< Isaya 31 >

1 Ole wao wale washukao Misri kwa ajili ya msaada, wale wategemeao farasi, wanaoweka tumaini katika wingi wa magari yao ya vita, na katika nguvu nyingi za wapanda farasi, lakini hawamwangalii yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, wala hawatafuti msaada kwa Bwana.
Горе сходящым во Египет помощи ради, уповающым на кони и на колесницы: суть бо многа, и конническое множество много зело: и не беша уповающе на Святаго Израилева, и Бога не взыскаша.
2 Hata hivyo yeye pia ana hekima na anaweza kuleta maafa, wala hayatangui maneno yake. Yeye atainuka dhidi ya nyumba ya mwovu, dhidi ya wale ambao huwasaidia watenda mabaya.
Тойже премудре наведе на них злая, и слово Его не отринется, и востанет на домы человеков злых и на надежду их тщетную,
3 Lakini Wamisri ni wanadamu, wala si Mungu, farasi wao ni nyama, wala si roho. Wakati Bwana atakaponyoosha Mkono wake, yeye anayesaidia atajikwaa, naye anayesaidiwa ataanguka, wote wawili wataangamia pamoja.
Египтянина человека, а не Бога, конски плоти, и не будет помощи: Господь же наведет руку Свою на ня, и утрудятся помагающии, и вси вкупе погибнут.
4 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Kama vile simba angurumavyo, simba mkubwa juu ya mawindo yake: hata ingawa kundi lote la wachunga mifugo huitwa pamoja dhidi yake, hatiwi hofu na kelele zao wala kusumbuliwa na ghasia zao; ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote atakavyoshuka kufanya vita juu ya Mlima Sayuni na juu ya vilele vyake.
Занеже тако рече мне Господь: якоже возревет лев, или львичищь о ловитве, юже имет, и возопиет над нею, дондеже наполнятся горы гласа его, и победишася и множества ярости убояшася: тако Господь Саваоф снидет на гору Сионю и на горы его воевати.
5 Kama ndege warukao, Bwana Mwenye Nguvu Zote ataukinga Yerusalemu; ataukinga na kuuokoa, atapita juu yake na kuufanya salama.”
Якоже птицы парящыя, сице защитит Господь Саваоф о Иерусалиме, защитит и избавит, и снабдит и спасет.
6 Mrudieni yeye ambaye nyumba ya Israeli imemwasi sana.
Обратитеся, совещавающии глубок совет и беззаконен, сынове Израилевы:
7 Kwa kuwa katika siku ile kila mmoja wenu atazikataa sanamu za fedha na za dhahabu zilizotengenezwa kwa mikono yenu yenye dhambi.
яко в той день отвергут человецы рукотворенная своя сребряная и рукотворенная златая, яже сотвориша руки их.
8 “Ashuru itaanguka kwa upanga ambao si wa mwanadamu; upanga usio wa kibinadamu utawaangamiza. Watakimbia mbele ya upanga na vijana wao wa kiume watafanyizwa kazi kwa lazima.
И падет Ассур не мечем человеческим, ни мечь мужеский пояст его, и побегнет не от лица меча: юноты же будут в побеждение.
9 Ngome zao zitaanguka kwa sababu ya hofu; kwa kuona bendera ya vita, majemadari wao watashikwa na hofu ya ghafula,” asema Bwana, ambaye moto wake uko Sayuni, nayo tanuru yake iko Yerusalemu.
Камением бо оымутся яко острогом и побеждени будут, а бежай пленен будет. Сия глаголет Господь: (блажен, ) иже имеет племя в Сионе и южики во Иерусалиме.

< Isaya 31 >