< Isaya 3 >

1 Tazama sasa, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yu karibu kuwaondolea Yerusalemu na Yuda upatikanaji wa mahitaji na misaada, upatikanaji wote wa chakula na tegemeo lote la maji,
Oto bowiem Pan, PAN zastępów, odbierze Jerozolimie i Judzie podporę i laskę, wszelką podporę w chlebie i wszelką podporę w wodzie.
2 shujaa na mtu wa vita, mwamuzi na nabii, mwaguzi na mzee,
Mocarza i męża walecznego, sędziego i proroka, mędrca i starca;
3 jemadari wa kikosi cha watu hamsini na mtu mwenye cheo, mshauri, fundi stadi na mlozi mjanja.
Dowódcę pięćdziesiątki i dostojnika, doradcę, wybitnego rzemieślnika i krasomówcę.
4 Nitawafanya wavulana wawe maafisa wao, watoto ndio watakaowatawala.
Książętami ustanowię chłopców, dzieci będą panować nad nimi.
5 Watu wataoneana wao kwa wao: mtu dhidi ya mtu, na jirani dhidi ya jirani yake. Kijana atainuka dhidi ya mzee, mtu mnyonge dhidi ya mtu mwenye heshima.
Ludzie będą gnębić jeden drugiego, każdy swego bliźniego. Dziecko powstanie przeciwko starcowi, a podły przeciwko dostojnikowi.
6 Mtu atamkamata mmoja wa ndugu zake katika nyumba ya baba yake na kusema, “Unalo joho, sasa uwe kiongozi wetu, tawala lundo hili la magofu!”
Gdy człowiek uchwyci się swego brata z domu swego ojca i [powie]: Masz ubranie, bądź naszym wodzem, niech te ruiny będą pod twoją ręką;
7 Lakini siku hiyo atapiga kelele akisema, “Sina uponyaji. Sina chakula wala mavazi katika nyumba yangu, msinifanye niwe kiongozi wa watu.”
Ten przysięgnie w tym dniu, mówiąc: Nie będę opatrywał [tych ran]; w moim domu bowiem nie ma chleba ani ubrania; nie czyńcie mnie wodzem ludu.
8 Yerusalemu inapepesuka, Yuda inaanguka; maneno yao na matendo yao ni kinyume na Bwana, wakiudharau uwepo wake uliotukuka.
Bo Jerozolima upada, a Juda się wali, gdyż ich język i czyny są przeciwko PANU, aby pobudzić do gniewu oczy jego majestatu.
9 Nyuso zao zinavyoonekana zinashuhudia dhidi yao, hujivunia dhambi yao kama Sodoma, wala hawaifichi. Ole wao! Wamejiletea maafa juu yao wenyewe.
Wyraz ich twarzy świadczy przeciwko nim; jak Sodoma ogłaszają swój grzech, nie kryją [go]. Biada ich duszy! Gdyż sami na siebie sprowadzają zło.
10 Waambie wanyofu itakuwa heri kwao, kwa kuwa watafurahia tunda la matendo yao.
Powiedzcie sprawiedliwemu, że będzie mu dobrze, bo będzie spożywać owoc swoich rąk.
11 Ole kwa watu waovu! Maafa yapo juu yao! Watalipwa kwa ajili ya yale mikono yao iliyotenda.
Biada niegodziwemu! Będzie mu źle, odpłacą [mu] bowiem według [czynów] jego rąk.
12 Vijana wanawatesa watu wangu, wanawake wanawatawala. Enyi watu wangu, viongozi wenu wanawapotosha, wanawapoteza njia.
Ciemięzcami mego ludu są dzieci i kobiety nim rządzą. O ludu mój! Twoi wodzowie cię zwodzą i niszczą drogę twoich ścieżek.
13 Bwana anachukua nafasi yake mahakamani, anasimama kuhukumu watu.
PAN powstał, aby się rozprawić, stoi, aby sądzić lud.
14 Bwana anaingia katika hukumu dhidi ya wazee na viongozi wa watu wake: “Ninyi ndio mlioharibu shamba langu la mizabibu, mali zilizonyangʼanywa maskini zimo nyumbani mwenu.
PAN stawi na sąd starszych swego ludu i ich książąt: Wy spustoszyliście [moją] winnicę, w waszych domach znajduje się łup ubogich.
15 Mnamaanisha nini kuwaponda watu wangu na kuzisaga nyuso za maskini?” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Po co miażdżycie mój lud i uciskacie oblicza ubogich? – mówi Pan BÓG zastępów.
16 Bwana asema, “Wanawake wa Sayuni wana kiburi, wanatembea na shingo ndefu, wakikonyeza kwa macho yao, wanatembea kwa hatua za madaha, wakiwa na mapambo ya njuga kwenye vifundo vya miguu yao.
PAN powiedział: Ponieważ wynoszą się córki Syjonu i chodzą z wyciągniętą szyją, uwodzą oczami, a chodząc, drepczą i pobrzękują swoimi nogami;
17 Kwa hiyo Bwana ataleta majipu kwenye vichwa vya wanawake wa Sayuni; Bwana atazifanya ngozi za vichwa vyao kuwa vipara.”
Dlatego Pan ogoli wierzch głowy córek Syjonu i PAN obnaży ich nagość.
18 Katika siku ile Bwana atawanyangʼanya uzuri wao: bangili, tepe za kichwani, mikufu yenye alama za mwezi mwandamo,
W tym dniu Pan odejmie ozdobne brzękadła [od ich stóp], ich czepce i księżyce;
19 vipuli, vikuku, shela,
Łańcuszki, bransolety i welony;
20 vilemba, mikufu ya vifundo vya miguu, mshipi, chupa za manukato na hirizi,
Czapeczki, ozdoby u nóg, opaski, naszyjniki i kolczyki;
21 pete zenye muhuri, pete za puani,
Pierścionki i wisiorki na czołach;
22 majoho mazuri, mitandio, mavazi, kifuko cha kutilia fedha,
Odświętne szaty, płaszcze, szale i torebki;
23 vioo, mavazi ya kitani, taji na shali.
Zwierciadełka, bisior, turbany i narzutki.
24 Badala ya harufu ya manukato kutakuwa na uvundo; badala ya mishipi, ni kamba; badala ya nywele zilizotengenezwa vizuri, ni upara; badala ya mavazi mazuri, ni nguo za magunia; badala ya uzuri, ni alama ya aibu kwa chuma cha moto.
I wtedy zamiast wonności będzie smród, zamiast pasa będzie rozdarcie, zamiast upiętych włosów będzie łysina, zamiast szerokiej szaty będzie przepasanie worem i zamiast piękna będzie oparzenie.
25 Wanaume wako watauawa kwa upanga, nao mashujaa wako watauawa vitani.
Twoi mężczyźni polegną od miecza i twoi mocarze – na wojnie.
26 Malango ya Sayuni yataomboleza na kulia, ataketi mavumbini akiwa fukara.
Jej bramy zasmucą się i zapłaczą, a [ona], spustoszona, usiądzie na ziemi.

< Isaya 3 >