< Isaya 31 >

1 Ole wao wale washukao Misri kwa ajili ya msaada, wale wategemeao farasi, wanaoweka tumaini katika wingi wa magari yao ya vita, na katika nguvu nyingi za wapanda farasi, lakini hawamwangalii yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, wala hawatafuti msaada kwa Bwana.
Alas! for them who are going down to Egypt for help, On horses, would rely, —And have trusted—In chariots—because they are many, and In horsemen, because they are very bold, But have not looked unto the Holy One of Israel, And onto Yahweh, have not sought.
2 Hata hivyo yeye pia ana hekima na anaweza kuleta maafa, wala hayatangui maneno yake. Yeye atainuka dhidi ya nyumba ya mwovu, dhidi ya wale ambao huwasaidia watenda mabaya.
But, he also, is wise, and hath brought in calamity, And his own words, hath he not set aside, —Therefore will he rise up, Against the house of evil-doers, and Against the help of the workers of iniquity.
3 Lakini Wamisri ni wanadamu, wala si Mungu, farasi wao ni nyama, wala si roho. Wakati Bwana atakaponyoosha Mkono wake, yeye anayesaidia atajikwaa, naye anayesaidiwa ataanguka, wote wawili wataangamia pamoja.
Now, the Egyptians, are, men, and not, GOD, And, their horses, flesh, and not, spirit; When, Yahweh, shall stretch out his hand, Then, he that is giving help, shall stumble And, he that is receiving help, shall fall, And, together, shall, all of them, vanish!
4 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Kama vile simba angurumavyo, simba mkubwa juu ya mawindo yake: hata ingawa kundi lote la wachunga mifugo huitwa pamoja dhidi yake, hatiwi hofu na kelele zao wala kusumbuliwa na ghasia zao; ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote atakavyoshuka kufanya vita juu ya Mlima Sayuni na juu ya vilele vyake.
For Thus, hath Yahweh said unto me—Like as a lion or a young lion growleth over his prey. Who—though there be called out against him a multitude of shepherds—Will not at their voice, be dismayed, Nor, at their noise, be daunted, So, will Yahweh of hosts come down, to make war over Mount Zion, and over the hill thereof.
5 Kama ndege warukao, Bwana Mwenye Nguvu Zote ataukinga Yerusalemu; ataukinga na kuuokoa, atapita juu yake na kuufanya salama.”
As little mother-birds hovering, so, will Yahweh of hosts throw a covering over Jerusalem, —Covering, so will he rescue, Passing over, so will he deliver!
6 Mrudieni yeye ambaye nyumba ya Israeli imemwasi sana.
Return ye unto him against whom the sons of Israel have deeply revolted,
7 Kwa kuwa katika siku ile kila mmoja wenu atazikataa sanamu za fedha na za dhahabu zilizotengenezwa kwa mikono yenu yenye dhambi.
For in that day, will every man reject his idols of silver, and his idols of gold, —Which your hands had made for you as a sin!
8 “Ashuru itaanguka kwa upanga ambao si wa mwanadamu; upanga usio wa kibinadamu utawaangamiza. Watakimbia mbele ya upanga na vijana wao wa kiume watafanyizwa kazi kwa lazima.
Then shall the Assyrian fall, by the sword, not of a great man, And the sword, not of a mean man, shall devour him, —Howbeit he shall take his flight from the face of a sword, And his young men, shall come under tribute;
9 Ngome zao zitaanguka kwa sababu ya hofu; kwa kuona bendera ya vita, majemadari wao watashikwa na hofu ya ghafula,” asema Bwana, ambaye moto wake uko Sayuni, nayo tanuru yake iko Yerusalemu.
And his own Cliff, through terror, shall he pass by, And his princes shall be dismayed at an ensign, —Declareth Yahweh. Who hath a flame in Zion, And hath a furnace in Jerusalem.

< Isaya 31 >