< Isaya 30 >
1 Bwana asema, “Ole kwa watoto wakaidi, kwa wale wanaotimiza mipango ambayo si yangu, wakifanya makubaliano, lakini si kwa Roho wangu, wakilundika dhambi juu ya dhambi,
Běda synům zpurným, dí Hospodin, skládajícím radu, kteráž není ze mne, a přikrývajícím ji přikrytím, ale ne z ducha mého, aby hřích k hříchu přidávali;
2 wale washukao kwenda Misri bila kutaka shauri langu, wanaotafuta msaada wa ulinzi wa Farao, watafutao kivuli cha Misri kwa ajili ya kimbilio.
Kteříž chodí a sstupují do Egypta, nedotazujíce se úst mých, aby se zmocňovali v síle Faraonově, a doufali v stínu Egyptském.
3 Lakini ulinzi wa Farao utakuwa kwa aibu yenu, kivuli cha Misri kitawaletea fedheha.
Nebo síla Faraonova bude vám k hanbě, a to odpočívání v stínu Egyptském k lehkosti,
4 Ingawa wana maafisa katika Soani na wajumbe wamewasili katika Hanesi,
Proto že knížata jeho byli v Soan, a poslové jeho do Chanes chodili.
5 kila mmoja ataaibishwa kwa sababu ya taifa lisilowafaa kitu, ambalo haliwaletei msaada wala faida, bali aibu tu na fedheha.”
Všeckyť k zahanbení přivede skrze lid, kterýž jim nic neprospěje, aniž bude ku pomoci, ani k užitku, ale k hanbě toliko a k útržce.
6 Neno kuhusu wanyama wa Negebu: Katika nchi ya taabu na shida, ya simba za dume na jike, ya nyoka mwenye sumu kali na nyoka warukao, wajumbe huchukua utajiri wao juu ya migongo ya punda, hazina zao juu ya nundu za ngamia, kwa lile taifa lisilokuwa na faida,
Břímě hovad poledních v zemi nátisku a ssoužení, odkudž lev a lvíče, ještěrka a drak ohnivý létající, odnesou na hřbetě hovádek bohatství svá, a na hrbu velbloudů poklady své k lidu, kterýž jim nic neprospěje.
7 kuvipeleka Misri, ambaye msaada wake haufai kabisa. Kwa hiyo nimemwita “Rahabu Asiyefanya Chochote.”
Nebo Egyptští nadarmo a na prázdno pomáhati budou. Pročež ohlašuji to, že by síla jejich byla s pokojem seděti.
8 Nenda sasa, liandike neno hili juu ya kibao kwa ajili yao, liandike kwenye kitabu, ili liweze kuwa shahidi milele kwa ajili ya siku zijazo.
Nyní jdi, napiš to na tabuli před očima jejich, a na knize vyrej to, aby to zůstávalo do nejposlednějšího dne, a až na věky věků,
9 Hawa ni watu waasi, watoto wadanganyifu, watoto ambao hawataki kusikiliza mafundisho ya Bwana.
Že lid tento zpurný jest, synové lháři, synové, kteříž nechtí poslouchati zákona Hospodinova;
10 Wanawaambia waonaji, “Msione maono tena!” Nako kwa manabii wanasema, “Msiendelee kutupatia maono ambayo ni ya kweli! Tuambieni mambo ya kupendeza, tabirini mambo ya uongo.
Kteříž říkají vidoucím: Nemívejte vidění, a prorokům: Neprorokujte nám toho, což pravého jest; mluvte nám pochlebenství, prorokujte oklamání.
11 Acheni njia hii, ondokeni katika mapito haya, nanyi acheni kutukabili pamoja na yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli!”
Sejděte s cesty, svozujte od stezky, nechať se vzdálí od tváří naší Svatý Izraelský.
12 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa sababu mmekataa ujumbe huu, mkategemea uonevu na kutumainia udanganyifu,
Protož takto praví Svatý Izraelský: Proto že pohrdáte slovem tím, a doufáte ve lsti a v převrácenosti, a spoléháte na ni:
13 dhambi hii itakuwa kwenu kama ukuta mrefu, wenye ufa na wenye kubetuka, ambao unaanguka ghafula, mara moja.
Z té příčiny bude vám tato nepravost jako zed tržená padající, a vydutí na zdi vysoké, jejíž brzké a náhlé bývá oboření.
14 Utavunjika vipande vipande kama chombo cha udongo ukipasuka pasipo huruma ambapo katika vipande vyake hakuna kipande kitakachopatikana kwa kuukulia makaa kutoka jikoni au kuchotea maji kisimani.”
A rozrazí ji, jako rozrážejí nádobu hrnčířskou rozbitou; neodpustíť, tak že nebude nalezena po rozražení jejím ani střepina k nabrání ohně z ohniště, anebo k nabrání vody z louže.
15 Hili ndilo Bwana Mwenyezi, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, asemalo: “Katika kutubu na kupumzika ndio wokovu wenu, katika kutulia na kutumaini ndizo nguvu zenu, lakini hamkutaka.
Nebo tak řekl Panovník Hospodin, Svatý Izraelský: Obrátíte-li se, a spokojíte-li se, zachováni budete. V utišení se a v doufání bude síla vaše. Ale nechcete.
16 Mlisema, ‘Hapana, tutakimbia kwa farasi.’ Kwa hiyo mtakimbia! Mlisema, ‘Tutakimbia kwa farasi waendao kasi.’ Kwa hiyo wanaowafukuza watakwenda kasi!
Nýbrž říkáte: Nikoli, ale na koních utečeme. Protož utíkati budete. Na rychlých ujedeme. Ale rychlejší budou stihající vás.
17 Watu 1,000 watakimbia kwa ajili ya kitisho cha mtu mmoja, kwa vitishio vya watu watano wote mtakimbia, hadi mtakapoachwa kama mlingoti wa bendera juu ya kilele cha mlima, kama bendera juu ya kilima.”
Jeden tisíc před okřiknutím jednoho, a před okřiknutím pěti utíkati budete, až (jestliže však vás co pozůstane), budete zanecháni jako okleštěné dřevo na vrchu hory, a jako korouhev na pahrbku.
18 Hata hivyo Bwana anatamani kutupatia neema, anainuka ili kuwaonyesha huruma. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa haki. Wamebarikiwa wote wanaomngojea yeye!
Protoť pak shovívá Hospodin, milost vám čině, a protoť se vyvýší, aby se smiloval nad vámi; nebo Hospodin jest Bůh spravedlivý. Blahoslavení všickni, kteříž očekávají na něj.
19 Enyi watu wa Sayuni, mnaoishi Yerusalemu, hamtalia tena. Tazameni jinsi atakavyokuwa na huruma mtakapolia kwa kumwomba msaada! Mara asikiapo, atawajibu.
Lid zajisté na Sionu a v Jeruzalémě bydliti bude. Nikoli plakati nebudeš; k hlasu volání tvého bude všelijak milost činiti s tebou. Hned jakž uslyší, ohlásíť se.
20 Ingawa Bwana huwapa chakula cha shida na maji ya taabu, walimu wenu hawatafichwa tena, kwa macho yenu wenyewe mtawaona.
A ačkoli Pán dá vám chleba úzkosti a vody ssoužení, však nebudou více odjati tobě učitelé tvoji, ale očima svýma vídati budeš učitele své,
21 Mkigeuka kuume au kushoto, masikio yenu yatasikia sauti nyuma yenu ikisema, “Hii ndiyo njia, ifuateni.”
A ušima svýma slýchati slovo tobě po zadu řkoucích: Toť jest ta cesta, choďte po ní, buď že byste se na pravo neb na levo uchýlili.
22 Kisha mtanajisi sanamu zenu zilizofunikwa kwa fedha, na vinyago vyenu vilivyofunikwa kwa dhahabu. Mtazitupilia mbali kama vitambaa vya wakati wa hedhi na kuziambia, “Haya, tokeni hapa!”
Tedy zavržete obestření rytin svých stříbrných, a oděv slitin svých zlatých; odloučíš je jako nemoc svou trpící, řka jim: Táhněte tam.
23 Pia atawapa mvua kwa ajili ya mbegu mnazootesha ardhini, chakula kinachotoka ardhini kitakuwa kizuri sana, tena tele. Katika siku ile, ngʼombe wenu watalisha katika shamba pana la majani.
Dáť i déšť na rozsívání tvé, kterýmž bys osíval zemi, a chléb z úrody země, kterýž bude jadrný a zdárný; v ten den pásti se bude i dobytek tvůj na pastvišti širokém.
24 Maksai na punda walimao watakula majani makavu na vyakula vilivyotengenezwa, vinavyotandazwa kwa uma na sepeto.
Volové také i oslové, dělající zemi, píci čistou jísti budou, kteráž opálkou a věječkou vyčištěna bývá.
25 Katika siku ile ya mauaji makuu, wakati minara itakapoanguka, vijito vya maji vitatiririka juu ya kila mlima mrefu na kila kilima kilichoinuka sana.
Budou také na všeliké hoře vysoké, a na všelikém pahrbku vyvýšeném pramenové a potokové vod, v den porážky veliké, když padnou věže.
26 Mwezi utaangaza kama jua, nao mwanga wa jua utangʼaa mara saba zaidi, kama nuru ya siku saba, wakati Bwana atakapoyafunga majeraha ya watu wake na kuwaponya vidonda alivyowatia.
Bude i světlo měsíce jako světlo slunce, světlo pak slunce bude sedmernásobní, jako světlo sedmi dnů, v den, v kterýž uváže Hospodin zlámání lidu svého, a ránu zbití jeho uzdraví.
27 Tazama, Jina la Bwana linakuja kutoka mbali, likiwa na hasira kali inayowaka pamoja na wingu zito la moshi, midomo yake imejaa ghadhabu na ulimi wake ni moto ulao.
Aj, jméno Hospodinovo přichází z daleka, jehožto hněv hořící a těžká pomsta; rtové jeho naplněni jsou prchlivostí, a jazyk jeho jako oheň sžírající.
28 Pumzi yake ni kama mkondo wa maji yaendayo kasi, yakipanda hadi shingoni. Hutikisa mataifa katika chekecheke ya uharibifu, huweka lijamu katika mataya ya mataifa ambayo huwaongoza upotevuni.
Duch pak jeho jako potok rozvodnilý, kterýž až do hrdla dosáhne, aby tříbil národy, až by v nic obráceni byli, a uzdou svíral čelisti národů.
29 Nanyi mtaimba kama usiku ule mnaadhimisha sikukuu takatifu. Mioyo yenu itashangilia kama vile watu wanapokwea na filimbi kwenye mlima wa Bwana, kwa Mwamba wa Israeli.
I budete zpívati, jako když se v noci zasvěcuje slavnost, a veseliti se srdečně, jako ten, kterýž jde s píšťalkou, bera se na horu Hospodinovu, k skále Izraelově,
30 Bwana atawasababisha watu waisikie sauti yake ya utukufu, naye atawafanya wauone mkono wake ukishuka pamoja na hasira yake kali na moto ulao, kukiwa na tufani ya mvua, ngurumo za radi na mvua ya mawe.
Když dá slyšeti Hospodin hlas důstojnosti své, a ukáže vztaženou ruku svou s hněvem prchlivosti a plamenem ohně sžírajícího, an vše rozráží i přívalem i kamenným krupobitím.
31 Sauti ya Bwana itaivunjavunja Ashuru, kwa fimbo yake ya utawala atawapiga.
Hlasem zajisté Hospodinovým potřín bude Assur, kterýž jiné kyjem bijíval.
32 Kila pigo Bwana atakaloliweka juu yao kwa fimbo yake ya kuadhibu, litakuwa kwa wimbo wa matari na vinubi, anapopigana nao katika vita kwa mapigo ya mkono wake.
Ale stane se, že každé udeření holí, kterouž doloží na něj Hospodin, silně dolehne; s bubny a harfami a bitvou veselou bojovati bude proti němu.
33 Tofethi imeandaliwa toka zamani, imewekwa tayari kwa ajili ya mfalme. Shimo lake la moto limetengenezwa kwa kina kirefu na kwa upana mkubwa, likiwa na moto na kuni tele; pumzi ya Bwana, kama kijito cha kiberiti, huuwasha moto.
Nebo připraveno jest již dávno peklo, také i samému králi připraveno jest. Hluboké a široké je učinil, hranic jeho, ohně a dříví mnoho; dmýchání Hospodinovo jako potoksiry je zapaluje. ()