< Isaya 27 >

1 Katika siku ile, Bwana ataadhibu kwa upanga wake, upanga wake mkali, mkubwa na wenye nguvu, ataadhibu Lewiathani yule nyoka apitaye kwa mwendo laini, Lewiathani yule nyoka mwenye kujipinda; atamuua joka huyo mkubwa sana wa baharini.
in/on/with day [the] he/she/it to reckon: punish LORD in/on/with sword his [the] severe and [the] great: large and [the] strong upon Leviathan serpent fleeing and upon Leviathan serpent crooked and to kill [obj] [the] serpent: monster which in/on/with sea
2 Katika siku ile: “Imbeni kuhusu shamba la mizabibu lililozaa:
in/on/with day [the] he/she/it vineyard (delight *LB(AH)*) to sing to/for her
3 Mimi, Bwana, ninalitunza, nalinyweshea maji mfululizo. Ninalichunga usiku na mchana ili mtu yeyote asije akalidhuru.
I LORD to watch her to/for moment to water: watering her lest to reckon: punish upon her night and day to watch her
4 Mimi sijakasirika. Licha pangekuwepo michongoma na miiba kunikabili! Ningepambana dhidi yake katika vita, ningeliichoma moto yote.
rage nothing to/for me who? to give: if only! me thorn thornbush in/on/with battle to step in/on/with her to burn her unitedness
5 Au niwaache waje kwangu kwa ajili ya kupata kimbilio, wao na wafanye amani nami, naam, wafanye amani nami.”
or to strengthen: hold in/on/with security my to make peace to/for me peace to make to/for me
6 Katika siku zijazo, Yakobo atatia mizizi, Israeli atatoa chipukizi na kuchanua maua, naye atajaza ulimwengu wote kwa matunda.
[the] to come (in): come to uproot Jacob to blossom and to sprout Israel and to fill face: surface world fruit
7 Je, Bwana amempiga vile alivyowapiga wale waliompiga? Je, yeye ameuawa vile walivyouawa wale waliomuua yeye?
like/as wound to smite him to smite him if: surely no like/as slaughter to kill his to kill
8 Kwa vita na kwa kumfukuza unapingana naye: kwa mshindo wake mkali anamfukuza, kama siku ile uvumapo upepo wa mashariki.
(in/on/with to drive away *L(abh)*) in/on/with to send: exile her to contend her to remove in/on/with spirit: breath his [the] severe in/on/with day east
9 Kwa hili, basi, hatia ya Yakobo itafanyiwa upatanisho, nalo hili litakuwa matunda ya utimilizo wa kuondolewa kwa dhambi yake: Wakati atakapoyafanya mawe yote ya madhabahu kuwa kama mawe ya chokaa yaliyopondwa vipande vipande, hakuna nguzo za Ashera au madhabahu za kufukizia uvumba zitakazobaki zimesimama.
to/for so in/on/with this to atone iniquity: guilt Jacob and this all fruit to turn aside: remove sin his in/on/with to set: make he all stone altar like/as stone chalk to shatter not to arise: rise Asherah and pillar
10 Mji ulio na boma umebaki ukiwa, makao yaliyotelekezwa, yaliyoachwa kama jangwa. Huko ndama hulisha, huko hujilaza, wanakwanyua matawi yake.
for city to gather/restrain/fortify isolation pasture to send: depart and to leave: forsake like/as wilderness there to pasture calf and there to stretch and to end: destroy cleft her
11 Wakati vijiti vyake vimekauka, huvunjwa nao wanawake huja na kuwasha navyo moto. Kwa kuwa hili ni taifa lisilo na ufahamu, kwa hiyo yeye aliyewafanya hana huruma juu yao, Muumba wao hawaonyeshi fadhili.
in/on/with to wither foliage her to break woman to come (in): come to light [obj] her for not people understanding he/she/it upon so not to have compassion him to make him and to form: formed him not be gracious him
12 Katika siku ile Bwana atapura kutoka matiririko ya Mto Frati hadi Kijito cha Misri, nanyi ee Waisraeli, mtakusanywa mmoja mmoja.
and to be in/on/with day [the] he/she/it to beat LORD from Euphrates [the] river till Brook (Brook of) Egypt and you(m. p.) to gather to/for one one son: descendant/people Israel
13 Katika siku ile tarumbeta kubwa italia. Wale waliokuwa wakiangamia katika nchi ya Ashuru, nao wale waliokuwa uhamishoni katika nchi ya Misri watakuja na kumwabudu Bwana katika mlima mtakatifu huko Yerusalemu.
and to be in/on/with day [the] he/she/it to blow in/on/with trumpet great: large and to come (in): come [the] to perish in/on/with land: country/planet Assyria and [the] to banish in/on/with land: country/planet Egypt and to bow to/for LORD in/on/with mountain: mount [the] holiness in/on/with Jerusalem

< Isaya 27 >