< Isaya 32 >

1 Tazama, mfalme atatawala kwa uadilifu na watawala watatawala kwa haki.
Se, med Retfærdighed skal en Konge regere, og efter Ret skulle Fyrsterne styre.
2 Kila mtu atakuwa kama kivuli cha kujificha kutokana na upepo na kimbilio kutokana na dhoruba, kama vijito vya maji jangwani na kivuli cha mwamba mkubwa katika ardhi yenye kiu.
Og enhver af dem skal være som Skjul imod Vejr og Ly imod Vandskyl, som Vandbække paa et tørt Sted og som en svar Klippes Skygge i et vansmægtende Land.
3 Ndipo macho ya wale wanaoona hayatafumbwa tena, nayo masikio ya wale wanaosikia yatasikiliza.
Og de seendes Øjne skulle ikke være blændede, og de hørendes Øren skulle give Agt.
4 Moyo wa mtu mwenye hamaki utafahamu na kuelewa, nao ulimi wenye kigugumizi utanena kwa ufasaha.
Og de ubesindiges Hjerte skal forstaa Kundskab; og de stammendes Tunge skal haste til at tale forstaaelige Ord.
5 Mpumbavu hataitwa tena muungwana, wala mtu mbaya kabisa kupewa heshima ya juu.
En Daare skal ikke ydermere kaldes ædel og en karrig ej kaldes rig.
6 Kwa kuwa mpumbavu hunena upumbavu, moyo wake hushughulika na uovu: Hutenda mambo yasiyo ya kumcha Mungu, na hueneza habari za makosa kuhusu Bwana; yeye huwaacha wenye njaa bila kitu, na wenye kiu huwanyima maji.
Thi en Daare taler Daarlighed, og hans Hjerte gør Uret for at øve Ugudelighed og for at tale Usandhed imod Herren, for at lade en hungrig Sjæl forblive tom og lade en tørstig fattes Drik.
7 Taratibu za mtu mbaya kabisa ni ovu, hufanya mipango miovu ili kumwangamiza maskini kwa uongo, hata wakati ambapo hoja za mhitaji ni za haki.
Og den karrige bruger slette Midler; han optænker List for at berede de elendige Fordærvelse med falske Ord, og det, naar den fattige taler sin Sag.
8 Lakini mtu muungwana hufanya mipango ya kiungwana, na kwa matendo ya kiungwana yeye hufanikiwa.
Men den ædle tænker paa ædle Ting, han skal bestaa ved sin ædle Daad.
9 Enyi wanawake wenye kuridhika sana, amkeni na mnisikilize. Enyi binti mnaojisikia kuwa salama, sikieni lile ninalotaka kuwaambia!
I Kvinder, som ere saa sorgløse, staar op og hører min Røst! I Døtre, som ere saa trygge, vender Øren til min Tale!
10 Muda zaidi kidogo ya mwaka mmoja, ninyi mnaojisikia salama mtatetemeka, mavuno ya zabibu yatakoma na mavuno ya matunda hayatakuwepo.
Om Aar og Dag skulle I, som ere trygge, blive urolige; thi det er forbi med Vinhøsten, der kommer ingen Frugtsamling.
11 Tetemekeni, enyi wanawake wenye kuridhika, tetemekeni kwa hofu, enyi binti mnaojisikia salama! Vueni nguo zenu, vaeni nguo ya gunia viunoni mwenu.
Vorder forfærdede, I sorgløse! vorder urolige, I trygge! klæd dig af, og blot dig, og bind om Lænderne!
12 Pigeni matiti yenu kwa ajili ya mashamba mazuri, kwa ajili ya mizabibu iliyozaa vizuri
De skulle slaa sig for Brystet for de yndige Agres, for de frugtbare Vintræers Skyld;
13 na kwa ajili ya nchi ya watu wangu, nchi ambayo miiba na michongoma imemea: naam, ombolezeni kwa ajili ya nyumba zote za furaha na kwa ajili ya mji huu wenye kufanya sherehe.
der skal opvokse Torne og Tidsler paa mit Folks Mark, ja, over alle Glædens Boliger i den lystige Stad.
14 Ngome itaachwa, mji wenye kelele nyingi utahamwa, ngome ndani ya mji na mnara wa ulinzi vitakuwa ukiwa milele, mahali pazuri pa punda na malisho ya makundi ya kondoo,
Thi Paladserne ere forladte, Stadens Tummel er ophørt; Ofel og Vagttaarnet er blevet til Huler evindelig, Vildæsler til Glæde, Hjorde til Føde,
15 mpaka Roho amwagwe juu yetu kutoka juu, nalo jangwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba kuwa kama msitu.
indtil Aanden fra det høje udgydes over os, og Ørken bliver til en frugtbar Mark, og den frugtbare Mark agtes som en Skov;
16 Haki itakaa katika jangwa, na uadilifu utakaa katika shamba lenye rutuba.
og Ret bor i Ørken, og Retfærdighed bliver paa den frugtbare Mark;
17 Matunda ya haki yatakuwa amani, matokeo ya haki yatakuwa utulivu na matumaini milele.
og Retfærdigheds Gerning bliver Fred, og Retfærdighedens Løn bliver Hvile og Tryghed indtil evig Tid;
18 Watu wangu wataishi katika makao ya mahali pa amani, katika nyumba zilizo salama, katika mahali pa kupumzika pasipo na usumbufu.
og mit Folk bor i Fredens Hytter og i Trygheds Boliger og i stille rolige Steder.
19 Hata kama mvua ya mawe iangushe msitu na mji ubomolewe kabisa,
Men det skal hagle, naar Skoven fældes, og Staden skal nedtrykkes i det lave.
20 tazama jinsi utakavyobarikiwa, ukipanda mbegu yako katika kila kijito, na kuwaacha ngʼombe wako na punda wajilishe kwa uhuru.
Lyksalige ere I, som saa ved alle Vande, I, som lade Oksen og Æselet frit løbe om!

< Isaya 32 >