< Isaya 30 >

1 Bwana asema, “Ole kwa watoto wakaidi, kwa wale wanaotimiza mipango ambayo si yangu, wakifanya makubaliano, lakini si kwa Roho wangu, wakilundika dhambi juu ya dhambi,
Alas! for sons who are rebellious, Declareth Yahweh. Executing a purpose, but not from me, And pouring out a libation but not from my spirit, —That they may add sin to sin:
2 wale washukao kwenda Misri bila kutaka shauri langu, wanaotafuta msaada wa ulinzi wa Farao, watafutao kivuli cha Misri kwa ajili ya kimbilio.
Who are setting out to go down to Egypt, But at my mouth, have not asked, —Betaking them to the protection of Pharaoh And seeking refuge under the shadow of Egypt.
3 Lakini ulinzi wa Farao utakuwa kwa aibu yenu, kivuli cha Misri kitawaletea fedheha.
Therefore shall the protection of Pharaoh become to you a shame, And, the refuge in the shadow of Egypt, an insult;
4 Ingawa wana maafisa katika Soani na wajumbe wamewasili katika Hanesi,
For their princes have been, in Zoan, —And, their messengers unto Hanes, would draw near.
5 kila mmoja ataaibishwa kwa sababu ya taifa lisilowafaa kitu, ambalo haliwaletei msaada wala faida, bali aibu tu na fedheha.”
Every one, hath felt ashamed of a people that could not serve them, —Neither with help, nor with service, But they are a shame, yea even a reproach.
6 Neno kuhusu wanyama wa Negebu: Katika nchi ya taabu na shida, ya simba za dume na jike, ya nyoka mwenye sumu kali na nyoka warukao, wajumbe huchukua utajiri wao juu ya migongo ya punda, hazina zao juu ya nundu za ngamia, kwa lile taifa lisilokuwa na faida,
The Oracle on the Beasts of the South, —Through a land of distress and oppression—Lioness and lion coming therefrom, Viper and fiery flying serpent, They would carry, on the shoulders of young asses their wealth And on the humps of camels their treasures Unto a people that cannot serve them.
7 kuvipeleka Misri, ambaye msaada wake haufai kabisa. Kwa hiyo nimemwita “Rahabu Asiyefanya Chochote.”
But, the Egyptians, with vanity and emptiness, would help, —Therefore have I proclaimed concerning this, Insolent, they sit still!
8 Nenda sasa, liandike neno hili juu ya kibao kwa ajili yao, liandike kwenye kitabu, ili liweze kuwa shahidi milele kwa ajili ya siku zijazo.
Now, enter—Write it upon a tablet before them And upon a scroll, inscribe it, —That it may serve for a later day, For futurity, unto times age-abiding: —
9 Hawa ni watu waasi, watoto wadanganyifu, watoto ambao hawataki kusikiliza mafundisho ya Bwana.
That it is, a rebellious people, Sons apt at deceiving, —Sons unwilling to hear the law of Yahweh:
10 Wanawaambia waonaji, “Msione maono tena!” Nako kwa manabii wanasema, “Msiendelee kutupatia maono ambayo ni ya kweli! Tuambieni mambo ya kupendeza, tabirini mambo ya uongo.
Who have said to the seers, Ye must not see! To the prophets, Ye must not prophesy to us reproofs! Speak to us smooth things, Prophesy delusions:
11 Acheni njia hii, ondokeni katika mapito haya, nanyi acheni kutukabili pamoja na yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli!”
Depart ye from the way, Turn aside from the path, —Desist from setting before us the Holy One of Israel.
12 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa sababu mmekataa ujumbe huu, mkategemea uonevu na kutumainia udanganyifu,
Therefore—Thus, saith the Holy One of Israel, Because ye have rejected this word, —And have trusted in oppression and perverseness, And have relied thereon,
13 dhambi hii itakuwa kwenu kama ukuta mrefu, wenye ufa na wenye kubetuka, ambao unaanguka ghafula, mara moja.
Therefore, shall this iniquity become to you As a breach ready to fall, A bulging in a high wall, —Whose breaking down cometh, suddenly in a twinkling.
14 Utavunjika vipande vipande kama chombo cha udongo ukipasuka pasipo huruma ambapo katika vipande vyake hakuna kipande kitakachopatikana kwa kuukulia makaa kutoka jikoni au kuchotea maji kisimani.”
Yea he will break it—as the breaking of the pitcher of a potter, crushed, he will not spare; So that there shall not be found when it is smashed, A sherd wherewith to snatch fire from a hearth, Or to skim off water out of a cistern.
15 Hili ndilo Bwana Mwenyezi, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, asemalo: “Katika kutubu na kupumzika ndio wokovu wenu, katika kutulia na kutumaini ndizo nguvu zenu, lakini hamkutaka.
For thus, said my Lord Yahweh, the Holy One of Israel—By returning and resting, shall ye be saved, In keeping quiet and trusting, shall be your strength, —Howbeit ye would not!
16 Mlisema, ‘Hapana, tutakimbia kwa farasi.’ Kwa hiyo mtakimbia! Mlisema, ‘Tutakimbia kwa farasi waendao kasi.’ Kwa hiyo wanaowafukuza watakwenda kasi!
But ye said, —Nay! but on horses, will we flee For this cause, shall ye indeed flee, —And on the swift, will we ride, For this cause, swift, shall be your pursuers:
17 Watu 1,000 watakimbia kwa ajili ya kitisho cha mtu mmoja, kwa vitishio vya watu watano wote mtakimbia, hadi mtakapoachwa kama mlingoti wa bendera juu ya kilele cha mlima, kama bendera juu ya kilima.”
One thousand, before the war-cry of one—before the war-cry of five, shall ye flee, —Until ye have been left, As a pole on the top of a mountain, And as an ensign upon a hill.
18 Hata hivyo Bwana anatamani kutupatia neema, anainuka ili kuwaonyesha huruma. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa haki. Wamebarikiwa wote wanaomngojea yeye!
And, therefore, will Yahweh wait, That he may grant you favour, And, therefore, will he lift himself up, That he may show you compassion, —For A God of justice, is, Yahweh, How happy all they who are waiting for him
19 Enyi watu wa Sayuni, mnaoishi Yerusalemu, hamtalia tena. Tazameni jinsi atakavyokuwa na huruma mtakapolia kwa kumwomba msaada! Mara asikiapo, atawajibu.
For, a people, In Zion, shall dwell, In Jerusalem, —As for weeping, thou shalt not weep! As for favour, he will grant thee favour, at the sound of thine outcry, —As soon as he heareth, he hath answered thee!
20 Ingawa Bwana huwapa chakula cha shida na maji ya taabu, walimu wenu hawatafichwa tena, kwa macho yenu wenyewe mtawaona.
Though My Lord, should give you bread in short measure and water in scant allowance Yet will thy Teacher not hide himself any more, But thine eyes shall ever be looking on thy Teacher.
21 Mkigeuka kuume au kushoto, masikio yenu yatasikia sauti nyuma yenu ikisema, “Hii ndiyo njia, ifuateni.”
So shall, thine own ears, hear a word from behind thee saying, —This, is the way, walk ye therein, When ye would turn to the right hand Or when ye would turn to the left.
22 Kisha mtanajisi sanamu zenu zilizofunikwa kwa fedha, na vinyago vyenu vilivyofunikwa kwa dhahabu. Mtazitupilia mbali kama vitambaa vya wakati wa hedhi na kuziambia, “Haya, tokeni hapa!”
Then will ye defile—The overlaying of thy graven images of silver, And the coating of thy molten image, of gold, —Thou wilt cash them away, as a woman the token of her sickness, Begone! shalt thou say thereto,
23 Pia atawapa mvua kwa ajili ya mbegu mnazootesha ardhini, chakula kinachotoka ardhini kitakuwa kizuri sana, tena tele. Katika siku ile, ngʼombe wenu watalisha katika shamba pana la majani.
Then will he give—Rain for thy seed—wherewith thou shalt sow thy ground and Bread as the increase of thy ground, which shall be fertile and fat, —Thy cattle, in that day, shall feed in broad pasture:
24 Maksai na punda walimao watakula majani makavu na vyakula vilivyotengenezwa, vinavyotandazwa kwa uma na sepeto.
And the oxen and the young asses that till the ground, salted provender, shall eat, which hath been winnowed with shovel or fan.
25 Katika siku ile ya mauaji makuu, wakati minara itakapoanguka, vijito vya maji vitatiririka juu ya kila mlima mrefu na kila kilima kilichoinuka sana.
Then shall there be, On every lofty mountain and On every lifted hill, Channels, Conduits of water, —In the great day of slaughter, When the towers fall.
26 Mwezi utaangaza kama jua, nao mwanga wa jua utangʼaa mara saba zaidi, kama nuru ya siku saba, wakati Bwana atakapoyafunga majeraha ya watu wake na kuwaponya vidonda alivyowatia.
Then shall the light of the moon, be as the light of the sun, And, the light of the sun, shall be sevenfold, as the light of seven days, —In the day—When Yahweh, bindeth up, the laceration of his people, and When the severe wound caused by smiting them, he healeth.
27 Tazama, Jina la Bwana linakuja kutoka mbali, likiwa na hasira kali inayowaka pamoja na wingu zito la moshi, midomo yake imejaa ghadhabu na ulimi wake ni moto ulao.
Lo! the Name of Yahweh, coming in from afar, His anger kindling, A heavy storm, —His lips, are full of indignation, And, his tongue, is like a fire that devoureth;
28 Pumzi yake ni kama mkondo wa maji yaendayo kasi, yakipanda hadi shingoni. Hutikisa mataifa katika chekecheke ya uharibifu, huweka lijamu katika mataya ya mataifa ambayo huwaongoza upotevuni.
And, his breath like an overflowing torrent, even unto the neck, doth reach, To sift nations with a sieve of calamity, —A bridle leading to ruin, being upon the jaws of the peoples.
29 Nanyi mtaimba kama usiku ule mnaadhimisha sikukuu takatifu. Mioyo yenu itashangilia kama vile watu wanapokwea na filimbi kwenye mlima wa Bwana, kwa Mwamba wa Israeli.
A song, shall ye have, As in the night of hallowing a festival, —And gladness of heart, As when one goeth with the flute to enter Into the mountain of Yahweh Unto the Rock of Israel.
30 Bwana atawasababisha watu waisikie sauti yake ya utukufu, naye atawafanya wauone mkono wake ukishuka pamoja na hasira yake kali na moto ulao, kukiwa na tufani ya mvua, ngurumo za radi na mvua ya mawe.
Then will Yahweh cause to be heard—the resounding of his voice And the bringing down of his arm, shall be seen, In a rage of anger, And with the flame of a devouring fire, —A burst and a downpour, and a hailstone!
31 Sauti ya Bwana itaivunjavunja Ashuru, kwa fimbo yake ya utawala atawapiga.
For at the voice of Yahweh, shall Assyria be crushed, —With his rod, will he smite.
32 Kila pigo Bwana atakaloliweka juu yao kwa fimbo yake ya kuadhibu, litakuwa kwa wimbo wa matari na vinubi, anapopigana nao katika vita kwa mapigo ya mkono wake.
And it shall come to pass, —that, every stroke of the staff of doom which Yahweh shall lay upon him, shall be with timbrels and with lyres, —when, with battles of brandished weapons, he hath fought against them.
33 Tofethi imeandaliwa toka zamani, imewekwa tayari kwa ajili ya mfalme. Shimo lake la moto limetengenezwa kwa kina kirefu na kwa upana mkubwa, likiwa na moto na kuni tele; pumzi ya Bwana, kama kijito cha kiberiti, huuwasha moto.
For there hath been set in order, beforehand a Topheth, Yea, the same, for the king, hath been prepared He hath made it deep—made it large, —The circumference thereof is for fire and wood in abundance, the breath of Yahweh, like a torrent of brimstone, is ready to kindle it.

< Isaya 30 >