< Isaya 30 >

1 Bwana asema, “Ole kwa watoto wakaidi, kwa wale wanaotimiza mipango ambayo si yangu, wakifanya makubaliano, lakini si kwa Roho wangu, wakilundika dhambi juu ya dhambi,
“Woe to the sons of apostasy!” says the Lord. For you would take advice, but not from me. And you would begin to weave, but not by my spirit. Thus do you add sin upon sin!
2 wale washukao kwenda Misri bila kutaka shauri langu, wanaotafuta msaada wa ulinzi wa Farao, watafutao kivuli cha Misri kwa ajili ya kimbilio.
You are walking so as to descend into Egypt, and you have not sought answers from my mouth, instead hoping for assistance from the strength of Pharaoh and placing trust in the shadow of Egypt.
3 Lakini ulinzi wa Farao utakuwa kwa aibu yenu, kivuli cha Misri kitawaletea fedheha.
And so, the strength of Pharaoh will be your confusion, and trust in the shadow of Egypt will be your disgrace.
4 Ingawa wana maafisa katika Soani na wajumbe wamewasili katika Hanesi,
For your leaders were at Tanis, and your messengers have traveled even as far as Hanes.
5 kila mmoja ataaibishwa kwa sababu ya taifa lisilowafaa kitu, ambalo haliwaletei msaada wala faida, bali aibu tu na fedheha.”
They have all been confounded because of a people who were not able to offer profit to them, who were not of assistance, nor of other usefulness, except to offer confusion and reproach.
6 Neno kuhusu wanyama wa Negebu: Katika nchi ya taabu na shida, ya simba za dume na jike, ya nyoka mwenye sumu kali na nyoka warukao, wajumbe huchukua utajiri wao juu ya migongo ya punda, hazina zao juu ya nundu za ngamia, kwa lile taifa lisilokuwa na faida,
The burden of the beasts in the south. In a land of tribulation and anguish, from which go forth the lioness and the lion, the viper and the flying king snake, they carry their riches upon the shoulders of beasts of burden, and their valuables upon the humps of camels, to a people who are not able to offer profit to them.
7 kuvipeleka Misri, ambaye msaada wake haufai kabisa. Kwa hiyo nimemwita “Rahabu Asiyefanya Chochote.”
For Egypt will offer assistance, but without purpose or success. Therefore, concerning this, I cried out: “It is only arrogance! Remain calm.”
8 Nenda sasa, liandike neno hili juu ya kibao kwa ajili yao, liandike kwenye kitabu, ili liweze kuwa shahidi milele kwa ajili ya siku zijazo.
Now, therefore, enter and write for them upon a tablet, and note it diligently in a book, and this shall be a testimony in the last days, and even unto eternity.
9 Hawa ni watu waasi, watoto wadanganyifu, watoto ambao hawataki kusikiliza mafundisho ya Bwana.
For they are a people who provoke to wrath, and they are lying sons, sons unwilling to listen to the law of God.
10 Wanawaambia waonaji, “Msione maono tena!” Nako kwa manabii wanasema, “Msiendelee kutupatia maono ambayo ni ya kweli! Tuambieni mambo ya kupendeza, tabirini mambo ya uongo.
They say to the seers, “Do not see,” and to those who behold: “Do not behold for us the things that are right. Speak to us of pleasing things. See errors for us.
11 Acheni njia hii, ondokeni katika mapito haya, nanyi acheni kutukabili pamoja na yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli!”
Take me from the way. Avert me from the path. Let the Holy One of Israel cease from before our face.”
12 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa sababu mmekataa ujumbe huu, mkategemea uonevu na kutumainia udanganyifu,
Because of this, thus says the Holy One of Israel: Since you have rejected this word, and you have hoped in calumny and rebellion, and since you have depended upon these things,
13 dhambi hii itakuwa kwenu kama ukuta mrefu, wenye ufa na wenye kubetuka, ambao unaanguka ghafula, mara moja.
for this reason, this iniquity will be to you like a breach that has fallen, and like a gap in a high wall. For its destruction will happen suddenly, when it is not expected.
14 Utavunjika vipande vipande kama chombo cha udongo ukipasuka pasipo huruma ambapo katika vipande vyake hakuna kipande kitakachopatikana kwa kuukulia makaa kutoka jikoni au kuchotea maji kisimani.”
And it will be crushed, just as the earthen vessel of a potter is destroyed by a sharp blow. And not even a fragment of its earthenware will be found, which might carry a little fire from the hearth, or which might draw a little water from a hollow.
15 Hili ndilo Bwana Mwenyezi, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, asemalo: “Katika kutubu na kupumzika ndio wokovu wenu, katika kutulia na kutumaini ndizo nguvu zenu, lakini hamkutaka.
For thus says the Lord God, the Holy One of Israel: If you return and are quiet, you shall be saved. Your strength will be found in silence and in hope. But you are not willing!
16 Mlisema, ‘Hapana, tutakimbia kwa farasi.’ Kwa hiyo mtakimbia! Mlisema, ‘Tutakimbia kwa farasi waendao kasi.’ Kwa hiyo wanaowafukuza watakwenda kasi!
And you have said: “Never! Instead, we will flee by horseback.” For this reason, you will be put to flight. And you have said, “We will climb upon swift ones.” For this reason, those who pursue you will be even swifter.
17 Watu 1,000 watakimbia kwa ajili ya kitisho cha mtu mmoja, kwa vitishio vya watu watano wote mtakimbia, hadi mtakapoachwa kama mlingoti wa bendera juu ya kilele cha mlima, kama bendera juu ya kilima.”
A thousand men will flee in terror from the face of one, and you will flee in terror from the face of five, until you who have been left behind are like the mast of a ship at the top of a mountain, or like a sign on a hill.
18 Hata hivyo Bwana anatamani kutupatia neema, anainuka ili kuwaonyesha huruma. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa haki. Wamebarikiwa wote wanaomngojea yeye!
Therefore, the Lord waits, so that he may take pity on you. And therefore, he will be exalted for sparing you. For the Lord is the God of judgment. Blessed are all those who wait for him.
19 Enyi watu wa Sayuni, mnaoishi Yerusalemu, hamtalia tena. Tazameni jinsi atakavyokuwa na huruma mtakapolia kwa kumwomba msaada! Mara asikiapo, atawajibu.
For the people of Zion will live in Jerusalem. Bitterly, you will not weep. Mercifully, he will take pity on you. At the voice of your outcry, as soon as he hears, he will respond to you.
20 Ingawa Bwana huwapa chakula cha shida na maji ya taabu, walimu wenu hawatafichwa tena, kwa macho yenu wenyewe mtawaona.
And the Lord will give you thick bread and accessible water. And he will not cause your teacher to fly away from you anymore. And your eyes will behold your instructor.
21 Mkigeuka kuume au kushoto, masikio yenu yatasikia sauti nyuma yenu ikisema, “Hii ndiyo njia, ifuateni.”
And your ears will listen to the word of one admonishing you behind your back: “This is the way! Walk in it! And do not turn aside, neither to the right, nor to the left.”
22 Kisha mtanajisi sanamu zenu zilizofunikwa kwa fedha, na vinyago vyenu vilivyofunikwa kwa dhahabu. Mtazitupilia mbali kama vitambaa vya wakati wa hedhi na kuziambia, “Haya, tokeni hapa!”
And you will defile the plates of your silver graven images and the vestment of your gold molten idols. And you will throw these things away like the uncleanness of a menstruating woman. You will say to it, “Go away!”
23 Pia atawapa mvua kwa ajili ya mbegu mnazootesha ardhini, chakula kinachotoka ardhini kitakuwa kizuri sana, tena tele. Katika siku ile, ngʼombe wenu watalisha katika shamba pana la majani.
And wherever you sow seed upon the earth, rain will be given to the seed. And bread from the grain of the earth will be very plentiful and full. In that day, the lamb will pasture in the spacious land of your possession.
24 Maksai na punda walimao watakula majani makavu na vyakula vilivyotengenezwa, vinavyotandazwa kwa uma na sepeto.
And your bulls, and the colts of the donkeys that work the ground, will eat a mix of grains like that winnowed on the threshing floor.
25 Katika siku ile ya mauaji makuu, wakati minara itakapoanguka, vijito vya maji vitatiririka juu ya kila mlima mrefu na kila kilima kilichoinuka sana.
And there will be, on every lofty mountain, and on every elevated hill, rivers of running water, in the day of the slaughter of many, when the tower will fall.
26 Mwezi utaangaza kama jua, nao mwanga wa jua utangʼaa mara saba zaidi, kama nuru ya siku saba, wakati Bwana atakapoyafunga majeraha ya watu wake na kuwaponya vidonda alivyowatia.
And the light of the moon will be like the light of the sun, and the light of the sun will be sevenfold, like the light of seven days, in the day when the Lord will bind the wound of his people, and when he will heal the stroke of their scourge.
27 Tazama, Jina la Bwana linakuja kutoka mbali, likiwa na hasira kali inayowaka pamoja na wingu zito la moshi, midomo yake imejaa ghadhabu na ulimi wake ni moto ulao.
Behold, the name of the Lord arrives from far away. His fury is burning and heavy to bear. His lips have been filled with indignation, and his tongue is like a devouring fire.
28 Pumzi yake ni kama mkondo wa maji yaendayo kasi, yakipanda hadi shingoni. Hutikisa mataifa katika chekecheke ya uharibifu, huweka lijamu katika mataya ya mataifa ambayo huwaongoza upotevuni.
His Spirit is like a torrent, inundating, even as high as the middle of the neck, in order to reduce the nations to nothing, along with the bridle of error that was in the jaws of the people.
29 Nanyi mtaimba kama usiku ule mnaadhimisha sikukuu takatifu. Mioyo yenu itashangilia kama vile watu wanapokwea na filimbi kwenye mlima wa Bwana, kwa Mwamba wa Israeli.
There will be a song for you, as in the night of a sanctified solemnity, and a joy of heart, as when one travels with music to arrive at the mountain of the Lord, to the Strong One of Israel.
30 Bwana atawasababisha watu waisikie sauti yake ya utukufu, naye atawafanya wauone mkono wake ukishuka pamoja na hasira yake kali na moto ulao, kukiwa na tufani ya mvua, ngurumo za radi na mvua ya mawe.
And the Lord will cause the glory of his voice to be heard, and, with a threatening fury and a devouring flame of fire, he will reveal the terror of his arm. He will crush with the whirlwind and with hailstones.
31 Sauti ya Bwana itaivunjavunja Ashuru, kwa fimbo yake ya utawala atawapiga.
For at the voice of the Lord, Assur will dread being struck with the staff.
32 Kila pigo Bwana atakaloliweka juu yao kwa fimbo yake ya kuadhibu, litakuwa kwa wimbo wa matari na vinubi, anapopigana nao katika vita kwa mapigo ya mkono wake.
And when the passage of the staff has been begun, the Lord will cause it to rest upon him, with timbrels and harps. And with special battles, he will fight against them.
33 Tofethi imeandaliwa toka zamani, imewekwa tayari kwa ajili ya mfalme. Shimo lake la moto limetengenezwa kwa kina kirefu na kwa upana mkubwa, likiwa na moto na kuni tele; pumzi ya Bwana, kama kijito cha kiberiti, huuwasha moto.
For a burning place, deep and wide, has been prepared from yesterday, prepared by the King. Its nourishment is fire and much wood. The breath of the Lord, like a torrent of brimstone, kindles it.

< Isaya 30 >