< Isaya 34 >

1 Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize; sikilizeni kwa makini, enyi kabila za watu! Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake, ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!
Přistuptež národové, abyste slyšeli, a lidé pozorujte. Nechať slyší země i plnost její, okršlek zemský i všeliký plod jeho.
2 Bwana ameyakasirikia mataifa yote; ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote. Atawaangamiza kabisa, atawatia mikononi mwa wachinjaji.
Proto že hněv Hospodinův jest proti všechněm národům, a prchlivost proti všemu vojsku jejich: vyhubí je jako proklaté, a vydá je k zabití.
3 Waliouawa watatupwa nje, maiti zao zitatoa uvundo, milima itatota kwa damu zao.
I budou povrženi zbití jejich, a z těl mrtvých jejich vzejde smrad, a rozplynou se hory od krve jejich.
4 Nyota zote za mbinguni zitayeyuka na anga litasokotwa kama kitabu, jeshi lote la angani litaanguka kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu, kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.
Chřadnouti bude i všecko vojsko nebeské, a svinuta budou nebesa jako kniha, a všecko vojsko jejich sprchne, jako prší list s vinného kmene, a jako nezralé ovoce s fíku.
5 Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni, tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu, wale watu ambao nimeshawahukumu, kuwaangamiza kabisa.
Nebo opojen jest na nebi meč můj; na Idumejské sstoupí, a na lid, na nějž jsem klatbu vydal, aby trestán byl.
6 Upanga wa Bwana umeoga katika damu, umefunikwa na mafuta ya nyama: damu ya kondoo na mbuzi, mafuta kutoka figo za kondoo dume. Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra, na machinjo makuu huko Edomu.
Meč Hospodinův bude plný krve, umastí se tukem a krví beranů a kozlů, tukem ledvin skopových; obět zajisté bude míti Hospodin v Bozra, a zabijení veliké v zemi Idumejské.
7 Nyati wataanguka pamoja nao, ndama waume na mafahali wakubwa. Nchi yao italowana kwa damu, nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.
Sstoupí s nimi i jednorožcové a volčata s voly, i opije se země jejich krví, a prach jejich tukem se omastí.
8 Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi, mwaka wa malipo, siku ya kushindania shauri la Sayuni.
Nebo den pomsty Hospodinovy, léto odplacování se, aby mštěno bylo Siona.
9 Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami, mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho, nchi yake itakuwa lami iwakayo!
A obráceni budou potokové její v smolu, a prach její v siru, a země její obrátí se v smolu hořící.
10 Haitazimishwa usiku wala mchana, moshi wake utapaa juu milele. Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa, hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.
V noci ani ve dne neuhasne, na věky vystupovati bude dým její, od národu až do pronárodu pustá zůstane, na věky věků nebude, kdo by šel přes ni.
11 Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki, bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo. Mungu atanyoosha juu ya Edomu kamba ya kupimia ya machafuko matupu, na timazi ya ukiwa.
Ale osednou ji pelikán a výr, kalous také a krkavec budou bydliti v ní, a roztáhne po ní šňůru zahanbení a závaží marnosti.
12 Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote kitakachoitwa ufalme huko, nao wakuu wao wote watatoweka.
Šlechticů jejích volati budou k království, ale nebude tam žádného, nebo všecka knížata její zhynou.
13 Miiba itaenea katika ngome za ndani, viwawi na michongoma itaota kwenye ngome zake. Itakuwa maskani ya mbweha, makao ya bundi.
A vzroste na palácích jejích trní, kopřivy a bodláčí na hradích jejích, a bude příbytkem draků a obydlím sov.
14 Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi, nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana; huko viumbe vya usiku vitastarehe pia na kujitafutia mahali pa kupumzika.
Tam se budou potkávati spolu zvěř s ptactvem, a příšera jedna druhé se ozývati; tam toliko noční přeluda se usadí, a odpočinutí sobě nalezne.
15 Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai, atayaangua na kutunza makinda yake chini ya uvuli wa mabawa yake; pia huko vipanga watakusanyika, kila mmoja na mwenzi wake.
Tam se zhnízdí sup, a škřečeti bude, a když vysedí, shromáždí je pod stín svůj; tam také shledají se luňáci jeden s druhým.
16 Angalieni katika gombo la Bwana na msome: Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana, hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake. Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza, na Roho wake atawakusanya pamoja.
Hledejte v knize Hospodinově, a čtěte. Ani jedno z těch nechybí, a jeden každý bez své druže nebude; nebo to ústa Páně přikázala, a duch jeho shromáždí je.
17 Huwagawia sehemu zao, mkono wake huwagawanyia kwa kipimo. Wataimiliki hata milele na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
Onť zajisté vrže jim losy, a ruka jeho jim rozdělí ji provazcem; až na věky dědičně ji osednou, od národu až do pronárodu v ní přebývati budou.

< Isaya 34 >