< Isaya 3 >

1 Tazama sasa, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yu karibu kuwaondolea Yerusalemu na Yuda upatikanaji wa mahitaji na misaada, upatikanaji wote wa chakula na tegemeo lote la maji,
Voilà que le Dominateur, Dieu des armées, va enlever de la Judée et de Jérusalem le puissant et la puissante, la force du pain et la force de l'eau;
2 shujaa na mtu wa vita, mwamuzi na nabii, mwaguzi na mzee,
Le grand, le fort et l'homme de guerre, le juge, le sage et l'ancien;
3 jemadari wa kikosi cha watu hamsini na mtu mwenye cheo, mshauri, fundi stadi na mlozi mjanja.
Le chef de cinquante hommes et le conseiller vénérable, l'habile architecte et l'auditeur intelligent.
4 Nitawafanya wavulana wawe maafisa wao, watoto ndio watakaowatawala.
Et je ferai des jeunes gens leurs princes, et des railleurs les gouverneront.
5 Watu wataoneana wao kwa wao: mtu dhidi ya mtu, na jirani dhidi ya jirani yake. Kijana atainuka dhidi ya mzee, mtu mnyonge dhidi ya mtu mwenye heshima.
Et le peuple en viendra aux mains, homme contre homme, ami contre ami; l'enfant frappera sur le vieillard, l'infâme sur l'honnête homme.
6 Mtu atamkamata mmoja wa ndugu zake katika nyumba ya baba yake na kusema, “Unalo joho, sasa uwe kiongozi wetu, tawala lundo hili la magofu!”
L'homme prendra son frère ou son proche parent dans la famille de son père, et il lui dira: Tu as un manteau, sois notre prince, et que ma nourriture soit dans ta main.
7 Lakini siku hiyo atapiga kelele akisema, “Sina uponyaji. Sina chakula wala mavazi katika nyumba yangu, msinifanye niwe kiongozi wa watu.”
Et ce jour-là l'antre répondra: Je ne serai pas ton prince, car il n'y a en ma maison ni pain ni manteau; je ne serai pas le prince de ce peuple.
8 Yerusalemu inapepesuka, Yuda inaanguka; maneno yao na matendo yao ni kinyume na Bwana, wakiudharau uwepo wake uliotukuka.
Car Jérusalem est ruinée et Juda est tombé; et leurs langues sont avec l'iniquité, et ils n'obéissent point au Seigneur. C'est pourquoi leur gloire est maintenant abaissée,
9 Nyuso zao zinavyoonekana zinashuhudia dhidi yao, hujivunia dhambi yao kama Sodoma, wala hawaifichi. Ole wao! Wamejiletea maafa juu yao wenyewe.
Et la confusion de leur visage porte témoignage contre eux; et, comme Sodome, ils ont montré et proclamé leur péché. Malheur à leurs âmes! car ils ont pris une funeste résolution contre eux-mêmes,
10 Waambie wanyofu itakuwa heri kwao, kwa kuwa watafurahia tunda la matendo yao.
Disant: Enchaînons le juste, parce qu'il nous est insupportable. Aussi goûteront-ils les fruits de leurs œuvres.
11 Ole kwa watu waovu! Maafa yapo juu yao! Watalipwa kwa ajili ya yale mikono yao iliyotenda.
Malheur à l'impie! il lui arrivera mal à cause des œuvres de ses mains.
12 Vijana wanawatesa watu wangu, wanawake wanawatawala. Enyi watu wangu, viongozi wenu wanawapotosha, wanawapoteza njia.
Mon peuple, tes exacteurs rapinent, et des usuriers te maîtrisent; mon peuple, ceux qui te déclarent heureux t'égarent, et ils bouleversent le sentier où tu marches.
13 Bwana anachukua nafasi yake mahakamani, anasimama kuhukumu watu.
Mais maintenant le Seigneur va siéger pour juger, et il entrera en jugement avec son peuple.
14 Bwana anaingia katika hukumu dhidi ya wazee na viongozi wa watu wake: “Ninyi ndio mlioharibu shamba langu la mizabibu, mali zilizonyangʼanywa maskini zimo nyumbani mwenu.
Le Seigneur en personne entrera en jugement avec les anciens et les princes du peuple. Ô vous donc, pourquoi avez-vous mis le feu à ma vigne? pourquoi la dépouille du pauvre est-elle en vos maisons?
15 Mnamaanisha nini kuwaponda watu wangu na kuzisaga nyuso za maskini?” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Pourquoi faites-vous tort à mon peuple? pourquoi couvrez-vous de confusion la face des pauvres?
16 Bwana asema, “Wanawake wa Sayuni wana kiburi, wanatembea na shingo ndefu, wakikonyeza kwa macho yao, wanatembea kwa hatua za madaha, wakiwa na mapambo ya njuga kwenye vifundo vya miguu yao.
Or voici ce que dit le Seigneur: Parce que les filles de Sion sont altières, et qu'elles ont marché la tête haute, en faisant signe des yeux, et qu'elles ont traîné leurs tuniques du mouvement de leurs pieds, et qu'elles ont eu une démarche étudiée,
17 Kwa hiyo Bwana ataleta majipu kwenye vichwa vya wanawake wa Sayuni; Bwana atazifanya ngozi za vichwa vyao kuwa vipara.”
Dieu humiliera dans Sion les filles du premier rang, et le Seigneur les dépouillera de leurs ornements.
18 Katika siku ile Bwana atawanyangʼanya uzuri wao: bangili, tepe za kichwani, mikufu yenye alama za mwezi mwandamo,
Et ce jour-là le Seigneur détruira la gloire de leur parure, leurs réseaux, leurs tresses et leurs épingles d'or,
19 vipuli, vikuku, shela,
Et leurs colliers et le fard de leur visage,
20 vilemba, mikufu ya vifundo vya miguu, mshipi, chupa za manukato na hirizi,
Et l'ensemble de leurs joyaux de gloire, bracelets, anneaux, chaînettes, bagues et pendants d'oreilles,
21 pete zenye muhuri, pete za puani,
Et leurs franges de pourpre et leurs robes de pourpre,
22 majoho mazuri, mitandio, mavazi, kifuko cha kutilia fedha,
Et leurs habits de l'intérieur de la maison, et leurs habits transparents de Laconie,
23 vioo, mavazi ya kitani, taji na shali.
Et leurs robes de fin lin, d'hyacinthe et d'écarlate, et leurs tissus de fin lin, d'or et d'hyacinthe, et leurs longs voiles d'été.
24 Badala ya harufu ya manukato kutakuwa na uvundo; badala ya mishipi, ni kamba; badala ya nywele zilizotengenezwa vizuri, ni upara; badala ya mavazi mazuri, ni nguo za magunia; badala ya uzuri, ni alama ya aibu kwa chuma cha moto.
Et au lieu de suaves parfums tu te couvriras de cendre; et au lieu de tes rubans tu te ceindras d'une corde; et au lieu d'une tête ornée de bijoux d'or tu auras un crâne chauve, en punition de tes œuvres; et au lieu d'une tunique de pourpre tu te revêtiras d'un cilice.
25 Wanaume wako watauawa kwa upanga, nao mashujaa wako watauawa vitani.
Et le fils si beau que tu chéris tombera sous le glaive, et tes forts périront par l'épée.
26 Malango ya Sayuni yataomboleza na kulia, ataketi mavumbini akiwa fukara.
Et ils seront humiliés, et les trésors où tu gardais tes bijoux pleureront; et tu resteras seule, et tu seras brisée contre terre.

< Isaya 3 >