< Isaya 29 >

1 Ole wako, wewe Arieli, Arieli, mji alimokaa Daudi! Ongezeni mwaka kwa mwaka, na mzunguko wa sikukuu zenu uendelee.
Woe to Ariel, to Ariel the city which David took: year is added to year: the solemnities are at an end.
2 Hata hivyo nitauzunguka Arieli kwa jeshi, utalia na kuomboleza, utakuwa kwangu kama mahali pa kuwashia moto madhabahuni.
And I will make a trench about Ariel, and it shall be in sorrow and mourning, and it shall be to me as Ariel.
3 Nitapiga kambi pande zote dhidi yako, nitakuzunguka kwa minara na kupanga mazingirwa yangu dhidi yako.
And I will make a circle round about thee, and will cast up a rampart against thee, and raise up bulwarks to besiege thee.
4 Utakaposhushwa, utanena kutoka ardhini, utamumunya maneno yako kutoka mavumbini. Sauti yako itatoka katika nchi kama vile ya mzimu, utanongʼona maneno yako toka mavumbini.
Thou shalt be brought down, thou shalt speak out of the earth, and thy speech shall be heard out of the ground: and thy voice shall be from the earth like that of the python, and out of the ground thy speech shall mutter.
5 Lakini adui zako wengi watakuwa kama vumbi laini, kundi la wakatili watakuwa kama makapi yapeperushwayo. Naam, ghafula, mara moja,
And the multitude of them that fan thee, shall be like small dust: and as ashes passing away, the multitude of them that have prevailed against thee.
6 Bwana Mwenye Nguvu Zote atakuja na ngurumo, tetemeko la ardhi, na kwa sauti kuu, atakuja na dhoruba, tufani na miali ya moto iteketezayo.
And it shall be at an instant suddenly. A visitation shall come from the Lord of hosts in thunder, and with earthquake, and with a great noise of whirlwind and tempest, and with the flame of devouring fire.
7 Kisha makundi ya mataifa yote yale yapiganayo dhidi ya Arieli, yale yanayomshambulia yeye na ngome zake, na kumzunguka kwa jeshi, watakuwa kama ilivyo ndoto, kama maono wakati wa usiku:
And the multitude of all nations that have fought against Ariel, shall be as the dream of a vision by night, and all that have fought, and besieged and prevailed against it.
8 kama vile mtu aliye na njaa aotavyo kuwa anakula, lakini huamka, bado njaa yake ingalipo, kama vile mtu mwenye kiu aotavyo kuwa anakunywa maji, lakini huamka akiwa anazimia, akiwa bado angali ana kiu. Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa makundi yote ya mataifa yanayopigana dhidi ya Mlima Sayuni.
And as he that is hungry dreameth, and eateth, but when he is awake, his soul is empty: and as he that is thirsty dreameth, and drinketh, and after he is awake, is yet faint with thirst, and his soul is empty: so shall be the multitude of all the Gentiles, that have fought against mount Sion.
9 Duwaeni na kushangaa, jifanyeni vipofu wenyewe na msione, leweni, lakini si kwa mvinyo, pepesukeni lakini si kwa kileo.
Be astonished, and wander, waver, and stagger: be drunk, and not with wine: stagger, and not with drunkenness.
10 Bwana amewaleteeni usingizi mzito: Ameziba macho yenu (ninyi manabii); amefunika vichwa vyenu (ninyi waonaji).
For the Lord hath mingled for you the spirit of a deep sleep, he will shut up your eyes, he will cover your prophets and princes, that see visions.
11 Kwa maana kwenu ninyi, maono haya yote si kitu ila maneno yaliyotiwa lakiri katika kitabu. Kama mkimpa mtu yeyote awezaye kusoma kitabu hiki, nanyi mkamwambia, “Tafadhali kisome,” yeye atajibu, “Mimi siwezi, kwa kuwa kimetiwa lakiri.”
And the vision of all shall be unto you as the words of a book that is sealed, which when they shall deliver to one that is learned, they shall say: Read this: and he shall answer: I cannot, for it is sealed.
12 Au kama mkimpa mtu yeyote kitabu hiki asiyeweza kusoma na kumwambia, “Tafadhali kisome,” atajibu, “Mimi sijui kusoma.”
And the book shall be given to one that knoweth no letters, and it shall be said to him: Read: and he shall answer: I know no letters.
13 Bwana anasema: “Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyao na kuniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami. Ibada yao kwangu inatokana na maagizo waliyofundishwa na wanadamu.
And the Lord said: Forasmuch as this people draw near me with their mouth, and with their lips glorify me, but their heart is far from me, and they have feared me with the commandment and doctrines of men:
14 Kwa hiyo mara nyingine tena nitawashangaza watu hawa, kwa ajabu juu ya ajabu. Hekima ya wenye hekima itapotea, nayo akili ya wenye akili itatoweka.”
Therefore behold I will proceed to cause an admiration in this people, by a great and wonderful miracle: for wisdom shall perish from their wise men, and the understanding of their prudent men shall be hid.
15 Ole kwa wale wanaokwenda kwenye vilindi virefu kumficha Bwana mipango yao, wafanyao kazi zao gizani na kufikiri, “Ni nani anayetuona? Ni nani atakayejua?”
Woe to you that are deep of heart, to hide your counsel from the Lord: and their works are in the dark, and they say: Who seeth us, and who knoweth us?
16 Mnapindua mambo juu chini, kana kwamba mfinyanzi aweza kufikiriwa kuwa kama udongo wa mfinyanzi! Je, kile kilichofinyangwa chaweza kumwambia yule aliyekifinyanga, “Wewe hukunifinyanga mimi?” Je, chungu kinaweza kumwambia mfinyanzi, “Wewe hujui chochote?”
This thought of yours is perverse: as if the clay should think against the potter, and the work should say to the maker thereof: Thou madest me not: or the thing framed should say to him that fashioned it: Thou understandest not.
17 Kwa muda mfupi sana, je, Lebanoni haitageuzwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba liwe kama msitu?
Is it not yet a very little while, and Libanus shall be turned into charmel, and charmel shall be esteemed as a forest?
18 Katika siku ile viziwi watasikia maneno ya kitabu, na katika utusitusi na giza macho ya kipofu yataona.
And in that day the deaf shall hear the words of the book, and out of darkness and obscurity the eyes of the blind shall see.
19 Mara nyingine tena wanyenyekevu watafurahi katika Bwana, wahitaji watafurahi katika yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
And the meek shall increase their joy in the Lord, and the poor men shall rejoice in the Holy One of Israel.
20 Wakatili watatoweka na wenye kudhihaki watatokomea, nao wote wenye jicho la uovu watakatiliwa mbali,
For he that did prevail hath failed, the scorner is consumed, and they are all cut off that watched for iniquity:
21 wale ambao kwa neno humfanya mtu kuwa mwenye hatia, wamtegeao mtego mtetezi katika mahakama, na kwa ushuhuda wa uongo humnyima haki yeye asiye na hatia.
That made men sin by word, and supplanted him that reproved them in the gate, and declined in vain from the just.
22 Kwa hiyo hili ndilo Bwana, aliyemkomboa Abrahamu, analosema kwa nyumba ya Yakobo: “Yakobo hataaibishwa tena, wala nyuso zao hazitabadilika sura tena.
Therefore thus saith the Lord to the house of Jacob, he that redeemed Abraham: Jacob shall not now be confounded, neither shall his countenance now be ashamed:
23 Wakati watakapoona watoto wao miongoni mwao, kazi ya mikono yangu, watalitakasa Jina langu takatifu; wataukubali utakatifu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Yakobo, nao watamcha Mungu wa Israeli.
But when he shall see his children, the work of my hands in the midst of him sanctifying my name, and they shall sanctify the Holy One of Jacob, and shall glorify the God of Israel:
24 Wale wanaopotoka rohoni watapata ufahamu, nao wale wanaolalamika watayakubali mafundisho.”
And they that erred in spirit, shall know understanding, and they that murmured, shall learn the law.

< Isaya 29 >