< Isaya 29 >
1 Ole wako, wewe Arieli, Arieli, mji alimokaa Daudi! Ongezeni mwaka kwa mwaka, na mzunguko wa sikukuu zenu uendelee.
Ho Ariel, Ariel, the city where David encamped! Add ye year to year. Let the feasts come round.
2 Hata hivyo nitauzunguka Arieli kwa jeshi, utalia na kuomboleza, utakuwa kwangu kama mahali pa kuwashia moto madhabahuni.
Then I will distress Ariel, and there shall be mourning and lamentation, and she shall be to me as Ariel.
3 Nitapiga kambi pande zote dhidi yako, nitakuzunguka kwa minara na kupanga mazingirwa yangu dhidi yako.
And I will encamp against thee round about, and will lay siege against thee with posted troops. And I will raise siege works against thee.
4 Utakaposhushwa, utanena kutoka ardhini, utamumunya maneno yako kutoka mavumbini. Sauti yako itatoka katika nchi kama vile ya mzimu, utanongʼona maneno yako toka mavumbini.
And thou shall be brought down, and shall speak out of the ground. And thy speech shall be low out of the dust, and thy voice shall be as of he who has a familiar spirit, out of the ground. And thy speech shall whisper out of the dust.
5 Lakini adui zako wengi watakuwa kama vumbi laini, kundi la wakatili watakuwa kama makapi yapeperushwayo. Naam, ghafula, mara moja,
But the multitude of thy foes shall be like small dust, and the multitude of the terrible ones as chaff that passes away. Yea, it shall be in an instant suddenly.
6 Bwana Mwenye Nguvu Zote atakuja na ngurumo, tetemeko la ardhi, na kwa sauti kuu, atakuja na dhoruba, tufani na miali ya moto iteketezayo.
She shall be visited by Jehovah of hosts with thunder, and with earthquake, and great noise, with whirlwind and tempest, and the flame of a devouring fire.
7 Kisha makundi ya mataifa yote yale yapiganayo dhidi ya Arieli, yale yanayomshambulia yeye na ngome zake, na kumzunguka kwa jeshi, watakuwa kama ilivyo ndoto, kama maono wakati wa usiku:
And the multitude of all the nations that fight against Ariel, even all that fight against her and her stronghold, and that distress her, shall be as a dream, a vision of the night.
8 kama vile mtu aliye na njaa aotavyo kuwa anakula, lakini huamka, bado njaa yake ingalipo, kama vile mtu mwenye kiu aotavyo kuwa anakunywa maji, lakini huamka akiwa anazimia, akiwa bado angali ana kiu. Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa makundi yote ya mataifa yanayopigana dhidi ya Mlima Sayuni.
And it shall be as when a hungry man dreams, and, behold, he eats. But he awakes, and his soul is empty. Or as when a thirsty man dreams, and, behold, he drinks. But he awakes, and, behold, he is faint, and his soul has appetite. So shall the multitude of all the nations be that fight against mount Zion.
9 Duwaeni na kushangaa, jifanyeni vipofu wenyewe na msione, leweni, lakini si kwa mvinyo, pepesukeni lakini si kwa kileo.
Tarry ye and wonder, take your pleasure and be blind. They are drunken, but not with wine. They stagger, but not with strong drink.
10 Bwana amewaleteeni usingizi mzito: Ameziba macho yenu (ninyi manabii); amefunika vichwa vyenu (ninyi waonaji).
For Jehovah has poured out upon you the spirit of deep sleep, and has closed your eyes. The prophets, and your heads, the seers, he has covered.
11 Kwa maana kwenu ninyi, maono haya yote si kitu ila maneno yaliyotiwa lakiri katika kitabu. Kama mkimpa mtu yeyote awezaye kusoma kitabu hiki, nanyi mkamwambia, “Tafadhali kisome,” yeye atajibu, “Mimi siwezi, kwa kuwa kimetiwa lakiri.”
And all vision has become to you as the words of a book that is sealed, which men deliver to a man who is learned, saying, Read this, I pray thee. And he says, I cannot, for it is sealed.
12 Au kama mkimpa mtu yeyote kitabu hiki asiyeweza kusoma na kumwambia, “Tafadhali kisome,” atajibu, “Mimi sijui kusoma.”
And the book is delivered to him who is not learned, saying, Read this, I pray thee. And he says, I am not learned.
13 Bwana anasema: “Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyao na kuniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami. Ibada yao kwangu inatokana na maagizo waliyofundishwa na wanadamu.
And the Lord said, Inasmuch as this people draw near me with their mouth, and honor me with their lips, but have removed their heart far from me, but in vain they worship me, teaching the commandments and doctrines of men.
14 Kwa hiyo mara nyingine tena nitawashangaza watu hawa, kwa ajabu juu ya ajabu. Hekima ya wenye hekima itapotea, nayo akili ya wenye akili itatoweka.”
Therefore, behold, I will proceed to do a marvelous work among this people, even a marvelous work and a wonder. I will destroy the wisdom of the wise, and the understanding of their prudent men shall be hidden.
15 Ole kwa wale wanaokwenda kwenye vilindi virefu kumficha Bwana mipango yao, wafanyao kazi zao gizani na kufikiri, “Ni nani anayetuona? Ni nani atakayejua?”
Woe to those who hide deep their counsel from Jehovah, and whose works are in the dark, and who say, Who sees us? and, Who knows us?
16 Mnapindua mambo juu chini, kana kwamba mfinyanzi aweza kufikiriwa kuwa kama udongo wa mfinyanzi! Je, kile kilichofinyangwa chaweza kumwambia yule aliyekifinyanga, “Wewe hukunifinyanga mimi?” Je, chungu kinaweza kumwambia mfinyanzi, “Wewe hujui chochote?”
Ye turn things upside down! Shall the potter be esteemed as clay, that the thing made should say of him who made it, He did not make me, or the thing formed say of him who formed it, He has no understanding?
17 Kwa muda mfupi sana, je, Lebanoni haitageuzwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba liwe kama msitu?
Is it not yet a very little while, and Lebanon shall be turned into a fruitful field, and the fruitful field shall be esteemed as a forest?
18 Katika siku ile viziwi watasikia maneno ya kitabu, na katika utusitusi na giza macho ya kipofu yataona.
And in that day the deaf shall hear the words of the book, and the eyes of the blind shall see out of obscurity and out of darkness.
19 Mara nyingine tena wanyenyekevu watafurahi katika Bwana, wahitaji watafurahi katika yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
The meek also shall increase their joy in Jehovah, and the poor among men shall rejoice in the Holy One of Israel.
20 Wakatili watatoweka na wenye kudhihaki watatokomea, nao wote wenye jicho la uovu watakatiliwa mbali,
For the terrible one is brought to nothing, and the scoffer ceases. And all those who watch for iniquity are cut off,
21 wale ambao kwa neno humfanya mtu kuwa mwenye hatia, wamtegeao mtego mtetezi katika mahakama, na kwa ushuhuda wa uongo humnyima haki yeye asiye na hatia.
who make a man an offender in his cause, and lay a snare for him who reproves in the gate, and turn aside the just with a thing of nothing.
22 Kwa hiyo hili ndilo Bwana, aliyemkomboa Abrahamu, analosema kwa nyumba ya Yakobo: “Yakobo hataaibishwa tena, wala nyuso zao hazitabadilika sura tena.
Therefore thus says Jehovah, who redeemed Abraham, concerning the house of Jacob: Jacob shall not now be ashamed, nor shall his face now grow pale.
23 Wakati watakapoona watoto wao miongoni mwao, kazi ya mikono yangu, watalitakasa Jina langu takatifu; wataukubali utakatifu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Yakobo, nao watamcha Mungu wa Israeli.
But when he sees his children, the work of my hands, in the midst of him, they shall sanctify my name. Yea, they shall sanctify the Holy One of Jacob, and shall stand in awe of the God of Israel.
24 Wale wanaopotoka rohoni watapata ufahamu, nao wale wanaolalamika watayakubali mafundisho.”
They also who err in spirit shall come to understanding, and those who murmur shall receive instruction.