< Isaya 31 >
1 Ole wao wale washukao Misri kwa ajili ya msaada, wale wategemeao farasi, wanaoweka tumaini katika wingi wa magari yao ya vita, na katika nguvu nyingi za wapanda farasi, lakini hawamwangalii yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, wala hawatafuti msaada kwa Bwana.
Malheur à ceux qui descendront en Egypte pour y chercher du secours, qui espèrent dans des chevaux, et qui ont confiance dans des quadriges, parce qu’ils sont nombreux, et dans des cavaliers, parce qu’ils sont très forts, et qui ne se sont pas confiés au saint d’Israël, et n’ont pas recherché le Seigneur.
2 Hata hivyo yeye pia ana hekima na anaweza kuleta maafa, wala hayatangui maneno yake. Yeye atainuka dhidi ya nyumba ya mwovu, dhidi ya wale ambao huwasaidia watenda mabaya.
Mais lui-même sage a amené le malheur, et n’a pas retiré ses paroles; et il s’élèvera contre la maison des méchants, et contre le secours de ceux qui opèrent l’iniquité.
3 Lakini Wamisri ni wanadamu, wala si Mungu, farasi wao ni nyama, wala si roho. Wakati Bwana atakaponyoosha Mkono wake, yeye anayesaidia atajikwaa, naye anayesaidiwa ataanguka, wote wawili wataangamia pamoja.
L’Egypte est un homme et non un Dieu; et leurs chevaux sont chair, et non esprit; et le Seigneur inclinera sa main, et l’auxiliaire sera renversé à terre, et il tombera, celui à qui est donné secours, et tous ensemble seront détruits.
4 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Kama vile simba angurumavyo, simba mkubwa juu ya mawindo yake: hata ingawa kundi lote la wachunga mifugo huitwa pamoja dhidi yake, hatiwi hofu na kelele zao wala kusumbuliwa na ghasia zao; ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote atakavyoshuka kufanya vita juu ya Mlima Sayuni na juu ya vilele vyake.
Parce que voici ce que dit le Seigneur: Comme si un lion et le petit d’un lion rugissent en se jetant sur leur proie, et que coure contre eux une multitude de pasteurs, ils ne s’effrayeront pas de leur voix, et ne s’épouvanteront pas de leur multitude; ainsi descendra le Seigneur des armées, afin de combattre sur la montagne de Sion et sur sa colline.
5 Kama ndege warukao, Bwana Mwenye Nguvu Zote ataukinga Yerusalemu; ataukinga na kuuokoa, atapita juu yake na kuufanya salama.”
Comme des oiseaux qui volent au secours de leurs petits, ainsi le Seigneur des armées protégera Jérusalem; la protégeant et la délivrant, passant et la sauvant.
6 Mrudieni yeye ambaye nyumba ya Israeli imemwasi sana.
Revenez, selon que vous vous étiez profondément éloignés, fils d’Israël.
7 Kwa kuwa katika siku ile kila mmoja wenu atazikataa sanamu za fedha na za dhahabu zilizotengenezwa kwa mikono yenu yenye dhambi.
Car en ce jour-là, chacun rejettera ses idoles d’argent et ses idoles d’or, que vos mains vous ont faites pour le péché.
8 “Ashuru itaanguka kwa upanga ambao si wa mwanadamu; upanga usio wa kibinadamu utawaangamiza. Watakimbia mbele ya upanga na vijana wao wa kiume watafanyizwa kazi kwa lazima.
Et Assur tombera, par le glaive non d’un homme, et le glaive non d’un homme le dévorera, et il fuira, non à la face du glaive, et ses jeunes hommes seront tributaires;
9 Ngome zao zitaanguka kwa sababu ya hofu; kwa kuona bendera ya vita, majemadari wao watashikwa na hofu ya ghafula,” asema Bwana, ambaye moto wake uko Sayuni, nayo tanuru yake iko Yerusalemu.
Et sa force disparaîtra par la terreur, et ses princes fuyant seront épouvantés, a dit le Seigneur, dont le feu est dans Sion, et le foyer dans Jérusalem.