< Isaya 31 >
1 Ole wao wale washukao Misri kwa ajili ya msaada, wale wategemeao farasi, wanaoweka tumaini katika wingi wa magari yao ya vita, na katika nguvu nyingi za wapanda farasi, lakini hawamwangalii yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, wala hawatafuti msaada kwa Bwana.
Woe to them that go down to Egypt for help, And put their trust in horses, And confide in chariots, because they are many, And in horsemen, because their number is great, But look not to the Holy One of Israel, And resort not to Jehovah.
2 Hata hivyo yeye pia ana hekima na anaweza kuleta maafa, wala hayatangui maneno yake. Yeye atainuka dhidi ya nyumba ya mwovu, dhidi ya wale ambao huwasaidia watenda mabaya.
Yet he, too, is wise; He will bring evil, and not take back his words; He will arise against the house of the evil-doers, And against the help of them that do iniquity.
3 Lakini Wamisri ni wanadamu, wala si Mungu, farasi wao ni nyama, wala si roho. Wakati Bwana atakaponyoosha Mkono wake, yeye anayesaidia atajikwaa, naye anayesaidiwa ataanguka, wote wawili wataangamia pamoja.
The Egyptians are men, and not God, And their horses are flesh, and not spirit. When Jehovah shall stretch forth his hand, Then shall the helper fall, and the helped be overthrown; And they shall all perish together.
4 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Kama vile simba angurumavyo, simba mkubwa juu ya mawindo yake: hata ingawa kundi lote la wachunga mifugo huitwa pamoja dhidi yake, hatiwi hofu na kelele zao wala kusumbuliwa na ghasia zao; ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote atakavyoshuka kufanya vita juu ya Mlima Sayuni na juu ya vilele vyake.
For thus hath Jehovah said to me: As when the lion and the young lion growl over their prey, And a multitude of shepherds is called forth against him, By their noise he is not terrified, Nor by their tumult disheartened; So shall Jehovah of hosts come down to fight for mount Zion, and her hill.
5 Kama ndege warukao, Bwana Mwenye Nguvu Zote ataukinga Yerusalemu; ataukinga na kuuokoa, atapita juu yake na kuufanya salama.”
As birds hover over their young, So shall Jehovah of hosts defend Jerusalem; He will defend and deliver, spare and save.
6 Mrudieni yeye ambaye nyumba ya Israeli imemwasi sana.
Turn, O ye children of Israel, To him from whom ye have so deeply revolted! For in that day shall every one cast away his idols of
7 Kwa kuwa katika siku ile kila mmoja wenu atazikataa sanamu za fedha na za dhahabu zilizotengenezwa kwa mikono yenu yenye dhambi.
silver and his idols of gold, Which your hands have made for sin.
8 “Ashuru itaanguka kwa upanga ambao si wa mwanadamu; upanga usio wa kibinadamu utawaangamiza. Watakimbia mbele ya upanga na vijana wao wa kiume watafanyizwa kazi kwa lazima.
The Assyrian shall fall by a sword not of man, Yea, a sword not of mortal shall devour him; He shall flee before the sword, And his young warriors shall be slaves.
9 Ngome zao zitaanguka kwa sababu ya hofu; kwa kuona bendera ya vita, majemadari wao watashikwa na hofu ya ghafula,” asema Bwana, ambaye moto wake uko Sayuni, nayo tanuru yake iko Yerusalemu.
Through fear shall he pass beyond his stronghold, And his princes shall be afraid of the standard. Thus saith Jehovah, who hath his fire in Zion, And his furnace in Jerusalem.