< Isaya 32 >

1 Tazama, mfalme atatawala kwa uadilifu na watawala watatawala kwa haki.
Katso, kuningas on hallitseva vanhurskaudessa, ja valtiaat vallitsevat oikeuden mukaan.
2 Kila mtu atakuwa kama kivuli cha kujificha kutokana na upepo na kimbilio kutokana na dhoruba, kama vijito vya maji jangwani na kivuli cha mwamba mkubwa katika ardhi yenye kiu.
Silloin on jokainen heistä oleva turvana tuulelta ja suojana rankkasateelta, oleva kuin vesipurot kuivassa maassa, kuin korkean kallion varjo nääntyvässä maassa.
3 Ndipo macho ya wale wanaoona hayatafumbwa tena, nayo masikio ya wale wanaosikia yatasikiliza.
Silloin eivät näkevien silmät ole soaistut, ja kuulevien korvat kuulevat tarkkaan.
4 Moyo wa mtu mwenye hamaki utafahamu na kuelewa, nao ulimi wenye kigugumizi utanena kwa ufasaha.
Ajattelemattomien sydän käsittää taidon, ja änkyttäväin kieli puhuu sujuvasti ja selkeästi.
5 Mpumbavu hataitwa tena muungwana, wala mtu mbaya kabisa kupewa heshima ya juu.
Ei houkkaa enää kutsuta jaloksi, eikä petollista enää sanota yleväksi.
6 Kwa kuwa mpumbavu hunena upumbavu, moyo wake hushughulika na uovu: Hutenda mambo yasiyo ya kumcha Mungu, na hueneza habari za makosa kuhusu Bwana; yeye huwaacha wenye njaa bila kitu, na wenye kiu huwanyima maji.
Sillä houkka puhuu houkan lailla, ja hänen sydämensä hankkii turmiota, ja niin hän harjoittaa riettautta ja puhuu eksyttäväisesti Herrasta, jättää tyhjäksi nälkäisen sielun ja janoavaisen juomaa vaille.
7 Taratibu za mtu mbaya kabisa ni ovu, hufanya mipango miovu ili kumwangamiza maskini kwa uongo, hata wakati ambapo hoja za mhitaji ni za haki.
Ja pahat ovat petollisen aseet, hän miettii ilkitöitä, tuhotakseen kurjat valheen sanoilla, vaikka köyhä kuinka oikeata asiaa puhuisi.
8 Lakini mtu muungwana hufanya mipango ya kiungwana, na kwa matendo ya kiungwana yeye hufanikiwa.
Mutta jalo jaloja miettii ja jaloudessa lujana pysyy.
9 Enyi wanawake wenye kuridhika sana, amkeni na mnisikilize. Enyi binti mnaojisikia kuwa salama, sikieni lile ninalotaka kuwaambia!
Nouskaa, te suruttomat naiset, kuulkaa minun ääntäni; te huolettomat tyttäret, tarkatkaa minun sanojani.
10 Muda zaidi kidogo ya mwaka mmoja, ninyi mnaojisikia salama mtatetemeka, mavuno ya zabibu yatakoma na mavuno ya matunda hayatakuwepo.
Vielä vuosi, ja päiviä päälle, niin vapisette, te huolettomat; sillä silloin on viininkorjuusta tullut loppu, hedelmänkorjuuta ei tule.
11 Tetemekeni, enyi wanawake wenye kuridhika, tetemekeni kwa hofu, enyi binti mnaojisikia salama! Vueni nguo zenu, vaeni nguo ya gunia viunoni mwenu.
Kauhistukaa, te suruttomat, vaviskaa, te huolettomat, riisuutukaa, paljastukaa, vyöttäkää säkki lanteillenne.
12 Pigeni matiti yenu kwa ajili ya mashamba mazuri, kwa ajili ya mizabibu iliyozaa vizuri
Silloin valitetaan ja lyödään rintoihin ihanien peltojen tähden ja hedelmällisten viiniköynnösten tähden,
13 na kwa ajili ya nchi ya watu wangu, nchi ambayo miiba na michongoma imemea: naam, ombolezeni kwa ajili ya nyumba zote za furaha na kwa ajili ya mji huu wenye kufanya sherehe.
minun kansani maan tähden, joka kasvaa orjantappuraa ja ohdaketta, remuavan kaupungin kaikkien iloisten talojen tähden.
14 Ngome itaachwa, mji wenye kelele nyingi utahamwa, ngome ndani ya mji na mnara wa ulinzi vitakuwa ukiwa milele, mahali pazuri pa punda na malisho ya makundi ya kondoo,
Sillä palatsi on hyljätty, kaupungin kohina lakannut, Oofel ja vartiotorni ovat jääneet luoliksi iankaikkisesti, villiaasien iloksi ja laumojen laitumeksi.
15 mpaka Roho amwagwe juu yetu kutoka juu, nalo jangwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba kuwa kama msitu.
Näin on hamaan siihen asti, kunnes meidän päällemme vuodatetaan Henki korkeudesta. Silloin erämaa muuttuu puutarhaksi,
16 Haki itakaa katika jangwa, na uadilifu utakaa katika shamba lenye rutuba.
ja puutarha on metsän veroinen. Ja erämaassa asuu oikeus, ja puutarhassa majailee vanhurskaus.
17 Matunda ya haki yatakuwa amani, matokeo ya haki yatakuwa utulivu na matumaini milele.
Silloin vanhurskauden hedelmä on rauha, vanhurskauden vaikutus lepo ja turvallisuus iankaikkisesti.
18 Watu wangu wataishi katika makao ya mahali pa amani, katika nyumba zilizo salama, katika mahali pa kupumzika pasipo na usumbufu.
Ja minun kansani asuu rauhan majoissa, turvallisissa asunnoissa, huolettomissa lepopaikoissa.
19 Hata kama mvua ya mawe iangushe msitu na mji ubomolewe kabisa,
Mutta raesade tulee, metsä kaatuu, ja kaupunki alennetaan alhaiseksi.
20 tazama jinsi utakavyobarikiwa, ukipanda mbegu yako katika kila kijito, na kuwaacha ngʼombe wako na punda wajilishe kwa uhuru.
Onnelliset te, jotka kylvätte kaikkien vetten vierille ja laskette härän ja aasin jalat valtoimina kulkemaan!

< Isaya 32 >