< Isaya 27 >

1 Katika siku ile, Bwana ataadhibu kwa upanga wake, upanga wake mkali, mkubwa na wenye nguvu, ataadhibu Lewiathani yule nyoka apitaye kwa mwendo laini, Lewiathani yule nyoka mwenye kujipinda; atamuua joka huyo mkubwa sana wa baharini.
En ce même jour, l'Éternel châtiera avec sa dure, grande et forte épée le léviathan, serpent fuyard, et le léviathan, serpent tortueux, et tuera le dragon de la mer.
2 Katika siku ile: “Imbeni kuhusu shamba la mizabibu lililozaa:
En ce même jour, chantez ainsi sur la vigne:
3 Mimi, Bwana, ninalitunza, nalinyweshea maji mfululizo. Ninalichunga usiku na mchana ili mtu yeyote asije akalidhuru.
« Moi, l'Éternel, je suis son gardien, je l'arrose en tout temps, contre les attaques nuit et jour je la garderai.
4 Mimi sijakasirika. Licha pangekuwepo michongoma na miiba kunikabili! Ningepambana dhidi yake katika vita, ningeliichoma moto yote.
Je suis sans colère! Qu'on m'oppose des ronces et des épines! en combattant je fondrai sur eux et les consumerai en entier;
5 Au niwaache waje kwangu kwa ajili ya kupata kimbilio, wao na wafanye amani nami, naam, wafanye amani nami.”
à moins qu'ils ne saisissent mon appui, et ne fassent leur paix avec moi, ne fassent leur paix avec moi. »
6 Katika siku zijazo, Yakobo atatia mizizi, Israeli atatoa chipukizi na kuchanua maua, naye atajaza ulimwengu wote kwa matunda.
A l'avenir Jacob poussera des racines, et Israël des bourgeons et des fleurs, et de leurs fruits ils rempliront le monde.
7 Je, Bwana amempiga vile alivyowapiga wale waliompiga? Je, yeye ameuawa vile walivyouawa wale waliomuua yeye?
Frappa-t-Il [Israël] des coups dont Il frappa ceux qui l'ont frappé? ou fut-il égorgé comme furent égorgés ceux qui l'ont égorgé?
8 Kwa vita na kwa kumfukuza unapingana naye: kwa mshindo wake mkali anamfukuza, kama siku ile uvumapo upepo wa mashariki.
Ce fut modérément, en le répudiant, que tu le punis, qu'il fut emporté par ton souffle violent au jour du vent d'Orient.
9 Kwa hili, basi, hatia ya Yakobo itafanyiwa upatanisho, nalo hili litakuwa matunda ya utimilizo wa kuondolewa kwa dhambi yake: Wakati atakapoyafanya mawe yote ya madhabahu kuwa kama mawe ya chokaa yaliyopondwa vipande vipande, hakuna nguzo za Ashera au madhabahu za kufukizia uvumba zitakazobaki zimesimama.
C'est aussi par là que fut expié le crime de Jacob; et c'est là justement le fruit de l'abandon qu'il fit de son péché, quand Il rendit toutes les pierres des autels pareilles à des pierres calcinées, concassées, pour qu'il ne s'élève plus d'aschères ni de colonnes solaires.
10 Mji ulio na boma umebaki ukiwa, makao yaliyotelekezwa, yaliyoachwa kama jangwa. Huko ndama hulisha, huko hujilaza, wanakwanyua matawi yake.
Car la cité [jadis] forte est dévastée; c'est un séjour abandonné et désolé comme le désert, le veau y pâture, il s'y couche et broute ses rameaux.
11 Wakati vijiti vyake vimekauka, huvunjwa nao wanawake huja na kuwasha navyo moto. Kwa kuwa hili ni taifa lisilo na ufahamu, kwa hiyo yeye aliyewafanya hana huruma juu yao, Muumba wao hawaonyeshi fadhili.
Quand ses branches sèchent, elles sont brisées, des femmes viennent et y mettent le feu. Car il ne fut pas un peuple sage; aussi son créateur n'eut pas pitié de lui, et son formateur ne lui fut pas propice.
12 Katika siku ile Bwana atapura kutoka matiririko ya Mto Frati hadi Kijito cha Misri, nanyi ee Waisraeli, mtakusanywa mmoja mmoja.
Mais en ce même jour, l'Éternel secouera des fruits depuis les flots du Fleuve jusqu'au torrent d'Egypte, et vous serez ramassés un à un, enfants d'Israël.
13 Katika siku ile tarumbeta kubwa italia. Wale waliokuwa wakiangamia katika nchi ya Ashuru, nao wale waliokuwa uhamishoni katika nchi ya Misri watakuja na kumwabudu Bwana katika mlima mtakatifu huko Yerusalemu.
Et en ce même jour la grande trompette sonnera, et ceux qui étaient perdus au pays d'Assyrie et bannis au pays d'Egypte, viendront et adoreront l'Éternel sur la montagne sainte à Jérusalem.

< Isaya 27 >