< Isaya 30 >

1 Bwana asema, “Ole kwa watoto wakaidi, kwa wale wanaotimiza mipango ambayo si yangu, wakifanya makubaliano, lakini si kwa Roho wangu, wakilundika dhambi juu ya dhambi,
Malheur à vous, enfants rebelles! dit le Seigneur; vous avez tenu conseil, et ce n'est pas avec moi; vous avez pris des résolutions, et ce n'est pas avec mon Esprit; vous entassez péchés sur péchés,
2 wale washukao kwenda Misri bila kutaka shauri langu, wanaotafuta msaada wa ulinzi wa Farao, watafutao kivuli cha Misri kwa ajili ya kimbilio.
O vous qui êtes partis pour descendre en Égypte, sans me consulter, pour demander du secours au Pharaon, et trouver un abri chez les Égyptiens.
3 Lakini ulinzi wa Farao utakuwa kwa aibu yenu, kivuli cha Misri kitawaletea fedheha.
Car l'appui du Pharaon sera pour vous une honte; et l'opprobre attend ceux qui se reposent sur l'Égypte.
4 Ingawa wana maafisa katika Soani na wajumbe wamewasili katika Hanesi,
Car vos princes sont allés à Tanis, messagers de malheur.
5 kila mmoja ataaibishwa kwa sababu ya taifa lisilowafaa kitu, ambalo haliwaletei msaada wala faida, bali aibu tu na fedheha.”
Ils ont pris une peine inutile auprès d'un peuple qui ne les aidera point pour le secours, mais pour la confusion et l'opprobre.
6 Neno kuhusu wanyama wa Negebu: Katika nchi ya taabu na shida, ya simba za dume na jike, ya nyoka mwenye sumu kali na nyoka warukao, wajumbe huchukua utajiri wao juu ya migongo ya punda, hazina zao juu ya nundu za ngamia, kwa lile taifa lisilokuwa na faida,
Ils vont dans l'affliction et la détresse, là où il y a un lion et un lionceau, et d'où viennent aussi des aspics et des petits d'aspics volants; ils ont transporté sur des ânes et des chamelles leurs richesses près d'une nation qui ne les aidera point.
7 kuvipeleka Misri, ambaye msaada wake haufai kabisa. Kwa hiyo nimemwita “Rahabu Asiyefanya Chochote.”
Les Égyptiens vous donneront un secours vain et inutile; dis-leur: Cette consolation pour vous est vaine.
8 Nenda sasa, liandike neno hili juu ya kibao kwa ajili yao, liandike kwenye kitabu, ili liweze kuwa shahidi milele kwa ajili ya siku zijazo.
Maintenant donc, assieds-toi; écris ces choses sur le buis et dans un livre; car ce sera pour les jours de l'avenir et même pour tous les siècles.
9 Hawa ni watu waasi, watoto wadanganyifu, watoto ambao hawataki kusikiliza mafundisho ya Bwana.
Parce que ce peuple est indocile; fils menteurs, qui ne veulent point écouter la loi de Dieu,
10 Wanawaambia waonaji, “Msione maono tena!” Nako kwa manabii wanasema, “Msiendelee kutupatia maono ambayo ni ya kweli! Tuambieni mambo ya kupendeza, tabirini mambo ya uongo.
Ils disent aux prophètes: Ne nous annoncez rien; ils disent à ceux qui ont des visions: Ne nous parlez pas; mais annoncez-nous quelque autre erreur.
11 Acheni njia hii, ondokeni katika mapito haya, nanyi acheni kutukabili pamoja na yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli!”
Détournez-nous de cette voie; ôtez-nous le sentier, ôtez-nous l'oracle d'Israël.
12 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa sababu mmekataa ujumbe huu, mkategemea uonevu na kutumainia udanganyifu,
A cause de cela, voici ce que dit le Saint d'Israël: Parce que vous n'avez point obéi à ces paroles, parce que vous avez espéré dans le mensonge, parce que vous avez murmuré et que vous avez mis votre confiance en vos murmures;
13 dhambi hii itakuwa kwenu kama ukuta mrefu, wenye ufa na wenye kubetuka, ambao unaanguka ghafula, mara moja.
A cause de cela, ce péché sera pour vous comme un mur qui s'écroule soudain, lorsque est prise une ville dont la chute est inopinée.
14 Utavunjika vipande vipande kama chombo cha udongo ukipasuka pasipo huruma ambapo katika vipande vyake hakuna kipande kitakachopatikana kwa kuukulia makaa kutoka jikoni au kuchotea maji kisimani.”
Et sa chute sera comme quand on brise un vase de poterie; les fragments en sont tels qu'on n'y peut trouver un tesson à transporter du feu, ou à puiser un peu d'eau.
15 Hili ndilo Bwana Mwenyezi, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, asemalo: “Katika kutubu na kupumzika ndio wokovu wenu, katika kutulia na kutumaini ndizo nguvu zenu, lakini hamkutaka.
Voici ce que dit le Seigneur, le Seigneur saint d'Israël: Lorsque après t'être perverti tu te lamenteras, tu seras sauvé, et tu sauras où tu étais; car tu croyais en des vanités, des vanités étaient ta force, et tu n'as pas voulu m'entendre.
16 Mlisema, ‘Hapana, tutakimbia kwa farasi.’ Kwa hiyo mtakimbia! Mlisema, ‘Tutakimbia kwa farasi waendao kasi.’ Kwa hiyo wanaowafukuza watakwenda kasi!
Mais vous avez dit: nous fuirons à cheval; à cause de cela, vous fuirez. Vous avez dit: Nous serons sur des chevaux agiles; à cause de cela, ils seront agiles aussi les chevaux qui vous poursuivront.
17 Watu 1,000 watakimbia kwa ajili ya kitisho cha mtu mmoja, kwa vitishio vya watu watano wote mtakimbia, hadi mtakapoachwa kama mlingoti wa bendera juu ya kilele cha mlima, kama bendera juu ya kilima.”
Mille des vôtres fuiront à la voix d'un seul ennemi; une multitude fuira à la voix de cinq hommes, jusqu'à ce que vous restiez comme un mât sur une montagne, ou comme la hampe qui porte un étendard sur une colline.
18 Hata hivyo Bwana anatamani kutupatia neema, anainuka ili kuwaonyesha huruma. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa haki. Wamebarikiwa wote wanaomngojea yeye!
Et Dieu vous attendra encore pour vous prendre en compassion; et en cela il signalera sa gloire en vous faisant miséricorde; car le Seigneur votre Dieu est le juge. Heureux ceux qui l'attendent!
19 Enyi watu wa Sayuni, mnaoishi Yerusalemu, hamtalia tena. Tazameni jinsi atakavyokuwa na huruma mtakapolia kwa kumwomba msaada! Mara asikiapo, atawajibu.
Car le peuple saint demeurera en Sion, et Jérusalem pleurera à chaudes larmes, disant: Ayez pitié de moi! Et le Seigneur aura pitié de toi, quand il t'aura vue crier et qu'il t'aura entendue.
20 Ingawa Bwana huwapa chakula cha shida na maji ya taabu, walimu wenu hawatafichwa tena, kwa macho yenu wenyewe mtawaona.
Et le Seigneur vous donnera le pain de l'affliction et l'eau de la détresse; et ceux qui t'égarent n'approcheront plus de toi; car tes yeux verront ceux qui t'égarent.
21 Mkigeuka kuume au kushoto, masikio yenu yatasikia sauti nyuma yenu ikisema, “Hii ndiyo njia, ifuateni.”
Et tes oreilles entendront les discours de ceux qui, derrière toi, t'auront égarée, disant: Voici la voie, suivons-la, soit à droite, soit à gauche.
22 Kisha mtanajisi sanamu zenu zilizofunikwa kwa fedha, na vinyago vyenu vilivyofunikwa kwa dhahabu. Mtazitupilia mbali kama vitambaa vya wakati wa hedhi na kuziambia, “Haya, tokeni hapa!”
Alors tu souilleras les idoles argentées, et tu réduiras en poudre les idoles d'or, et tu les jetteras au loin comme l'eau des menstrues, et tu les repousseras comme la fange.
23 Pia atawapa mvua kwa ajili ya mbegu mnazootesha ardhini, chakula kinachotoka ardhini kitakuwa kizuri sana, tena tele. Katika siku ile, ngʼombe wenu watalisha katika shamba pana la majani.
Alors il tombera de la pluie sur les grains que tu auras semés; alors le pain des fruits de la terre sera plantureux et succulent. Et en ce jour tout bétail broutera dans des pâturages spacieux et fertiles.
24 Maksai na punda walimao watakula majani makavu na vyakula vilivyotengenezwa, vinavyotandazwa kwa uma na sepeto.
Et vos taureaux et vos bœufs de labour mangeront de la paille assaisonnée d'orge vannée.
25 Katika siku ile ya mauaji makuu, wakati minara itakapoanguka, vijito vya maji vitatiririka juu ya kila mlima mrefu na kila kilima kilichoinuka sana.
Et en ce jour l'eau coulera sur toute haute montagne, sur toute colline élevée, longue beaucoup d'hommes auront péri et que leurs tours seront tombées.
26 Mwezi utaangaza kama jua, nao mwanga wa jua utangʼaa mara saba zaidi, kama nuru ya siku saba, wakati Bwana atakapoyafunga majeraha ya watu wake na kuwaponya vidonda alivyowatia.
Et la lumière de la lune sera comme la lumière du soleil; et la lumière du soleil sera septuple durant le jour, lorsque le Seigneur aura pansé les meurtrissures de son peuple, et guéri les douleurs de ses plaies.
27 Tazama, Jina la Bwana linakuja kutoka mbali, likiwa na hasira kali inayowaka pamoja na wingu zito la moshi, midomo yake imejaa ghadhabu na ulimi wake ni moto ulao.
Voici que le nom du Seigneur arrive après un long temps; sa fureur est ardente; la parole de ses lèvres est pleine de gloire; sa parole est pleine de colère, et les transports de sa fureur dévorent comme le feu.
28 Pumzi yake ni kama mkondo wa maji yaendayo kasi, yakipanda hadi shingoni. Hutikisa mataifa katika chekecheke ya uharibifu, huweka lijamu katika mataya ya mataifa ambayo huwaongoza upotevuni.
Et son souffle, comme l'eau qui se précipite dans un vallon, montera jusqu'au cou; et il se divisera pour troubler les nations au sujet de leurs vaines erreurs; et l'erreur aussi les poursuivra, et les prendra en face.
29 Nanyi mtaimba kama usiku ule mnaadhimisha sikukuu takatifu. Mioyo yenu itashangilia kama vile watu wanapokwea na filimbi kwenye mlima wa Bwana, kwa Mwamba wa Israeli.
Ne devrez-vous pas alors être toujours en joie, et toujours entrer dans mes lieux saints, comme aux jours de fête? Ne devrez-vous pas, comme ceux qui se réjouissent, venir au son des flûtes sur la montagne du Seigneur, devant le Dieu d'Israël?
30 Bwana atawasababisha watu waisikie sauti yake ya utukufu, naye atawafanya wauone mkono wake ukishuka pamoja na hasira yake kali na moto ulao, kukiwa na tufani ya mvua, ngurumo za radi na mvua ya mawe.
Et le Seigneur fera entendre sa voix glorieuse, et la fureur de son bras, qui se manifestera par des transports de colère et une flamme dévorante; sa foudre éditera violemment comme de l'eau et de la grêle qui tombe avec impétuosité.
31 Sauti ya Bwana itaivunjavunja Ashuru, kwa fimbo yake ya utawala atawapiga.
Car les Assyriens seront vaincus à la voix du Seigneur, par la plaie dont il les frappera.
32 Kila pigo Bwana atakaloliweka juu yao kwa fimbo yake ya kuadhibu, litakuwa kwa wimbo wa matari na vinubi, anapopigana nao katika vita kwa mapigo ya mkono wake.
Et c'est là ce qui lui arrivera de tous les alentours, de toute contrée d'où il espérait du secours, et en qui il se confiait; les peuples, au contraire, viendront le combattre au son des tambours et des cithares.
33 Tofethi imeandaliwa toka zamani, imewekwa tayari kwa ajili ya mfalme. Shimo lake la moto limetengenezwa kwa kina kirefu na kwa upana mkubwa, likiwa na moto na kuni tele; pumzi ya Bwana, kama kijito cha kiberiti, huuwasha moto.
Car vous serez requis avant le temps, Seigneur; tout n'est-il pas préparé pour votre règne, un ravin profond, des arbres abattus, le feu et un vaste bûcher? La colère du Seigneur est comme une vallée embrasée par le soufre.

< Isaya 30 >