< Isaya 31 >

1 Ole wao wale washukao Misri kwa ajili ya msaada, wale wategemeao farasi, wanaoweka tumaini katika wingi wa magari yao ya vita, na katika nguvu nyingi za wapanda farasi, lakini hawamwangalii yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, wala hawatafuti msaada kwa Bwana.
Wo to hem that goon doun in to Egipt to help, and hopen in horsis, and han trist on cartis, for tho ben manye, and on knyytis, for thei ben ful stronge; and thei tristiden not on the hooli of Israel, and thei souyten not the Lord.
2 Hata hivyo yeye pia ana hekima na anaweza kuleta maafa, wala hayatangui maneno yake. Yeye atainuka dhidi ya nyumba ya mwovu, dhidi ya wale ambao huwasaidia watenda mabaya.
Forsothe he that is wijs, hath brouyt yuel, and took not awei hise wordis; and he schal rise togidere ayens the hous of worste men, and ayens the helpe of hem that worchen wickidnesse.
3 Lakini Wamisri ni wanadamu, wala si Mungu, farasi wao ni nyama, wala si roho. Wakati Bwana atakaponyoosha Mkono wake, yeye anayesaidia atajikwaa, naye anayesaidiwa ataanguka, wote wawili wataangamia pamoja.
Egipt is a man, and not God; and the horsis of hem ben fleisch, and not spirit; and the Lord schal bowe doun his hond, and the helpere schal falle doun, and he schal falle, to whom help is youun, and alle schulen be wastid togidere.
4 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Kama vile simba angurumavyo, simba mkubwa juu ya mawindo yake: hata ingawa kundi lote la wachunga mifugo huitwa pamoja dhidi yake, hatiwi hofu na kelele zao wala kusumbuliwa na ghasia zao; ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote atakavyoshuka kufanya vita juu ya Mlima Sayuni na juu ya vilele vyake.
For whi the Lord seith these thingis to me, If a lioun rorith, and a whelp of a lioun on his prey, whanne the multitude of schipherdis cometh ayens hym, he schal not drede of the vois of hem, and he schal not drede of the multitude of hem; so the Lord of oostis schal come doun, for to fiyte on the mounteyn of Sion, and on the litil hil therof.
5 Kama ndege warukao, Bwana Mwenye Nguvu Zote ataukinga Yerusalemu; ataukinga na kuuokoa, atapita juu yake na kuufanya salama.”
As briddis fleynge, so the Lord of oostis schal defende Jerusalem; he defendynge and delyuerynge, passynge forth and sauynge.
6 Mrudieni yeye ambaye nyumba ya Israeli imemwasi sana.
Ye sones of Israel, be conuertid, as ye hadden go awei in to depthe.
7 Kwa kuwa katika siku ile kila mmoja wenu atazikataa sanamu za fedha na za dhahabu zilizotengenezwa kwa mikono yenu yenye dhambi.
Forsothe in that dai a man schal caste awei the idols of his siluer, and the idols of his gold, whiche youre hondis maden to you in to synne.
8 “Ashuru itaanguka kwa upanga ambao si wa mwanadamu; upanga usio wa kibinadamu utawaangamiza. Watakimbia mbele ya upanga na vijana wao wa kiume watafanyizwa kazi kwa lazima.
And Assur schal falle bi swerd, not of man, and a swerd, not of man, schal deuoure hym; and he schal fle, not fro the face of swerd, and hise yonge men schulen be tributaries;
9 Ngome zao zitaanguka kwa sababu ya hofu; kwa kuona bendera ya vita, majemadari wao watashikwa na hofu ya ghafula,” asema Bwana, ambaye moto wake uko Sayuni, nayo tanuru yake iko Yerusalemu.
and the strengthe of hym schal passe fro ferdfulnesse, and hise princes fleynge schulen drede. The Lord seide, whos fier is in Sion, and his chymeney is in Jerusalem.

< Isaya 31 >