< Isaya 29 >

1 Ole wako, wewe Arieli, Arieli, mji alimokaa Daudi! Ongezeni mwaka kwa mwaka, na mzunguko wa sikukuu zenu uendelee.
Alas for the city of Ariel, which David besieged. Gather you fruits year by year; eat you, for you shall eat with Moab.
2 Hata hivyo nitauzunguka Arieli kwa jeshi, utalia na kuomboleza, utakuwa kwangu kama mahali pa kuwashia moto madhabahuni.
For I will grievously afflict Ariel: and her strength and her wealth shall be mine.
3 Nitapiga kambi pande zote dhidi yako, nitakuzunguka kwa minara na kupanga mazingirwa yangu dhidi yako.
And I will compass you about like David, and will raise a mound about you, and set up towers round you.
4 Utakaposhushwa, utanena kutoka ardhini, utamumunya maneno yako kutoka mavumbini. Sauti yako itatoka katika nchi kama vile ya mzimu, utanongʼona maneno yako toka mavumbini.
And your words shall be brought down to the earth, and your words shall sink down to the earth, and your voice shall be as they that speak out of the earth, and your voice shall be lowered to the ground.
5 Lakini adui zako wengi watakuwa kama vumbi laini, kundi la wakatili watakuwa kama makapi yapeperushwayo. Naam, ghafula, mara moja,
But the wealth of the ungodly shall be as dust from a wheel, and the multitude of them that oppress you as flying chaff, and it shall be suddenly as a moment,
6 Bwana Mwenye Nguvu Zote atakuja na ngurumo, tetemeko la ardhi, na kwa sauti kuu, atakuja na dhoruba, tufani na miali ya moto iteketezayo.
from the Lord of Hosts: for there shall be a visitation with thunder, and earthquake, and a loud noise, a rushing tempest, and devouring flame of fire.
7 Kisha makundi ya mataifa yote yale yapiganayo dhidi ya Arieli, yale yanayomshambulia yeye na ngome zake, na kumzunguka kwa jeshi, watakuwa kama ilivyo ndoto, kama maono wakati wa usiku:
And the wealth of all the nations together, as many as have fought against Ariel, and all they that war against Jerusalem, and all who are gathered against her, and they that distress her, shall be as one that dreams in sleep by night.
8 kama vile mtu aliye na njaa aotavyo kuwa anakula, lakini huamka, bado njaa yake ingalipo, kama vile mtu mwenye kiu aotavyo kuwa anakunywa maji, lakini huamka akiwa anazimia, akiwa bado angali ana kiu. Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa makundi yote ya mataifa yanayopigana dhidi ya Mlima Sayuni.
And as men drink and eat in sleep, and when they have arisen, the dream is vain: and as a thirsty man dreams as if he drank, and having arisen is still thirsty, and his soul has desired in vain: so shall be the wealth of all the nations, as many as have fought against the mount Sion.
9 Duwaeni na kushangaa, jifanyeni vipofu wenyewe na msione, leweni, lakini si kwa mvinyo, pepesukeni lakini si kwa kileo.
Faint you, and be amazed, and be overpowered, not with strong drink nor with wine.
10 Bwana amewaleteeni usingizi mzito: Ameziba macho yenu (ninyi manabii); amefunika vichwa vyenu (ninyi waonaji).
For the Lord has made you to drink a spirit of deep sleep; and he shall close their eyes, and [the eyes] of their prophets and of their rulers, who see secret things.
11 Kwa maana kwenu ninyi, maono haya yote si kitu ila maneno yaliyotiwa lakiri katika kitabu. Kama mkimpa mtu yeyote awezaye kusoma kitabu hiki, nanyi mkamwambia, “Tafadhali kisome,” yeye atajibu, “Mimi siwezi, kwa kuwa kimetiwa lakiri.”
And all these things shall be to you as the words of this sealed book, which if they shall give to a learned man, saying, Read this, he shall then say, I can’t read [it], for it is sealed.
12 Au kama mkimpa mtu yeyote kitabu hiki asiyeweza kusoma na kumwambia, “Tafadhali kisome,” atajibu, “Mimi sijui kusoma.”
And this book shall be given into the hands of a man that is unlearned, and [one] shall say to him, Read this; and he shall say, I am not learned.
13 Bwana anasema: “Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyao na kuniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami. Ibada yao kwangu inatokana na maagizo waliyofundishwa na wanadamu.
And the Lord has said, This people draw near to me with their mouth, and they honor me with their lips, but their heart is far from me: but in vain do they worship me, teaching the commandments and doctrines of men.
14 Kwa hiyo mara nyingine tena nitawashangaza watu hawa, kwa ajabu juu ya ajabu. Hekima ya wenye hekima itapotea, nayo akili ya wenye akili itatoweka.”
Therefore behold I will proceed to remove this people, and I will remove them: and I will destroy the wisdom of the wise, and will hide the understanding of the prudent.
15 Ole kwa wale wanaokwenda kwenye vilindi virefu kumficha Bwana mipango yao, wafanyao kazi zao gizani na kufikiri, “Ni nani anayetuona? Ni nani atakayejua?”
Woe to them that deepen their counsel, and not by the Lord. Woe to them that take secret counsel, and whose works are in darkness, and they say, Who has seen us? and who shall know us, or what we do?
16 Mnapindua mambo juu chini, kana kwamba mfinyanzi aweza kufikiriwa kuwa kama udongo wa mfinyanzi! Je, kile kilichofinyangwa chaweza kumwambia yule aliyekifinyanga, “Wewe hukunifinyanga mimi?” Je, chungu kinaweza kumwambia mfinyanzi, “Wewe hujui chochote?”
Shall you not be counted as clay of the potter? Shall the thing formed say to him that formed it, You did not form me? or the work to the maker, You have not made me wisely?
17 Kwa muda mfupi sana, je, Lebanoni haitageuzwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba liwe kama msitu?
[Is it] not yet a little while, and Libanus shall be changed as the mountains of Chermel, and Chermel shall be reckoned as a forest?
18 Katika siku ile viziwi watasikia maneno ya kitabu, na katika utusitusi na giza macho ya kipofu yataona.
And in that day the deaf shall hear the words of the book, and they that are in darkness, and they that are in mist: the eyes of the blind shall see,
19 Mara nyingine tena wanyenyekevu watafurahi katika Bwana, wahitaji watafurahi katika yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
and the poor shall rejoice with joy because of the Lord, and they that had no hope among men shall be filled with joy.
20 Wakatili watatoweka na wenye kudhihaki watatokomea, nao wote wenye jicho la uovu watakatiliwa mbali,
The lawless man has come to nothing, and the proud man has perished, and they that transgress mischievously have been utterly destroyed:
21 wale ambao kwa neno humfanya mtu kuwa mwenye hatia, wamtegeao mtego mtetezi katika mahakama, na kwa ushuhuda wa uongo humnyima haki yeye asiye na hatia.
and they that cause men to sin by a word: and men shall make all that reprove in the gates an offense, because they have unjustly turned aside the righteous.
22 Kwa hiyo hili ndilo Bwana, aliyemkomboa Abrahamu, analosema kwa nyumba ya Yakobo: “Yakobo hataaibishwa tena, wala nyuso zao hazitabadilika sura tena.
Therefore thus says the Lord concerning the house of Jacob, whom he set apart from Abraam, Jacob shall not now be ashamed, neither shall he now change countenance.
23 Wakati watakapoona watoto wao miongoni mwao, kazi ya mikono yangu, watalitakasa Jina langu takatifu; wataukubali utakatifu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Yakobo, nao watamcha Mungu wa Israeli.
But when their children shall have seen my works, they shall sanctify my name for my sake, and they sanctify the Holy One of Jacob, and shall fear the God of Israel.
24 Wale wanaopotoka rohoni watapata ufahamu, nao wale wanaolalamika watayakubali mafundisho.”
And they that erred in spirit shall know understanding, and the murmurers shall learn obedience, and the stammering tongues shall learn to speak peace.

< Isaya 29 >