< Isaya 30 >

1 Bwana asema, “Ole kwa watoto wakaidi, kwa wale wanaotimiza mipango ambayo si yangu, wakifanya makubaliano, lakini si kwa Roho wangu, wakilundika dhambi juu ya dhambi,
Malheur à vous, fils déserteurs, dit le Seigneur, de ce que vous formez des desseins, et non par moi, et que vous ourdissez une trame, et non par mon esprit, afin d’ajouter péché à péché;
2 wale washukao kwenda Misri bila kutaka shauri langu, wanaotafuta msaada wa ulinzi wa Farao, watafutao kivuli cha Misri kwa ajili ya kimbilio.
Vous qui marchez pour descendre en Egypte, et n’avez pas interrogé ma bouche, espérant du secours de la force de Pharaon, et ayant confiance dans l’ombre de l’Egypte.
3 Lakini ulinzi wa Farao utakuwa kwa aibu yenu, kivuli cha Misri kitawaletea fedheha.
Et la force de Pharaon vous sera à confusion, et la confiance dans l’ombre de l’Egypte, à ignominie.
4 Ingawa wana maafisa katika Soani na wajumbe wamewasili katika Hanesi,
Car tes princes étaient à Tanis, et tes messagers sont parvenus jusqu’à Hanès.
5 kila mmoja ataaibishwa kwa sababu ya taifa lisilowafaa kitu, ambalo haliwaletei msaada wala faida, bali aibu tu na fedheha.”
Tous ont été confondus à la vue d’un peuple qui ne pouvait leur être utile; ils ne leur ont pas été à secours et à quelque utilité, mais à confusion et à opprobre.
6 Neno kuhusu wanyama wa Negebu: Katika nchi ya taabu na shida, ya simba za dume na jike, ya nyoka mwenye sumu kali na nyoka warukao, wajumbe huchukua utajiri wao juu ya migongo ya punda, hazina zao juu ya nundu za ngamia, kwa lile taifa lisilokuwa na faida,
Malheur accablant des bêtes du Midi. Elles vont dans une terre de tribulation et d’angoisse, d’où sortent la lionne et le lion, la vipère et le basilic volant; ils portent sur les épaules des ânes leurs richesses, et sur la bosse des chameaux leurs trésors, à un peuple qui ne pourra pas leur être utile.
7 kuvipeleka Misri, ambaye msaada wake haufai kabisa. Kwa hiyo nimemwita “Rahabu Asiyefanya Chochote.”
Car inutilement et vainement l’Egypte les secourra; voilà pourquoi j’ai crié à ce sujet: C’est de l’orgueil seulement, reste en repos.
8 Nenda sasa, liandike neno hili juu ya kibao kwa ajili yao, liandike kwenye kitabu, ili liweze kuwa shahidi milele kwa ajili ya siku zijazo.
Maintenant donc entre, écris cela pour lui sur le buis, et dans un livre grave-le soigneusement, et il sera au dernier jour un témoignage à jamais;
9 Hawa ni watu waasi, watoto wadanganyifu, watoto ambao hawataki kusikiliza mafundisho ya Bwana.
Car c’est un peuple provoquant au courroux, et ce sont des fils menteurs, des fils qui ne veulent pas entendre la loi de Dieu;
10 Wanawaambia waonaji, “Msione maono tena!” Nako kwa manabii wanasema, “Msiendelee kutupatia maono ambayo ni ya kweli! Tuambieni mambo ya kupendeza, tabirini mambo ya uongo.
Qui disent à ceux qui voient: Ne voyez pas; et à ceux qui regardent: Ne regardez pas pour nous des choses qui sont justes; dites-nous des choses qui nous plaisent, voyez pour nous des erreurs.
11 Acheni njia hii, ondokeni katika mapito haya, nanyi acheni kutukabili pamoja na yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli!”
Eloignez de moi cette voie, détournez de moi ce sentier; qu’il disparaisse de notre face, le saint d’Israël.
12 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa sababu mmekataa ujumbe huu, mkategemea uonevu na kutumainia udanganyifu,
À cause de cela, voici ce que dit le saint d’Israël: Parce que vous avez rejeté cette parole, et que vous avez espéré dans la calomnie et dans le tumulte, et que vous y avez mis votre appui,
13 dhambi hii itakuwa kwenu kama ukuta mrefu, wenye ufa na wenye kubetuka, ambao unaanguka ghafula, mara moja.
À cause de cela, cette iniquité sera pour vous comme une brèche qui menace ruine, et qui est recherchée dans un mur élevé, parce que tout à coup, tandis qu’on ne s’y attend pas, vient son écroulement.
14 Utavunjika vipande vipande kama chombo cha udongo ukipasuka pasipo huruma ambapo katika vipande vyake hakuna kipande kitakachopatikana kwa kuukulia makaa kutoka jikoni au kuchotea maji kisimani.”
Et elle sera mise en pièces, comme on brise d’un brisement très fort un vase de potier; et on ne trouvera pas parmi ses fragments un têt dans lequel on puisse porter un peu de feu pris d’une incendie, ou puiser un peu d’eau à une fosse,
15 Hili ndilo Bwana Mwenyezi, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, asemalo: “Katika kutubu na kupumzika ndio wokovu wenu, katika kutulia na kutumaini ndizo nguvu zenu, lakini hamkutaka.
Parce que voici ce que dit le Seigneur Dieu, le saint d’Israël: Si vous revenez, et vous vous tenez en repos, vous serez sauvés; dans le silence et dans l’espérance sera votre force. Et vous n’avez pas voulu;
16 Mlisema, ‘Hapana, tutakimbia kwa farasi.’ Kwa hiyo mtakimbia! Mlisema, ‘Tutakimbia kwa farasi waendao kasi.’ Kwa hiyo wanaowafukuza watakwenda kasi!
Et vous avez dit: Pas du tout; mais nous fuirons vers des chevaux; c’est pour cela que vous fuirez. Et nous monterons sur de rapides coursiers; c’est pour cela que plus rapides seront ceux qui vous poursuivront.
17 Watu 1,000 watakimbia kwa ajili ya kitisho cha mtu mmoja, kwa vitishio vya watu watano wote mtakimbia, hadi mtakapoachwa kama mlingoti wa bendera juu ya kilele cha mlima, kama bendera juu ya kilima.”
Vous fuirez an nombre de mille hommes par la terreur d’un seul, et tous par la terreur de cinq, jusqu’à ce que vous soyez laissés comme un mât de vaisseau sur une cime de montagne, et comme un étendard sur une colline.
18 Hata hivyo Bwana anatamani kutupatia neema, anainuka ili kuwaonyesha huruma. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa haki. Wamebarikiwa wote wanaomngojea yeye!
À cause de cela, le Seigneur attend, afin d’avoir pitié de vous; et pour cela il sera exalté en vous épargnant; car c’est un Dieu de justice que le Seigneur; bienheureux tous ceux qui l’attendent.
19 Enyi watu wa Sayuni, mnaoishi Yerusalemu, hamtalia tena. Tazameni jinsi atakavyokuwa na huruma mtakapolia kwa kumwomba msaada! Mara asikiapo, atawajibu.
Car le peuple de Sion habitera dans Jérusalem; pleurant tu ne pleureras pas du tout; ayant pitié il aura pitié de toi; à la voix de ton cri, dès qu’il entendra, il te répondra.
20 Ingawa Bwana huwapa chakula cha shida na maji ya taabu, walimu wenu hawatafichwa tena, kwa macho yenu wenyewe mtawaona.
Et le Seigneur vous donnera un pain restreint et une eau peu abondante; et il ne fera pas que celui qui t’instruit s’en aille loin de toi; et tes yeux verront ton maître.
21 Mkigeuka kuume au kushoto, masikio yenu yatasikia sauti nyuma yenu ikisema, “Hii ndiyo njia, ifuateni.”
Et tes oreilles entendront la voix de celui qui, derrière toi, t’avertira: Voici la voie, marchez-y; et ne vous détournez ni à droite ni à gauche,
22 Kisha mtanajisi sanamu zenu zilizofunikwa kwa fedha, na vinyago vyenu vilivyofunikwa kwa dhahabu. Mtazitupilia mbali kama vitambaa vya wakati wa hedhi na kuziambia, “Haya, tokeni hapa!”
Et tu regarderas comme choses souillées les lames d’argent de tes images taillées au ciseau, et le vêtement de ta statue d’or jetée en fonte, et tu les rejetteras comme un linge souillé. Sors, lui diras-tu;
23 Pia atawapa mvua kwa ajili ya mbegu mnazootesha ardhini, chakula kinachotoka ardhini kitakuwa kizuri sana, tena tele. Katika siku ile, ngʼombe wenu watalisha katika shamba pana la majani.
Et la pluie sera accordée à ta semence, partout où tu auras semé sur la terre, et le pain produit des grains de la terre sera très abondant et gras; dans ta possession, en ce jour-là, l’agneau paîtra spacieusement.
24 Maksai na punda walimao watakula majani makavu na vyakula vilivyotengenezwa, vinavyotandazwa kwa uma na sepeto.
Et les taureaux et les petits des ânes qui labourent la terre, mangeront les grains mêlés ensemble, comme dans l’aire ils auront été vannés.
25 Katika siku ile ya mauaji makuu, wakati minara itakapoanguka, vijito vya maji vitatiririka juu ya kila mlima mrefu na kila kilima kilichoinuka sana.
Et il y aura sur toute haute montagne et sur toute colline élevée, des ruisseaux d’eaux courantes, au jour où beaucoup auront été tués, et lorsque seront tombées les tours.
26 Mwezi utaangaza kama jua, nao mwanga wa jua utangʼaa mara saba zaidi, kama nuru ya siku saba, wakati Bwana atakapoyafunga majeraha ya watu wake na kuwaponya vidonda alivyowatia.
Et sera la lumière de la lune comme la lumière du soleil, et la lumière du soleil sera septuplée, égale à la lumière de sept jours, au jour où le Seigneur aura lié la blessure de son peuple et guéri le coup de sa plaie.
27 Tazama, Jina la Bwana linakuja kutoka mbali, likiwa na hasira kali inayowaka pamoja na wingu zito la moshi, midomo yake imejaa ghadhabu na ulimi wake ni moto ulao.
Voici que le nom du Seigneur vient de loin; ardente est sa fureur, et lourde à porter; ses lèvres sont pleines d’indignation, sa langue est comme un feu dévorant.
28 Pumzi yake ni kama mkondo wa maji yaendayo kasi, yakipanda hadi shingoni. Hutikisa mataifa katika chekecheke ya uharibifu, huweka lijamu katika mataya ya mataifa ambayo huwaongoza upotevuni.
Son souffle est un torrent débordé, qui atteint jusqu’au milieu du cou, pour réduire des nations au néant, et briser le frein d’erreur qui était aux mâchoires des peuples.
29 Nanyi mtaimba kama usiku ule mnaadhimisha sikukuu takatifu. Mioyo yenu itashangilia kama vile watu wanapokwea na filimbi kwenye mlima wa Bwana, kwa Mwamba wa Israeli.
Vous chanterez comme dans la nuit d’une sainte solennité, et la joie de votre cœur sera comme la joie de celui qui va avec la flûte, afin de se présenter sur la montagne du Seigneur, au fort d’Israël.
30 Bwana atawasababisha watu waisikie sauti yake ya utukufu, naye atawafanya wauone mkono wake ukishuka pamoja na hasira yake kali na moto ulao, kukiwa na tufani ya mvua, ngurumo za radi na mvua ya mawe.
Et le Seigneur fera entendre la majesté de sa voix, et il montrera la terreur de son bras dans une menace de fureur, et dans la flamme d’un feu dévorant; il brisera par un tourbillon et par des pierres de grêle.
31 Sauti ya Bwana itaivunjavunja Ashuru, kwa fimbo yake ya utawala atawapiga.
Car à la voix du Seigneur Assur tremblera d’effroi, frappé de sa verge.
32 Kila pigo Bwana atakaloliweka juu yao kwa fimbo yake ya kuadhibu, litakuwa kwa wimbo wa matari na vinubi, anapopigana nao katika vita kwa mapigo ya mkono wake.
Et le passage de la verge sera affermi; le Seigneur la fera reposer sur lui au milieu des tambours et des harpes, et dans des guerres considérables il les vaincra.
33 Tofethi imeandaliwa toka zamani, imewekwa tayari kwa ajili ya mfalme. Shimo lake la moto limetengenezwa kwa kina kirefu na kwa upana mkubwa, likiwa na moto na kuni tele; pumzi ya Bwana, kama kijito cha kiberiti, huuwasha moto.
Car Topheth est préparée depuis hier, par le roi préparée, profonde et étendue. Ses aliments sont du feu et beaucoup de bois; le souffle du Seigneur comme un torrent de soufre l’embrase.

< Isaya 30 >