< Isaya 34 >

1 Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize; sikilizeni kwa makini, enyi kabila za watu! Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake, ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!
Draw near, O ye nations, and hear! Attend, O ye people! Let the earth hear, and all that is therein; The world, and all that springs from it!
2 Bwana ameyakasirikia mataifa yote; ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote. Atawaangamiza kabisa, atawatia mikononi mwa wachinjaji.
For the wrath of Jehovah is kindled against all the nations, And his fury against all their armies; He hath devoted them to destruction; He hath given them up to slaughter.
3 Waliouawa watatupwa nje, maiti zao zitatoa uvundo, milima itatota kwa damu zao.
Their slain shall be cast out; From their carcasses their stench shall ascend, And the mountains shall flow down with their blood.
4 Nyota zote za mbinguni zitayeyuka na anga litasokotwa kama kitabu, jeshi lote la angani litaanguka kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu, kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.
And all the hosts of heaven shall melt away; And the heavens shall be rolled up like a scroll, And all their host shall fall down, As the withered leaf faileth from the vine, As the blighted fruit from the fig-tree.
5 Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni, tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu, wale watu ambao nimeshawahukumu, kuwaangamiza kabisa.
For my sword hath become drunk in heaven; Behold, upon Edom shall it descend, Upon the people under my curse, for vengeance.
6 Upanga wa Bwana umeoga katika damu, umefunikwa na mafuta ya nyama: damu ya kondoo na mbuzi, mafuta kutoka figo za kondoo dume. Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra, na machinjo makuu huko Edomu.
The sword of Jehovah is full of blood; It is covered with fat, With the blood of lambs and goats, With the fat of the kidneys of rams; For Jehovah holdeth a sacrifice in Bozrah, And a great slaughter in the land of Edom.
7 Nyati wataanguka pamoja nao, ndama waume na mafahali wakubwa. Nchi yao italowana kwa damu, nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.
The wild buffaloes shall fall down with them. And the bullocks with the bulls; The hind shall be drunk with blood, And the ground enriched with fat.
8 Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi, mwaka wa malipo, siku ya kushindania shauri la Sayuni.
For Jehovah holdeth a day of vengeance, A year of recompense in the cause of Zion.
9 Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami, mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho, nchi yake itakuwa lami iwakayo!
Her streams shall be turned into pitch, And her dust into brimstone, And her whole land shall become burning pitch.
10 Haitazimishwa usiku wala mchana, moshi wake utapaa juu milele. Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa, hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.
Day and night it shall not be quenched; Its smoke shall ascend forever; From generation to generation it shall lie waste; None shall pass through it for ever and ever.
11 Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki, bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo. Mungu atanyoosha juu ya Edomu kamba ya kupimia ya machafuko matupu, na timazi ya ukiwa.
The pelican and the hedgehog shall possess it; The heron and the raven shall dwell in it; Over it will he draw the measuring-line of destruction. And the plummet of desolation.
12 Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote kitakachoitwa ufalme huko, nao wakuu wao wote watatoweka.
Her nobles — none are there, who may proclaim a kingdom, And all her princes have come to naught.
13 Miiba itaenea katika ngome za ndani, viwawi na michongoma itaota kwenye ngome zake. Itakuwa maskani ya mbweha, makao ya bundi.
Thorns shall spring up in her palaces; Nettles and thistles in her strongholds. She shall become a habitation for jackals, A court for ostriches.
14 Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi, nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana; huko viumbe vya usiku vitastarehe pia na kujitafutia mahali pa kupumzika.
The wild-cats shall fall upon the wolves, And the satyr shall call to his fellow; There also shall the night-spectre light, And find a place of rest.
15 Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai, atayaangua na kutunza makinda yake chini ya uvuli wa mabawa yake; pia huko vipanga watakusanyika, kila mmoja na mwenzi wake.
There also shall the arrow-snake make her nest, and lay her eggs; She shall hatch them, and gather her young under her shadow: There also shall the vultures be gathered together, Every one with her mate.
16 Angalieni katika gombo la Bwana na msome: Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana, hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake. Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza, na Roho wake atawakusanya pamoja.
Search ye the book of Jehovah, and read! Not one of these shall fail; Not one shall want her mate; For His mouth, it shall command, And His spirit, it shall gather them.
17 Huwagawia sehemu zao, mkono wake huwagawanyia kwa kipimo. Wataimiliki hata milele na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
He shall cast the lot for them; His hand shall divide it for them with a line; They shall possess it forever; From generation to generation shall they dwell therein.

< Isaya 34 >