< Isaya 31 >

1 Ole wao wale washukao Misri kwa ajili ya msaada, wale wategemeao farasi, wanaoweka tumaini katika wingi wa magari yao ya vita, na katika nguvu nyingi za wapanda farasi, lakini hawamwangalii yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, wala hawatafuti msaada kwa Bwana.
Woe to those who go down to Egypt for help and lean on horses, and trust in chariots (for they are many) and in horsemen (for they are countless). But they are not concerned about the Holy One of Israel, nor do they seek Yahweh!
2 Hata hivyo yeye pia ana hekima na anaweza kuleta maafa, wala hayatangui maneno yake. Yeye atainuka dhidi ya nyumba ya mwovu, dhidi ya wale ambao huwasaidia watenda mabaya.
Yet he is wise, and he will bring disaster and will not retract his words. He will arise against the evil house and against the helpers of those who commit sin.
3 Lakini Wamisri ni wanadamu, wala si Mungu, farasi wao ni nyama, wala si roho. Wakati Bwana atakaponyoosha Mkono wake, yeye anayesaidia atajikwaa, naye anayesaidiwa ataanguka, wote wawili wataangamia pamoja.
Egypt is a man and not God, their horses flesh and not spirit. When Yahweh reaches out with his hand, both the one who helps will stumble, and the one who is helped will fall; both will perish together.
4 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Kama vile simba angurumavyo, simba mkubwa juu ya mawindo yake: hata ingawa kundi lote la wachunga mifugo huitwa pamoja dhidi yake, hatiwi hofu na kelele zao wala kusumbuliwa na ghasia zao; ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote atakavyoshuka kufanya vita juu ya Mlima Sayuni na juu ya vilele vyake.
This is what Yahweh says to me, “As a lion, even a young lion, growls over its torn prey, when a group of shepherds is called out against it, but it does not tremble at their voices, nor creep away from their sound; thus Yahweh of hosts will descend to fight on Mount Zion, on that hill.
5 Kama ndege warukao, Bwana Mwenye Nguvu Zote ataukinga Yerusalemu; ataukinga na kuuokoa, atapita juu yake na kuufanya salama.”
Like birds in flight, so Yahweh of hosts will protect Jerusalem; he will protect and rescue as he passes over it and preserves it.
6 Mrudieni yeye ambaye nyumba ya Israeli imemwasi sana.
Return to him from whom you have deeply turned away, people of Israel.
7 Kwa kuwa katika siku ile kila mmoja wenu atazikataa sanamu za fedha na za dhahabu zilizotengenezwa kwa mikono yenu yenye dhambi.
For in that day each one will get rid of his idols of silver and his idols of gold that your own hands have sinfully made.
8 “Ashuru itaanguka kwa upanga ambao si wa mwanadamu; upanga usio wa kibinadamu utawaangamiza. Watakimbia mbele ya upanga na vijana wao wa kiume watafanyizwa kazi kwa lazima.
Assyria will fall by the sword; a sword not wielded by man will consume him. He will flee from the sword, and his young men will be forced to do hard labor.
9 Ngome zao zitaanguka kwa sababu ya hofu; kwa kuona bendera ya vita, majemadari wao watashikwa na hofu ya ghafula,” asema Bwana, ambaye moto wake uko Sayuni, nayo tanuru yake iko Yerusalemu.
They will lose all confidence because of terror, and his princes will be afraid at the sight of Yahweh's battle flag— this is Yahweh's declaration—whose fire is in Zion and whose firepot is in Jerusalem.”

< Isaya 31 >