and to gather in/on/with shadow her surely there to gather hawk woman: another neighbor her
16 Angalieni katika gombo la Bwana na msome: Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana, hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake. Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza, na Roho wake atawakusanya pamoja.
to seek from upon scroll: book LORD and to call: read out one from them not to lack woman: another neighbor her not to reckon: missing for lip my he/she/it to command and spirit his he/she/it to gather them
17 Huwagawia sehemu zao, mkono wake huwagawanyia kwa kipimo. Wataimiliki hata milele na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
and he/she/it to fall: allot to/for them allotted and hand his to divide her to/for them in/on/with line till forever: enduring to possess: possess her to/for generation and generation to dwell in/on/with her

< Isaya 34 >