< Isaya 27 >
1 Katika siku ile, Bwana ataadhibu kwa upanga wake, upanga wake mkali, mkubwa na wenye nguvu, ataadhibu Lewiathani yule nyoka apitaye kwa mwendo laini, Lewiathani yule nyoka mwenye kujipinda; atamuua joka huyo mkubwa sana wa baharini.
En ce jour-là, Yahvé, avec son épée dure, grande et forte, punira le léviathan, le serpent fuyant, et le léviathan, le serpent tordu, et il tuera le dragon qui est dans la mer.
2 Katika siku ile: “Imbeni kuhusu shamba la mizabibu lililozaa:
En ce jour-là, chantez pour elle: « Une agréable vigne!
3 Mimi, Bwana, ninalitunza, nalinyweshea maji mfululizo. Ninalichunga usiku na mchana ili mtu yeyote asije akalidhuru.
Moi, Yahvé, j'en suis le gardien. Je l'arroserai à chaque instant. De peur que quelqu'un ne l'endommage, je la garderai nuit et jour.
4 Mimi sijakasirika. Licha pangekuwepo michongoma na miiba kunikabili! Ningepambana dhidi yake katika vita, ningeliichoma moto yote.
La colère n'est pas en moi, mais si je trouvais des ronces et des épines, je me battrais! Je marcherais sur elles et je les brûlerais ensemble.
5 Au niwaache waje kwangu kwa ajili ya kupata kimbilio, wao na wafanye amani nami, naam, wafanye amani nami.”
Ou bien qu'il se saisisse de ma force, pour faire la paix avec moi. Qu'il fasse la paix avec moi. »
6 Katika siku zijazo, Yakobo atatia mizizi, Israeli atatoa chipukizi na kuchanua maua, naye atajaza ulimwengu wote kwa matunda.
Dans les jours à venir, Jacob prendra racine. Israël fleurira et bourgeonnera. Ils rempliront de fruits la surface du monde.
7 Je, Bwana amempiga vile alivyowapiga wale waliompiga? Je, yeye ameuawa vile walivyouawa wale waliomuua yeye?
Les a-t-il frappés comme il a frappé ceux qui les ont frappés? Ou bien les tue-t-il comme ont été tués ceux qui les ont tués?
8 Kwa vita na kwa kumfukuza unapingana naye: kwa mshindo wake mkali anamfukuza, kama siku ile uvumapo upepo wa mashariki.
Dans la mesure où tu les renvoies, tu leur fais un procès. Il les a fait disparaître avec son souffle rude, au jour du vent d'orient.
9 Kwa hili, basi, hatia ya Yakobo itafanyiwa upatanisho, nalo hili litakuwa matunda ya utimilizo wa kuondolewa kwa dhambi yake: Wakati atakapoyafanya mawe yote ya madhabahu kuwa kama mawe ya chokaa yaliyopondwa vipande vipande, hakuna nguzo za Ashera au madhabahu za kufukizia uvumba zitakazobaki zimesimama.
C'est pourquoi, par ceci, l'iniquité de Jacob sera pardonnée, et c'est là tout le fruit de l'enlèvement de son péché: qu'il rende toutes les pierres de l'autel comme des pierres de craie battues en pièces, afin que les mâts d'ashère et les autels à encens ne s'élèvent plus.
10 Mji ulio na boma umebaki ukiwa, makao yaliyotelekezwa, yaliyoachwa kama jangwa. Huko ndama hulisha, huko hujilaza, wanakwanyua matawi yake.
Car la ville fortifiée est solitaire, une habitation abandonnée et délaissée, comme le désert. Le veau y paîtra, il s'y couchera, et il consumera ses branches.
11 Wakati vijiti vyake vimekauka, huvunjwa nao wanawake huja na kuwasha navyo moto. Kwa kuwa hili ni taifa lisilo na ufahamu, kwa hiyo yeye aliyewafanya hana huruma juu yao, Muumba wao hawaonyeshi fadhili.
Quand ses rameaux seront desséchés, on les brisera. Les femmes viendront y mettre le feu, car c'est un peuple sans intelligence. C'est pourquoi celui qui les a faits n'aura pas de compassion pour eux, et celui qui les a formés ne leur fera pas de cadeau.
12 Katika siku ile Bwana atapura kutoka matiririko ya Mto Frati hadi Kijito cha Misri, nanyi ee Waisraeli, mtakusanywa mmoja mmoja.
En ce jour-là, l'Éternel frappera depuis le torrent de l'Euphrate jusqu'au ruisseau d'Égypte, et vous serez rassemblés un par un, enfants d'Israël.
13 Katika siku ile tarumbeta kubwa italia. Wale waliokuwa wakiangamia katika nchi ya Ashuru, nao wale waliokuwa uhamishoni katika nchi ya Misri watakuja na kumwabudu Bwana katika mlima mtakatifu huko Yerusalemu.
En ce jour-là, on sonnera de la grande trompette; ceux qui étaient prêts à périr dans le pays d'Assyrie, et ceux qui étaient bannis dans le pays d'Égypte, viendront; et ils se prosterneront devant Yahvé sur la montagne sainte de Jérusalem.