< Isaya 27 >

1 Katika siku ile, Bwana ataadhibu kwa upanga wake, upanga wake mkali, mkubwa na wenye nguvu, ataadhibu Lewiathani yule nyoka apitaye kwa mwendo laini, Lewiathani yule nyoka mwenye kujipinda; atamuua joka huyo mkubwa sana wa baharini.
En ce jour-là, Yahweh visitera de son épée dure, grande et forte, Léviathan, le serpent agile, Léviathan, le serpent tortueux, et il tuera le monstre qui est dans la mer.
2 Katika siku ile: “Imbeni kuhusu shamba la mizabibu lililozaa:
En ce jour-là on dira: " Une vigne au vin généreux, chantez-la!
3 Mimi, Bwana, ninalitunza, nalinyweshea maji mfululizo. Ninalichunga usiku na mchana ili mtu yeyote asije akalidhuru.
C'est moi, Yahweh, qui la garde; je l'arrose en tout temps; de peur qu'on y pénètre, nuit et jour je la garde; je n'ai plus de colère.
4 Mimi sijakasirika. Licha pangekuwepo michongoma na miiba kunikabili! Ningepambana dhidi yake katika vita, ningeliichoma moto yote.
Qui me donnera des ronces, et des épines à combattre? Je marcherai contre elles, je les brûlerai toutes.
5 Au niwaache waje kwangu kwa ajili ya kupata kimbilio, wao na wafanye amani nami, naam, wafanye amani nami.”
Ou bien, qu'on s'attache à ma protection, qu'on fasse la paix avec moi, qu'avec moi on fasse la paix!
6 Katika siku zijazo, Yakobo atatia mizizi, Israeli atatoa chipukizi na kuchanua maua, naye atajaza ulimwengu wote kwa matunda.
Dans les jours à venir, Jacob poussera des racines, Israël donnera des fleurs et des rejetons, et il remplira de ses fruits la face du monde.
7 Je, Bwana amempiga vile alivyowapiga wale waliompiga? Je, yeye ameuawa vile walivyouawa wale waliomuua yeye?
L'a-t-il frappé comme il a frappé ceux qui le frappaient? L'a-t-il tué comme furent tués ceux qu'il avait tués?
8 Kwa vita na kwa kumfukuza unapingana naye: kwa mshindo wake mkali anamfukuza, kama siku ile uvumapo upepo wa mashariki.
Avec mesure, par l'exil vous le châtiez! Il l'a chassé d'un souffle impérieux, en un jour de vent d'Orient.
9 Kwa hili, basi, hatia ya Yakobo itafanyiwa upatanisho, nalo hili litakuwa matunda ya utimilizo wa kuondolewa kwa dhambi yake: Wakati atakapoyafanya mawe yote ya madhabahu kuwa kama mawe ya chokaa yaliyopondwa vipande vipande, hakuna nguzo za Ashera au madhabahu za kufukizia uvumba zitakazobaki zimesimama.
Ainsi donc sera expiée l'iniquité de Jacob, et voici tout le fruit du pardon de son péché: Quand il aura mis les pierres des autels en poudre, comme des pierres à chaux, les aschérahs et les images du Soleil ne se relèveront plus.
10 Mji ulio na boma umebaki ukiwa, makao yaliyotelekezwa, yaliyoachwa kama jangwa. Huko ndama hulisha, huko hujilaza, wanakwanyua matawi yake.
Car la ville forte est devenue une solitude, une demeure délaissée et abandonnée, comme le désert; là paissent les veaux; ils s'y couchent et broutent les rameaux.
11 Wakati vijiti vyake vimekauka, huvunjwa nao wanawake huja na kuwasha navyo moto. Kwa kuwa hili ni taifa lisilo na ufahamu, kwa hiyo yeye aliyewafanya hana huruma juu yao, Muumba wao hawaonyeshi fadhili.
Quand les branches sont sèches, on les brise; des femmes viennent et les brûlent. Car ce n'est pas un peuple sage; c'est pourquoi celui qui l'a fait n'en aura point pitié, et celui qui l'a formé ne lui fera pas grâce.
12 Katika siku ile Bwana atapura kutoka matiririko ya Mto Frati hadi Kijito cha Misri, nanyi ee Waisraeli, mtakusanywa mmoja mmoja.
Et il arrivera en ce jour-là, que Yahweh secouera le blé depuis le cours du Fleuve jusqu'au torrent d'Egypte, et vous serez recueillis un à un, enfants d'Israël.
13 Katika siku ile tarumbeta kubwa italia. Wale waliokuwa wakiangamia katika nchi ya Ashuru, nao wale waliokuwa uhamishoni katika nchi ya Misri watakuja na kumwabudu Bwana katika mlima mtakatifu huko Yerusalemu.
Et il arrivera, en ce jour-là, que sonnera la grande trompette, et ceux qui étaient perdus au pays d'Assur, et ceux qui étaient bannis au pays d'Egypte, reviendront et se prosterneront devant Yahweh, sur la sainte montagne, à Jérusalem.

< Isaya 27 >