< Isaya 3 >

1 Tazama sasa, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yu karibu kuwaondolea Yerusalemu na Yuda upatikanaji wa mahitaji na misaada, upatikanaji wote wa chakula na tegemeo lote la maji,
Porque eis que o Senhor DEUS dos exércitos tirará de Jerusalém e de Judá o apoio e o sustento: todas as fontes de comida e de água,
2 shujaa na mtu wa vita, mwamuzi na nabii, mwaguzi na mzee,
O guerreiro, o soldado, o juiz, o profeta, o adivinho, e o ancião;
3 jemadari wa kikosi cha watu hamsini na mtu mwenye cheo, mshauri, fundi stadi na mlozi mjanja.
O chefe de cinquenta, o nobre, o conselheiro, o sábio entre os artífices, e o que tem habilidade de falar palavras.
4 Nitawafanya wavulana wawe maafisa wao, watoto ndio watakaowatawala.
E [lhes] darei garotos como seus príncipes, e rapazes dominarão sobre eles.
5 Watu wataoneana wao kwa wao: mtu dhidi ya mtu, na jirani dhidi ya jirani yake. Kijana atainuka dhidi ya mzee, mtu mnyonge dhidi ya mtu mwenye heshima.
E o povo será oprimido; um será contra o outro, e cada um contra seu próximo; o jovem se atreverá contra o ancião, e o reles contra o nobre.
6 Mtu atamkamata mmoja wa ndugu zake katika nyumba ya baba yake na kusema, “Unalo joho, sasa uwe kiongozi wetu, tawala lundo hili la magofu!”
Porque um homem tomará seu irmão da casa de seu pai, [e dirá]: Tu tens capa; sê nosso governante, e estejam estas ruínas debaixo de tua mão.
7 Lakini siku hiyo atapiga kelele akisema, “Sina uponyaji. Sina chakula wala mavazi katika nyumba yangu, msinifanye niwe kiongozi wa watu.”
[Então] em tal dia ele levantará sua mão, dizendo: Não posso solucionar este problema; também em minha casa não há pão nem vestido algum; não me ponhais como governante do povo.
8 Yerusalemu inapepesuka, Yuda inaanguka; maneno yao na matendo yao ni kinyume na Bwana, wakiudharau uwepo wake uliotukuka.
Porque Jerusalém tropeçou, e Judá está caído; pois sua língua e suas obras são contra o SENHOR, para irritar os seus gloriosos olhos.
9 Nyuso zao zinavyoonekana zinashuhudia dhidi yao, hujivunia dhambi yao kama Sodoma, wala hawaifichi. Ole wao! Wamejiletea maafa juu yao wenyewe.
A aparência de seus rostos dão testemunho contra eles, e mostram abertamente seus pecados; assim como Sodoma, não os disfarçam. Ai da alma deles, porque estão fazendo mal a si mesmos.
10 Waambie wanyofu itakuwa heri kwao, kwa kuwa watafurahia tunda la matendo yao.
Dizei a justo, que o bem [lhe sucederá], que comerão do fruto de suas obras.
11 Ole kwa watu waovu! Maafa yapo juu yao! Watalipwa kwa ajili ya yale mikono yao iliyotenda.
Ai do perverso! O mal [lhe sucederá], porque lhe será feito conforme o trabalho de suas mãos.
12 Vijana wanawatesa watu wangu, wanawake wanawatawala. Enyi watu wangu, viongozi wenu wanawapotosha, wanawapoteza njia.
Os dominadores de meu povo são garotos, e mulheres dominam sobre ele; ah, meu povo, os que te guiam te enganam e confundem o caminho de tuas veredas.
13 Bwana anachukua nafasi yake mahakamani, anasimama kuhukumu watu.
O SENHOR se apresenta para brigar a causa judicial, e se põe para julgar aos povos.
14 Bwana anaingia katika hukumu dhidi ya wazee na viongozi wa watu wake: “Ninyi ndio mlioharibu shamba langu la mizabibu, mali zilizonyangʼanywa maskini zimo nyumbani mwenu.
O SENHOR vem a juízo contra os anciãos de seu povo, e [contra] seus líderes: Pois vós consumistes a vinha, o despojo do pobre está em vossas casas.
15 Mnamaanisha nini kuwaponda watu wangu na kuzisaga nyuso za maskini?” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Por que vós esmagastes ao meu povo, e moestes o rosto dos pobres?, diz o Senhor DEUS dos exércitos.
16 Bwana asema, “Wanawake wa Sayuni wana kiburi, wanatembea na shingo ndefu, wakikonyeza kwa macho yao, wanatembea kwa hatua za madaha, wakiwa na mapambo ya njuga kwenye vifundo vya miguu yao.
Além disso o SENHOR diz: Dado que as filhas de Sião se exaltam, e andam com o pescoço levantado, e [procuram] seduzir com os olhos, e vão andando a passos curtos, fazendo ruídos com os ornamentos dos pés,
17 Kwa hiyo Bwana ataleta majipu kwenye vichwa vya wanawake wa Sayuni; Bwana atazifanya ngozi za vichwa vyao kuwa vipara.”
Por isso o Senhor fará chagas no topo das cabeças das filhas de Sião, e descobrirá suas partes íntimas.
18 Katika siku ile Bwana atawanyangʼanya uzuri wao: bangili, tepe za kichwani, mikufu yenye alama za mwezi mwandamo,
Naquele dia o Senhor tirará [delas] os enfeites: tornozeleiras, testeiras, gargantilhas,
19 vipuli, vikuku, shela,
Brincos, pulseiras, véus,
20 vilemba, mikufu ya vifundo vya miguu, mshipi, chupa za manukato na hirizi,
Chapéus, braceletes, cintos, bolsinhas de perfume, amuletos,
21 pete zenye muhuri, pete za puani,
Anéis, pingentes de nariz,
22 majoho mazuri, mitandio, mavazi, kifuko cha kutilia fedha,
Vestidos de festa, mantas, capas, bolsas,
23 vioo, mavazi ya kitani, taji na shali.
Transparências, saias de linho, toucas e túnicas.
24 Badala ya harufu ya manukato kutakuwa na uvundo; badala ya mishipi, ni kamba; badala ya nywele zilizotengenezwa vizuri, ni upara; badala ya mavazi mazuri, ni nguo za magunia; badala ya uzuri, ni alama ya aibu kwa chuma cha moto.
E será que, no lugar de aromas haverá fedor; e no lugar de cinto [haverá] corda; e no lugar de cabelos cacheados [haverá] calvície, e no lugar de roupa luxuosa [haverá] roupa de saco; e queimadura no lugar de beleza.
25 Wanaume wako watauawa kwa upanga, nao mashujaa wako watauawa vitani.
Teus homens cairão à espada; teus guerreiros na batalha.
26 Malango ya Sayuni yataomboleza na kulia, ataketi mavumbini akiwa fukara.
E as portas delas gemerão, e chorarão; e ela, ficando desolada, se sentará no chão.

< Isaya 3 >