< Isaya 3 >
1 Tazama sasa, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yu karibu kuwaondolea Yerusalemu na Yuda upatikanaji wa mahitaji na misaada, upatikanaji wote wa chakula na tegemeo lote la maji,
Car voici que le Seigneur, Yahweh des armées, va retirer de Jérusalem et de Juda toute ressource et tout appui, toute ressource de pain et toute ressource d’eau,
2 shujaa na mtu wa vita, mwamuzi na nabii, mwaguzi na mzee,
héros et homme de guerre, juge, prophète et devin, ancien,
3 jemadari wa kikosi cha watu hamsini na mtu mwenye cheo, mshauri, fundi stadi na mlozi mjanja.
capitaine et notable, conseiller, ouvrier expert en son art et habile enchanteur.
4 Nitawafanya wavulana wawe maafisa wao, watoto ndio watakaowatawala.
Et je leur donnerai des jeunes gens pour princes, et des enfants domineront sur eux.
5 Watu wataoneana wao kwa wao: mtu dhidi ya mtu, na jirani dhidi ya jirani yake. Kijana atainuka dhidi ya mzee, mtu mnyonge dhidi ya mtu mwenye heshima.
Et le peuple se ruera homme contre homme, chacun contre son voisin; ils se précipiteront, le jeune homme contre le vieillard, et l’homme de rien contre le plus illustre.
6 Mtu atamkamata mmoja wa ndugu zake katika nyumba ya baba yake na kusema, “Unalo joho, sasa uwe kiongozi wetu, tawala lundo hili la magofu!”
Lorsqu’un homme prendra son frère dans la maison de son père, en disant: « Tu as un manteau, sois notre chef, et que cette ruine soit sous ta garde! »
7 Lakini siku hiyo atapiga kelele akisema, “Sina uponyaji. Sina chakula wala mavazi katika nyumba yangu, msinifanye niwe kiongozi wa watu.”
Il se récriera en ce jour-là: « Je ne veux pas être le médecin: je n’ai dans ma maison ni pain ni manteau; ne me faites pas chef du peuple. »
8 Yerusalemu inapepesuka, Yuda inaanguka; maneno yao na matendo yao ni kinyume na Bwana, wakiudharau uwepo wake uliotukuka.
Car Jérusalem chancelle et Juda s’écroule, parce que leurs paroles et leurs œuvres sont contre Yahweh, pour braver le regard de sa majesté.
9 Nyuso zao zinavyoonekana zinashuhudia dhidi yao, hujivunia dhambi yao kama Sodoma, wala hawaifichi. Ole wao! Wamejiletea maafa juu yao wenyewe.
L’air de leur visage dépose contre eux; comme Sodome, ils publient leur péché et ne s’en cachent point. Malheur à eux! car ils sont eux-mêmes les auteurs de leur perte.
10 Waambie wanyofu itakuwa heri kwao, kwa kuwa watafurahia tunda la matendo yao.
Dites au juste qu’il est heureux, car il mangera le fruit de ses œuvres.
11 Ole kwa watu waovu! Maafa yapo juu yao! Watalipwa kwa ajili ya yale mikono yao iliyotenda.
Malheur au méchant! mal lui arrivera, car ce que ses mains ont fait lui sera rendu.
12 Vijana wanawatesa watu wangu, wanawake wanawatawala. Enyi watu wangu, viongozi wenu wanawapotosha, wanawapoteza njia.
Mon peuple est opprimé par des enfants, et des femmes le gouvernent. Mon peuple, ceux qui te dirigent t’égarent, et ils ruinent le chemin où tu dois passer.
13 Bwana anachukua nafasi yake mahakamani, anasimama kuhukumu watu.
Yahweh s’est levé pour rendre la justice, et il est debout pour juger les peuples.
14 Bwana anaingia katika hukumu dhidi ya wazee na viongozi wa watu wake: “Ninyi ndio mlioharibu shamba langu la mizabibu, mali zilizonyangʼanywa maskini zimo nyumbani mwenu.
Yahweh entre en jugement avec les anciens et les princes de son peuple: « Vous avez brouté la vigne; la dépouille du pauvre est dans vos maisons.
15 Mnamaanisha nini kuwaponda watu wangu na kuzisaga nyuso za maskini?” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote.
De quel droit foulez-vous mon peuple, et écrasez-vous la face des malheureux? » — oracle du Seigneur Yahweh des armées.
16 Bwana asema, “Wanawake wa Sayuni wana kiburi, wanatembea na shingo ndefu, wakikonyeza kwa macho yao, wanatembea kwa hatua za madaha, wakiwa na mapambo ya njuga kwenye vifundo vya miguu yao.
Yahweh a dit: Parce que les filles de Sion sont devenues orgueilleuses, qu’elles s’avancent la tête haute, lançant des regards, qu’elles vont à petits pas, et font sonner les anneaux de leurs pieds,
17 Kwa hiyo Bwana ataleta majipu kwenye vichwa vya wanawake wa Sayuni; Bwana atazifanya ngozi za vichwa vyao kuwa vipara.”
le Seigneur rendra chauve le crâne des filles de Sion, et Yahweh découvrira leur nudité.
18 Katika siku ile Bwana atawanyangʼanya uzuri wao: bangili, tepe za kichwani, mikufu yenye alama za mwezi mwandamo,
En ce jour-là, le Seigneur enlèvera le luxe des anneaux, les soleils et les croissants;
19 vipuli, vikuku, shela,
les pendants d’oreille, les bracelets et les voiles;
20 vilemba, mikufu ya vifundo vya miguu, mshipi, chupa za manukato na hirizi,
les diadèmes, les chaînettes des pieds et les ceintures;
21 pete zenye muhuri, pete za puani,
les boîtes à parfum et les amulettes, les bagues et les anneaux du nez;
22 majoho mazuri, mitandio, mavazi, kifuko cha kutilia fedha,
les robes de fête et les larges tuniques, les manteaux et les bourses;
23 vioo, mavazi ya kitani, taji na shali.
les miroirs et les mousselines, les turbans et les mantilles.
24 Badala ya harufu ya manukato kutakuwa na uvundo; badala ya mishipi, ni kamba; badala ya nywele zilizotengenezwa vizuri, ni upara; badala ya mavazi mazuri, ni nguo za magunia; badala ya uzuri, ni alama ya aibu kwa chuma cha moto.
Et, au lieu de parfum, il y aura la pourriture; au lieu de ceinture, une corde; au lieu de cheveux bouclés, une tête chauve; au lieu d’une ample robe, un sac; au lieu de beauté, la marque imprimée par le feu.
25 Wanaume wako watauawa kwa upanga, nao mashujaa wako watauawa vitani.
Tes guerriers tomberont par l’épée, et tes héros dans la bataille.
26 Malango ya Sayuni yataomboleza na kulia, ataketi mavumbini akiwa fukara.
Les portes de Sion gémiront et seront dans le deuil, et, désolée, elle sera assise dans la poussière.